Katibu Mkuu wa CCM, Kinana na timu yake wabisha hodi katika vijiji vya Jimbo la Nachingwea

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Mar 22, 2013
5,536
2,264
Katibu Mkuu wa CCM, Kinana na timu yake wabisha hodi katika vijiji vya Jimbo la Nachingwea
IMG_2360.JPG

Kinana akizungumza na mmoja wa wananchama waasisi wa TANU, aliyejiunga mwaka 1957, Asha Kanduru (89), alipokuwa akitoka kushiriki kulima shamba kwa trekta katika shamba la Umoja Rika katika Kijiji cha Mkotokuyana, Nachingwea
IMG_2382.JPG

Wananchi wa Kijiji cha Naipanga wakimshangilia Katibu Mkuu wa CCM, Kinana wakati akitoa hotuba fupi baada ya ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Serikalai ya Kijiji hicho, wilayani Nachingwea

01.JPG

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisaidia kulima shamba na Mbunge wa Jimbo la Nachingwea ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias Chikawekwa kutumia trekta katika shamba la Umoja Rika katika Kijiji cha Mkotokuyama katika ziara yake ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi wilayani, Nachingwea, Lindi
IMG_2343.JPG

Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akisaidia kung'oa visiki katika shamba la Umoja la Rika baada ya kushiriki kulima kwa kutumia trekta katika Kijiji cha Mkotokuyana, wilayani Nachingwea
IMG_2347.JPG

Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, ambaye pia Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe akisaidia kung'oa visiki katika shamba la Umoja Rika, Nachingwea
IMG_2387.JPG

Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akisaidia kuweka zege katika jengo la Ofisi ya Kijiji cha Naipanga wilayani Nachingwea.
IMG_2409.JPG

Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akizungumza na baadhi ya madereva wa malori waliokuwa wakilalamikia kitendo cha kucheleweshwa upakuaji wa korosho katika maghala hayo.
IMG_2416.JPG

IMG_2420.JPG

Wananchi wakishangilia huku wakiwa na picha ya Katibu Mkuu wa CCM, Kinana alipowasili kwenye Uwanja wa Mashujaa, mjini Nachingwea
IMG_2436.JPG

Katibu Mkuu wa CCM-Taifa, Ndugu Abrahmani Kinana ameitaka Serikali kuchukua hatua kali dhidi ya waliobinafshiwa viwanda nchini sanjali ili wanyang'anywe viwanda hivyo na kurudishwa kuwa mali ya umma.

Hatua hii imekuja mara baada ya Kinana kutembelea na kujionea mlundikano wa korosho na msururu wa magari ya kisubili kupakuliwa, huku moja ya kiwanda cha kubangua korosho na ufuta kikigeuzwa ghala la kuifadhia vifaa vya kusambazaia umeme.

Ndugu Kinana akihutubia kwenye mkutano wa hadhara katika mji mdogo wa Nachingwea Mkoani Lindi, ameitaka serikali kuwawajibisha viongozi au watumishi wa umma ambapo amesema serikali haipaswi kusua sua na kuogopa watu wachache hasa wenye fedha na kuwaacha mamilioni ya watanzania waliowaweka madarakani wakitaabika kupata huduma ambayo wanaitegemea baada ya kuipatia CCM ridhaa ya kuongoza nchi.

Aidha, amewataka viongozi na watendaji, kukubali kukosolewa, kukosoa na kukosoana ili kukiimarisha chama na utendaji ndani ya serikali.

Alisema ni vyema viongozi wakajenga utaratibu huo, ambao utasaidia kukijenga na kukiimarisha chama , pamoja na serikali.

“Hakuna chama ambacho kimejitosheleza, hivyo mnapaswa kukosoana na kurekebishana na yule anayekosolewa asikasirike, hata mimi ninakosolewa ninapokosea, faida ya kukosoana ni kuondoa maovu ndani ya chama, hivyo, kikubwa zaidi muwe na mmeshikamana,” alisema Kinana.

Alisema, CCM kinaweza kuwa chama bora duniani kutokana na kukiimarisha kwa kukosoana

IMG_2422.JPG

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Mashujaa, mjini Nachingwea, pamoja na mambo mengine, aliwahimiza wananchi kujiandikisha na kwenda kupiga kura ili wawachague viongozi wao wanaowataka kupitia CCM katika kuwaletea maendeleo.

Nape Nnauye, amesema kuwa Wananchi wanatakiwa kufanya maamuzi sahihi kwa kukiweka chama hicho madarakani kuanzia ngazi za chini ili kuweza kumalizia miradi waliyoianzisha au ina tija katika maendeleo yao ya baadae.


Nape aliwaambia wananchi kuwa, vyama vya upinzani vilificha maradhi wakati wananchi walikuwa wakivieleza kuwa, vina ugonjwa wa kutokuwa na uwezo wa kupambana na Sera na Ilani za Uchaguzi za CCM kwa sababu kuanzia mwaka 1995, wananchi wengi wamekuwa wakivikataa katika sanduku la kura.

Kushindwa kwa vyama hivyo Katika chaguzi mbali mbali kulisababisha matatizo ndani ya vyama vyao ambayo yalipelekea viongozi wakuu wa vyama vya upinzani kukimbia vivuli vyao na kuunda kikundi wanachokiita UKAWA.


Nape alisema, kwa sasa wameanza kuzungukana. Kuna wengine wamesambaza waraka unaowahimiza viongozi wao mikoani kuhakikisha kila nafasi ya kugombea katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Desemba 14, mwaka huu kuhakikisha wanawekwa wanachama wa chama hicho tofauti na makubaliano waliyowekeana na vyama vilivyo kwenye kikundi cha umoja huo.
 
Kinyume cha ujumbe huu ni futa kabisa ndoto za ukawa na chadema yao... Utaweza wapi mbowe na vilaza wako kudelete ccm. Msahau kabisa ccm ya jenga nchi ccm ndio tegemeo la wanyonge wa nchi hii
hongera kinana na Nape.

Mbowe unapita angani na chopaaaa wenzako wanapita nchi kavu mtaa kwa mtaa kijiji kwa kijiji kata kwa kata wilaya kwa wilaya mkoa kwa mkoa .... Na kwa kutumia barabara na mashua.

Je utaweza jenga chama kwa kupita angani .
 
Safi sana Kinana hayo ndio mambo ambayo tulitegemea CCM iyafanye, CCM pigeni kazi,in has a swap ending kivile lkn mzigo unaopiga Kinana umetisha, inawauma sana wapiga kelele.
 
Kwanini haulizwi maswali ya kwanini anatuhumiwa kuhusika na biashara ya meno ya tembo
 
Kinyume cha ujumbe huu ni futa kabisa ndoto za ukawa na chadema yao... Utaweza wapi mbowe na vilaza wako kudelete ccm.. Msahau kabisa ccm ya jenga nchi ccm ndio tegemeo la wanyonge wa nchi hii
hongera kinana na nape.
Mbowe unapita angani na chopaaaa wenzako wanapita nchi kavu mtaa kwa mtaa kijiji kwa kijiji kata kwa kata wilaya kwa wilaya mkoa kwa mkoa .... Na kwa kutumia barabara na mashua.... Je utaweza jenga chama kwa kupita angani .

Mapovu yote haya ya nini? na tangu lini chama cha mafisadi kikawa tegemeo la wanyonge? au hujui wanyonge hao ndio wanao kufa kwa kukosa matibabu wakati viongozi wa CCM wakienda nje ya nchi kutibu matezi dume?
 
Ila Jamani nasi CCM tumekuwa na siasa za maigizo kama wapinzani..sasa hayo matrekta picha za kushika jembe kulima ama kushika tofali ndio tuseme twajenga nchi sio. Na kwa nini namsikia Katibu Mkuu wetu analalamika ahadi za (Chama) serikali zilizotolewa wakati wa kampeni na Mh Rais (Mweneyekiti wetu) kuwa hazitekelezwi?? Hapo anamhoji Bosi wake kama kashindwa kazi ama..mi naona Nape ndio anafanya la maana yeye ni kuwananga wapinzani tu mwanzo mwisho kwa kila aina ya tusi na masimango..Ila ifike wakati awageukie na mafisadi awanange japo wamo ndani ya Chama chetu walipe kodi ili hizo ahadi zitekelezwe bila hivyo hamna maana ya kuzunguka kufilisi mfuko wa Chama. Ifikie wakati viongozi wa CCM na Serikali yetu tuache kulalamika tufanye maamuzi magumu tuendeleee na tujenge uaminifu zaidi kwa wananchi.

Ni hayo tu MwanaDiwani
 
Kinyume cha ujumbe huu ni futa kabisa ndoto za ukawa na chadema yao... Utaweza wapi mbowe na vilaza wako kudelete ccm.. Msahau kabisa ccm ya jenga nchi ccm ndio tegemeo la wanyonge wa nchi hii
hongera kinana na nape.
Mbowe unapita angani na chopaaaa wenzako wanapita nchi kavu mtaa kwa mtaa kijiji kwa kijiji kata kwa kata wilaya kwa wilaya mkoa kwa mkoa .... Na kwa kutumia barabara na mashua.... Je utaweza jenga chama kwa kupita angani .

Comrade,
Maneno yako ni fikirishi kwa watu wenye fikra pevu.

Tuendelee kuwaonyesha mwanga katika hoja na vitendo hawa mabingwa wa kuongea na ulaghai
 
Ila Jamani nasi CCM tumekuwa na siasa za maigizo kama wapinzani..sasa hayo matrekta picha za kushika jembe kulima ama kushika tofali ndio tuseme twajenga nchi sio. Na kwa nini namsikia Katibu Mkuu wetu analalamika ahadi za (Chama) serikali zilizotolewa wakati wa kampeni na Mh Rais (Mweneyekiti wetu) kuwa hazitekelezwi?? Hapo anamhoji Bosi wake kama kashindwa kazi ama..mi naona Nape ndio anafanya la maana yeye ni kuwananga wapinzani tu mwanzo mwisho kwa kila aina ya tusi na masimango..Ila ifike wakati awageukie na mafisadi awanange japo wamo ndani ya Chama chetu walipe kodi ili hizo ahadi zitekelezwe bila hivyo hamna maana ya kuzunguka kufilisi mfuko wa Chama. Ifikie wakati viongozi wa CCM na Serikali yetu tuache kulalamika tufanye maamuzi magumu tuendeleee na tujenge uaminifu zaidi kwa wananchi.

Ni hayo tu MwanaDiwani
Ndugu,
Wapinzani wamekuja katika ulingo wa siasa na kutukuta tunafanya siasa unazodhani ni maagizo.

Ni siasa hizi hizi unazodhani ni maigizo ndiyo zinaifanya CCM iendelee kupewa ridhaa ya kuingoza nchi kutokana na Sera na Ilani ya Uchaguzi unayodhani ni maagizo.

Endelea kudhani ni maagizo kwa sababu huo ndiyo mtazamo wako.

Tukubali kutokubaliana!

nyerere4.jpeg
 
Mwishoe avunjike mgongo bure, yeye aende akalee wajukuu tu.

Ndugu,
Ni baraka kwa Mwenyezi Mungu kuwa na wajukuu

Kuna wazee wengine ambao ni viongozi wakuu wa vyama bado wanatafuta watoto wakati wana miaka zaidi ya 66 achilia mbali wajukuu.
 
Mikoa ya kusini iko mingapi ? na huko si ndo zilichomwa nyumba za viongozi wa ccm ? na population yao hivi ikoje ?
 
Back
Top Bottom