Ni lazima nibaki na msimamo huu pamoja na ukweli kuwa rafiki zangu wamenishauri ni tafakari lakini hii haiwezekani, nilitokea kumpenda binti mmoja ambaye toka yupo kidato cha tatu tumekuwa marafiki.
Baada ya kubainika na wazazi wa binti kuwa mimi ndiye niliyemenya ndizi kwa binti, wazazi wake hawakuwa na papara, makubaliano nikuwa nimtunze, nimsomeshe vinginevyo waende mbele (tulikubaliana niishi naye).
Nilikubali yote, binti alimaliza kidato cha nne kwa bahati akafaulu akaenda kidato cha tano na kumaliza kidato cha sita kwa ufaulu mzuri, pamoja na ugumu wa pesa nilijitahidi aende kwenye Chuo kimoja Kikuu kilichoko mkoa wa Morogoro.
Mambo yalibadilika alipokuwa mwaka wa tatu ambapo alikutana na wajanja wanaojua mapenzi wasiojali kuwa mpaka kufika hapo alipofikia kuna mtu aliteseka na kuhangaika, sikujua kilichoendelea lakini nilihisi kuwa kuna kitu.
Kwanza siku moja usiku wakati tumemaliza kuwasiliana na mpenzi wangu huyu simu yake alisahau kuizima nilisikia kama sauti ya mwanaume ikinon'gona ikimtaka ageuke, lakini baadae kidogo nilisikia binti akisema weka mafuta kwanza.
Kwa namna ya sauti ilivyotoka ilionyesha wazi kuwa mpenzi wangu huyu yupo na mtu na wanafanya mapenzi, baadae simu ilikatika na sikuelewa tena kilichoendelea.
Pamoja na kuwa idadi ya mawasiliano aliyoyokuwa anayafanya kwangu yalipungua sana na mara nyingi nikimpigia simu iliita na hata akipokea alinishauri nimcheki baadaye
Maana wapo kwenye discussion (kumbuka mimi ndiyo mlipaji ada na kila kitu unachojua chuo maana yeye hakupata mkopo kwa asilimia 100).Baada ya binti kurudi likizo nilimuona kama mtu asiye na furaha.
Hata hivyo jioni moja nikamuuliza kuwa mbona amebadilika alinyamaza kimya tu siku ya pili niliporudi kutoka kibaruani akaniambia ana neno lakini nisimuelewe vibaya.
Alianza kwa kuniambia kuwa kwa kweli tumeishi vizuri toka yupo kidato cha tatu na anashukuru kwa moyo wangu wa kusaidia lakini alinieleza kuwa kwakweli huko(chuoni) amepata mtu anampenda na moyo wake ndiyo unampenda na wameshakubaliana wafunge ndoa.
Kwakweli nilisikitika na nilimweleza kuwa anachokifanya sio sawa na kuwa tumetoka mbali nk, kwa kweli hakunisikiliza na kwakuwa wazazi wake hawakai mbali na hapo tulipokuwa tukiishi nilimshauri twende kwa wazani wake ambapo baadaye niligundua kuwa hata wazazi wake wanaunga mkono binti kunibwaga.
Basi binti aliondoka ila kilichotokea ni kuwa ule muda ambao alisema angeolewa hakuolewa aliendelea na Chuo akamaliza na baadaye akarudi mtaani kwao, akijaribu kutafuta kibarua kwa njia mbalimbali, mimi nimekuwa nikiendelea na maisha yangu na kwa bahati Mungu alinishushia neema fulani kwa kweli nafurahia maisha kiasi cha kumiliki kauafiri kangu tena sio ka mkopo.
Majuzi binti amekuja kuniomba radhi kuwa yale yaliyotokea ilikuwa ni shetani tu ila anatubu na kuwa siku zote hapati usingizi akijutia kosa alilolifanya na anajisikia vibaya ukizingatia toka kidato cha tatu mimi ndiye nilikuwa namlipia ada na matumizi yote muhimu, sasa imekuwa ni kero maana hata wazazi wake wanataka nisamehe.
Ila mimi nilishajipanga kivingine pamoja na ukweli kuwa huyu binti wakiitwa warembo hawezi kuacha kutoka lakini nahisi kumrudia ni sawa na kula makombo kauli yangu sasa ni kuwa "katu sitakula makombo hata yawe ya biriani".
Nakaribisha ushauri!
Baada ya kubainika na wazazi wa binti kuwa mimi ndiye niliyemenya ndizi kwa binti, wazazi wake hawakuwa na papara, makubaliano nikuwa nimtunze, nimsomeshe vinginevyo waende mbele (tulikubaliana niishi naye).
Nilikubali yote, binti alimaliza kidato cha nne kwa bahati akafaulu akaenda kidato cha tano na kumaliza kidato cha sita kwa ufaulu mzuri, pamoja na ugumu wa pesa nilijitahidi aende kwenye Chuo kimoja Kikuu kilichoko mkoa wa Morogoro.
Mambo yalibadilika alipokuwa mwaka wa tatu ambapo alikutana na wajanja wanaojua mapenzi wasiojali kuwa mpaka kufika hapo alipofikia kuna mtu aliteseka na kuhangaika, sikujua kilichoendelea lakini nilihisi kuwa kuna kitu.
Kwanza siku moja usiku wakati tumemaliza kuwasiliana na mpenzi wangu huyu simu yake alisahau kuizima nilisikia kama sauti ya mwanaume ikinon'gona ikimtaka ageuke, lakini baadae kidogo nilisikia binti akisema weka mafuta kwanza.
Kwa namna ya sauti ilivyotoka ilionyesha wazi kuwa mpenzi wangu huyu yupo na mtu na wanafanya mapenzi, baadae simu ilikatika na sikuelewa tena kilichoendelea.
Pamoja na kuwa idadi ya mawasiliano aliyoyokuwa anayafanya kwangu yalipungua sana na mara nyingi nikimpigia simu iliita na hata akipokea alinishauri nimcheki baadaye
Maana wapo kwenye discussion (kumbuka mimi ndiyo mlipaji ada na kila kitu unachojua chuo maana yeye hakupata mkopo kwa asilimia 100).Baada ya binti kurudi likizo nilimuona kama mtu asiye na furaha.
Hata hivyo jioni moja nikamuuliza kuwa mbona amebadilika alinyamaza kimya tu siku ya pili niliporudi kutoka kibaruani akaniambia ana neno lakini nisimuelewe vibaya.
Alianza kwa kuniambia kuwa kwa kweli tumeishi vizuri toka yupo kidato cha tatu na anashukuru kwa moyo wangu wa kusaidia lakini alinieleza kuwa kwakweli huko(chuoni) amepata mtu anampenda na moyo wake ndiyo unampenda na wameshakubaliana wafunge ndoa.
Kwakweli nilisikitika na nilimweleza kuwa anachokifanya sio sawa na kuwa tumetoka mbali nk, kwa kweli hakunisikiliza na kwakuwa wazazi wake hawakai mbali na hapo tulipokuwa tukiishi nilimshauri twende kwa wazani wake ambapo baadaye niligundua kuwa hata wazazi wake wanaunga mkono binti kunibwaga.
Basi binti aliondoka ila kilichotokea ni kuwa ule muda ambao alisema angeolewa hakuolewa aliendelea na Chuo akamaliza na baadaye akarudi mtaani kwao, akijaribu kutafuta kibarua kwa njia mbalimbali, mimi nimekuwa nikiendelea na maisha yangu na kwa bahati Mungu alinishushia neema fulani kwa kweli nafurahia maisha kiasi cha kumiliki kauafiri kangu tena sio ka mkopo.
Majuzi binti amekuja kuniomba radhi kuwa yale yaliyotokea ilikuwa ni shetani tu ila anatubu na kuwa siku zote hapati usingizi akijutia kosa alilolifanya na anajisikia vibaya ukizingatia toka kidato cha tatu mimi ndiye nilikuwa namlipia ada na matumizi yote muhimu, sasa imekuwa ni kero maana hata wazazi wake wanataka nisamehe.
Ila mimi nilishajipanga kivingine pamoja na ukweli kuwa huyu binti wakiitwa warembo hawezi kuacha kutoka lakini nahisi kumrudia ni sawa na kula makombo kauli yangu sasa ni kuwa "katu sitakula makombo hata yawe ya biriani".
Nakaribisha ushauri!