Katibu Mkuu Mpya Nishati na Madini?

Katibu Mkuu Mpya Nishati na Madini?

JOHN MADIBA

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2011
Posts
251
Reaction score
155
Wizara hii imesababisa waziri mkuu E. Lowassa kujiuzulu, Karamagi na wengine wengi wakati huo hoja kuu ikiwa ni Richmond. Hivi majuzi Katibu mkuu amefukuzwa kazi Bwana Jairo kwa ajili ya rushwa. Na ni wizara inayoipeleka serikali ya JK puta, mchakamchaka, kudhaurauliwa na kupoteza mvuto.
............................................................JE NI KWANINI IMELAANIWA MAWAZO YAKO MUHIMU......................................................................
 
kwani Jairo kafukuzwa kazi? mhh!!!! si PM alipewa maagizo mapya na sasa Jairo kapewa likizo yenye malipo kupisha uchunguzi?
 
Hiyo wizara inataka mtu makini na shupavu ili iende mbele.
 
Yangu leo machache. Ila kwa wale mnaotaka ushahidi wa ujambazi au ufisadi wa Wizara ya Nishati. Ushahidi huu hapa.Nawapa ili kama uchunguzi utamrudisha Jairo kazini muone jinsi CCM ilivyokuwa compromised. Kama hiyo attachment ujionee mwenyewe. JAIRO CAUGHT PANTS DOWN.jpg
 
wizara ya nishati na madini wizara hii imelaaniwa.
 
Ukifatilia sakata la Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, ni wazi kuwa hatua zoote hizi zilizochukuliwa ni za kumpunguza presha ili asife kihoro lakini ukweli ni kwamba huyu jamaa atakaa nje ya post hiyo (japo kwa staili ile ya kumaliza muda wake wa utumishi wa umma). Jambo la msingi hapa ni kuanza kufikiria ni nani atamrithi bw Jairo na atakayeweza kufanya la maana katika hiyo wizara kimeo?

This is the proposed list
1. Christopher Sayi
2. John Haule
3. Eng. Omar Chambo
4..........?
5..........?
 
This is the proposed list
1. Christopher Sayi
2. John Haule
3. Eng. Omar Chambo
4..........?
5..........?

Bwana mipangomingi,
Mimi nasema, jaribu kuwa na fikra huru. Kwanini wewe ukae unafikiria tu watu ambao tayari wapo kwenye system ambayo imeoza? nani kati yao hao unafikiri anaweza kuleta mabadiliko? wote hao ni uozo mtupuuuuu
Tunataka damu changa, ya mabadiliko, yenye uzalendo.
Kama ni suala la kumhamisha mtu toka idara moja hadi ingine, basi aache tu kuteua manake huyo atakua tayari anauzoefu wa kufanya madudu kwenye mtandao wa wezi wa mali za umma
 
mmmmh!kweli hii nchi imeoza kama ndiyo hiyo list umetoa wote ni ''manzi ga nyanza''.Huyo Sayi madudu yake hana tofauti na Jairo ni basi tu Jairo katangulia kunaswa kwenye mtego.Chambooo.....fuswadi lisilo na mpinzani kwa sasa baada ya Gwiji Mgonja kuvunja rekodi nakupitiliza hadi kwa pilato.
 
kwani Jairo kafukuzwa kazi? mhh!!!! si PM alipewa maagizo mapya na sasa Jairo kapewa likizo yenye malipo kupisha uchunguzi?

Sasa hiyo Likizo ya Malipo si ndio wizi wa Kodi za Watanzania? Nchi hii kazi Ufisadi. Mtu alipwe bila ya Kufanyakazi si bora afukuzwe
 
wizara hii imeanza kulaniwa toka Vasco da Gama II alipokuwa waziri. Ndo akaanza mikataba mibovu ya IPTL
 
wizara hii imeanza kulaniwa toka Vasco da Gama II alipokuwa waziri. Ndo akaanza mikataba mibovu ya IPTL

Mkuu hata ukimwita hivyo umemtwika cheo kisicholandana naye..
Vasco aligundua mengi na sehemu nyingi mpya!??
Huyu wetu labda tumuite "Matonya International" maana kwa kutuhemea vibaba...hajambo!
 
Tatizo sio Wizara, Ebu tujaribu pia kuangalia Serikali huenda ndio chanzo cha haya yote. Siamini kama Jairo peke yake ndiye aliyehusika katika hili. JK ajaribu tu pia kuangalia Wizara nzima kwa ujumla, na kama akiiona Wizara iko safi, basi ajiangalie mwenyewe pia huenda ndicho chanzo cha yote
 
kwani Jairo kafukuzwa kazi? mhh!!!! si PM alipewa maagizo mapya na sasa Jairo kapewa likizo yenye malipo kupisha uchunguzi?
Jairo ana likizo ya kula na kuna huku akiingiza siku akisubiri tu kuambiwa kuwa mzee hayo yote ulisingiziwa rudi ofisini kwako.
 
kwani Jairo kafukuzwa kazi? mhh!!!! si PM alipewa maagizo mapya na sasa Jairo kapewa likizo yenye malipo kupisha uchunguzi?
Jairo ana likizo ya kula na kunywa huku akiingiza siku akisubiri tu kuambiwa kuwa mzee hayo yote ulisingiziwa rudi ofisini kwako.
 
Yangu leo machache. Ila kwa wale mnaotaka ushahidi wa ujambazi au ufisadi wa Wizara ya Nishati. Ushahidi huu hapa.Nawapa ili kama uchunguzi utamrudisha Jairo kazini muone jinsi CCM ilivyokuwa compromised. Kama hiyo attachment ujionee mwenyewe.View attachment 34243
Best ulikuwa umelala nini? Ndio unazinduka na kukuta barua juu ya meza.. wenzako wameitafuna kisha kuicheua na sasa imebaki kuwa kinyesi
 
Back
Top Bottom