Katika hatua nyingine, mpasuko ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) umezidi kuendelea baada ya katibu wa chama hicho wilaya ya Arumeru, Hamis Juma Kieni kujiengua katika chama hicho na kujiunga na NRA na jana, alirejesha fomu ya kugombea.
Akizungumza na Mwananchi, Kieni alisema ameamua kujiondoa CUF na kujiunga na NRA baada ya kuona chama hicho, kinatangaza kutosimamisha mgombea bila kuwasiliana na uongozi wa wilaya.
"Mimi nilikuwa nimeweka nia ya kugombea ubunge ila ghafla chama changu kikatangaza kutosimamisha mgombea, nikaona chama sasa kinapoteza mwelekeo na kinaelekea kufa sasa kwanini hawakuwasiliana na sisi na hivyo nikajivua uanachama,"alisema Kieni.
Source:Mwananchi
Akizungumza na Mwananchi, Kieni alisema ameamua kujiondoa CUF na kujiunga na NRA baada ya kuona chama hicho, kinatangaza kutosimamisha mgombea bila kuwasiliana na uongozi wa wilaya.
"Mimi nilikuwa nimeweka nia ya kugombea ubunge ila ghafla chama changu kikatangaza kutosimamisha mgombea, nikaona chama sasa kinapoteza mwelekeo na kinaelekea kufa sasa kwanini hawakuwasiliana na sisi na hivyo nikajivua uanachama,"alisema Kieni.
Source:Mwananchi