Katibu wa CCM tawi kishanje apigwa

Katibu wa CCM tawi kishanje apigwa

KITANGE

Senior Member
Joined
Apr 12, 2013
Posts
138
Reaction score
42
Katika kile kinachoonekana ni kukataliwa CCM kwenye jamii kutokana na ugumu wa hali ya maisha, jana mchana Katibu wa CCM Tawi Kishanje Bukoba Vijijini anayejulikana kwa Jina la Peter Zelamula alipigwa na vijana aliowakuta wakipata kinywaji huku wakitafakari ukali wa maisha. Aliwaambia kuwa tarehe 19.07.2013 kuna wajumbe wa Wilaya toka CCM watafika kijijini kutoa mafunzo ya kuikataa RASIMU YA KATIBA MPYA.

Kwa mujibu wa mtoa habari vijana hao walimuuliza katibu huyo mambo yanayowasibu wakaazi wa kijiji hicho kwa muda mrefu huku CCM wakiangalia bila kujali shida zao za muda mrefu kama zifuatazo.

1. Sheria ya kuwazuia kuvua samaki wakati wao ni wavuvi wa asili, sheria inawalinda wavuvi wakubwa tu wanaovua samaki na kuwapeleka viwandani wananchi wakiambulia mapanki.

2. Juzi walikuwepo maofisa wa samaki kijijini wakawapiga na kuwajeruhi vijana huku wakipora fedha za baadhi ya wananchi kati ya 50,000.00- 200,000.00 kila waliyekutana naye njiani na kumshuku kuwa ni mvuvi, walipasua mitumbwi na kuleta hasara kubwa wa vijana hao.

3. Walitaka awaambie mbona CCM Tawi la kijijini halijachukua hatua zozote kulaani vitendo viovu vya maafisa samaki wanapomkuta na mtu amebeba samaki mmoja huulizwa kampata wapi, na kuchukua hatua za kuwapiga au kuwafungulia mashtaka kwa kupatikana na kitoweo cha samaki.

4. Baada ya katibu kokosa majibu wakati yeye nyumba yake ipo ufukweni mwa ziwa victoria kitongoji Bweza wakaamua kumpa kichapo lakini akaja kuokolewa na jamaa wapita njia.

Kuanzia Alhamis wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya wilaya kutoka kata zote za Wilaya Bukoba wameitwa Bukoba mjini kwa ajili ya kupewa mafunzo ya kuikataa RASIMU YA KATIBA MPYA wakati mabaraza yatakapoanza vikao vyao.

Hayo ndiyo yanayojiri huku Kishanje Bukoba Vijijini.
 
Nashangaa sana kuona wavuvi wadogo wadogo wanapigwa marufuku kuvua samaki kwa ajili ya kitoweo na kuuza. Nijuavyo kwa miaka ya nyuma ziwa Victoria limekuwa likitoa ajira kwa vijana wengi hasa wale wenye elimu ya chini. Hapo cha maana ni kuikataa CCM, basi.
 
Huyo Kiongozi naye ni mbulula tu. Huwezi kuwaambia watu waikatae rasimu ya Katiba bila kutaja sababu za kuikataa. Kipigo ni stahili yake.
 
Kazi nzuri sana!....watanzania wanaanza kupona, ccm imewadanganya kiasi cha kutosha, imewapuuza kiasi cha kutosha.
 
wananchi wameanza kusambaza visago -- haha pole sana kada wa chama twawala.
 
Na mimi nnasema wapigwe tu maana tumechoka-Wananchi nnaona wameipokea hii kauli ya Pinda kwa njia nzuri sana.Kupiga ni njia mojawapo ya kujilinda,piga hao mafisadi wa ccm kwanini hamkumzamisha kwenye maji anywe walau kisado kimoja!!!?.
 
Katika kile kinachoonekana ni kukataliwa CCM kwenye jamii kutokana na ugumu wa hali ya maisha, jana mchana Katibu wa CCM Tawi Kishanje Bukoba Vijijini anayejulikana kwa Jina la Peter Zelamula alipigwa na vijana aliowakuta wakipata kinywaji huku wakitafakari ukali wa maisha. Aliwaambia kuwa tarehe 19.07.2013 kuna wajumbe wa Wilaya toka CCM watafika kijijini kutoa mafunzo ya kuikataa RASIMU YA KATIBA MPYA.

Kwa mujibu wa mtoa habari vijana hao walimuuliza katibu huyo mambo yanayowasibu wakaazi wa kijiji hicho kwa muda mrefu huku CCM wakiangalia bila kujali shida zao za muda mrefu kama zifuatazo.

1. Sheria ya kuwazuia kuvua samaki wakati wao ni wavuvi wa asili, sheria inawalinda wavuvi wakubwa tu wanaovua samaki na kuwapeleka viwandani wananchi wakiambulia mapanki.

2. Juzi walikuwepo maofisa wa samaki kijijini wakawapiga na kuwajeruhi vijana huku wakipora fedha za baadhi ya wananchi kati ya 50,000.00- 200,000.00 kila waliyekutana naye njiani na kumshuku kuwa ni mvuvi, walipasua mitumbwi na kuleta hasara kubwa wa vijana hao.

3. Walitaka awaambie mbona CCM Tawi la kijijini halijachukua hatua zozote kulaani vitendo viovu vya maafisa samaki wanapomkuta na mtu amebeba samaki mmoja huulizwa kampata wapi, na kuchukua hatua za kuwapiga au kuwafungulia mashtaka kwa kupatikana na kitoweo cha samaki.

4. Baada ya katibu kokosa majibu wakati yeye nyumba yake ipo ufukweni mwa ziwa victoria kitongoji Bweza wakaamua kumpa kichapo lakini akaja kuokolewa na jamaa wapita njia.

Kuanzia Alhamis wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya wilaya kutoka kata zote za Wilaya Bukoba wameitwa Bukoba mjini kwa ajili ya kupewa mafunzo ya kuikataa RASIMU YA KATIBA MPYA wakati mabaraza yatakapoanza vikao vyao.

Hayo ndiyo yanayojiri huku Kishanje Bukoba Vijijini.

Ndugu, Mwanza: Kipigo sio tu ni halali na hali haki yao bali pia wanastahili. Jambo la muhimu lilikuwa ni kuambiwa faida na hasara za hiyo rasmu ya katiba alafu wao wananchi (mmoja mmoja) wachambue ambapo watakubaliana na mapendekezo au watayakataa. Pili: Kwa nini wajumbe wa mabaraza wa katiba waitwe na kuelezwa kuikataa rasmu, hivi ni kwa faida ya nani?
 
Kwa faida ya mafisadi wa CCM. Mwigulu na Nape wote ni maskini kama mimi, kwa nini kuendelea kukipigania chama kinachoelekea kufa? Pigaaaaaaa haoooo. Nasema Pigaaa haooo! Mzee Mangula naye kaingia kichwa kichwa, kwa nini hakumuuliza kwanza Nape wakati anajuwa kuwa alipambana akashindwa?
 
ccm biashara yenu imekwisha jamani wananchi kipindi hiki wamebadilika kweli na wanaakili na wanajua kuchagua pia.
 
Kwa style hii ya akili ndogo kutaka kutawala akili kubwa watapigwa sana!!haiwezekani masisiem yanapitisha kampeni za kutaka tuikatae rasimu ya katiba,kwa hoja zipi?haki ya nani hata kama ni mimi nikikutana na hilo gamba na kuniambia huu upuuzi nitatekeleza amri ya pumb..avu immediately maana tumechoka sasa na upuuzi huu wa masisim!!
 
Inapendeza kuona wananchi wanahoji haki zao za msingi.
Tumefika pazuri kama taifa, zamani ilikua kuihoji ccm ni dhambi. siku hizi kuiunga mkono sio tu dhambi ila ni utaila.!!
 
kazi ...ndo inaanza mimi mwenyewe nshasema CCM asijichanganye kabisa....nawachukia mno..
 
Back
Top Bottom