Katiba ya CHADEMA na muda wa Uongozi

Katiba ya CHADEMA na muda wa Uongozi

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,348
Reaction score
26,144
Kumekuwa na mijadala isiyokoma kuhusu uchaguzi mkuu ndani ya CHADEMA. Lakini,mijadala mingi imejaa ushabiki,'unazi' na upofu wa sheria inayosimamia uchaguzi huo ndani ya chama. Kama mtanzania mpenda demokrasia nisiye na chama chochote,nimeona heri kudurusu Ibara za Katiba ya sasa ya CHADEMA (humu nitaiita Katiba) inayogusia muda wa uongozi ndani ya chama hicho.

Kwanza, kuna Ibara ya 6.3.2 ya Katiba inayotoa kipindi cha miaka mitano kwa uongozi unaochaguliwa katika Uchaguzi Mkuu. Ibara husika inasomeka hivi:

6.3.2 Muda wa Uongozi
[FONT=Arial,Arial][FONT=Arial,Arial](a) Kila uongozi uliochaguliwa au kuteuliwa wakati wa uchaguzi mkuu wa Chama utashika wadhifa wake kwa kipindi cha miaka mitano.

Pili, Ibara hiyo hiyo ya 6.3.2, katika kifungu (d) inatoa mwanya kwa Mamlaka iliyochhagua au kuteua Uongozi uliopo madarakani kufupisha muda wa uchaguzi. Hapa,kadiri ya uelewa wangu, kuna maana kuwa uchaguzi Mkuu waweza kuitishwa kabla ya miaka mitano husika. Kifungu husika (d) cha Ibara ya 6.3.2 kinasomeka:

(d) Muda wa uongozi unaweza kufupishwa kama mamlaka iliyochagua au kuteua itaamua hivyo.

Hii ina maana kuwa Mamlaka iliyoteua Kamati Kuu,kwa mfano, yaweza kufupisha muda wa Kamati Kuu. Hatahivyo, taratibu nyingine za kawaida za kichama kama vikao husika na sababu za kufanya hivyo lazima ziwepo. Ieleweke kuwa, Ibara ya 6.3.2 (d) inaruhusu Mamlaka fulani inayohusika na uchaguzi au uteuzi wa uongozi fulani ndani ya chama,kufupisha muda wa uongozi huo tu. Si vinginevyo.

Tatu, kuna Ibara ya 6.3.3 ya Katiba. Hii inazungumzia kurekebishwa kwa tarehe ya Uchaguzi ndani ya chama. Hapa,hasa, panazungumziwa kurefusha/kusogeza mbele tarehe ya uchaguzi ndani ya chama. Kamati Kuu ya chama ndiyo iliyopewa mamlaka ya kurekebisha tarehe ya uchaguzi. Kwa uelewa mzuri,naweka hapa Ibara ya 6.3.3 kama ilivyo.Hatahivyo,Ibara ya 6.3.3 (a) na (b) ni muhimu zaidi. Inasomeka:
6.3.3 Kurekebisha tarehe ya Uchaguzi Mkuu wa Chama

[FONT=Arial,Arial][FONT=Arial,Arial](a) Tarehe ya uchaguzi mkuu wa Chama inaweza kurekebishwa kwa kusogezwa mbele kwa muda usiozidi mwaka mmoja toka mwisho wa uhalali wa uongozi uliopo.
(b) Mamlaka ya kufanya marekebisho haya yameachiwa Kamati Kuu
(c) Kamati Kuu ndiyo itapanga tarehe ya uchaguzi wa Mabaraza ya Vijana, Wanawake na Wazee wa Chama.

Itoshe kusema kuwa mijadala na matamko yote yahusuyo uchaguzi ndani ya CHADEMA yaongozwe na uelewa wa Ibara hizo zilizotajwa hapo juu. Kinyume na hapo,ni kujadili na kutamka kwa upofu na upotofu .
[/FONT]
[/FONT]

[FONT=Arial,Arial][FONT=Arial,Arial][/FONT][/FONT]



[/FONT]
[/FONT]
 
Nategemea Kamati kuu makini itapeleka uchaguzi huu mbele.
 
Toa hoja.Toa sababu

Wanachama hatuko tayari kuona Chama chetu kinachezeshwa ngoma na CCM, Tunaamini chama chetu ni cha Kidemocrasia na hivyo Kamati kuu itatumia Madaraka ya kidemocrasia iliyepewa na Katika katiba kutimiza wajibu wake kwa makini.

Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Chadema sio Uchaguzi wa Rais wa Tanzania, tunaimani na Mwenyekiti aliyepo.
 
Wanachama hatuko tayari kuona Chama chetu kinachezeshwa ngoma na CCM, Tunaamini chama chetu ni cha Kidemocrasia na hivyo Kamati kuu itatumia Madaraka ya kidemocrasia iliyepewa na Katika katiba kutimiza wajibu wake kwa makini.

Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Chadema sio Uchaguzi wa Rais wa Tanzania, tunaimani na Mwenyekiti aliyepo.
Now you are talking.Lakini,sisi tunataka mfanye mwaka huu na ikiwezekana kesho ha ha ha ha ha ha ha ha
 
Wanachama hatuko tayari kuona Chama chetu kinachezeshwa ngoma na CCM, Tunaamini chama chetu ni cha Kidemocrasia na hivyo Kamati kuu itatumia Madaraka ya kidemocrasia iliyepewa na Katika katiba kutimiza wajibu wake kwa makini.

Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Chadema sio Uchaguzi wa Rais wa Tanzania, tunaimani na Mwenyekiti aliyepo.

Uchaguzi wa SACCOS ni hadi MTEI aamue maana yeye ndo mwenye kumiliki SACCOS
 
Uchaguzi wa SACCOS ni hadi MTEI aamue maana yeye ndo mwenye kumiliki SACCOS

tumejiandaa madhubuti kuvumilia matusi haya, sababu tunatambua uamuzi wa kutokufanya uchaguzi wa mwenyekiti taifa na pigo la mwisho kwa ccm.
 
Mpaka mbowe astaafu ndipo chadema kifanye uchaguzi kwa sasa mwenye chama hataki.
 
Nategemea Kamati kuu makini itapeleka uchaguzi huu mbele.

Hata ikipeleka mbele haitazidi siku ya uchaguzi. Maana muda halisi wa uchaguzi ni September 2014, one year later should not exceed September 2015,
 
tumejiandaa madhubuti kuvumilia matusi haya, sababu tunatambua uamuzi wa kutokufanya uchaguzi wa mwenyekiti taifa na pigo la mwisho kwa ccm.
Ccm hapa imeingiaje inakufanya usilale kuiwaza ccm bavicha mnavioja.
 
Hata ikipeleka mbele haitazidi siku ya uchaguzi. Maana muda halisi wa uchaguzi ni September 2014, one year later should not exceed September 2015,

Tutavunja katiba, nakubaliana na uchaguzi kufanyika baada ya uchaguzi Mkuu wa Taifa wakati wowote ule, iwe october 2015 au November 2017.
 
Ccm hapa imeingiaje inakufanya usilale kuiwaza ccm bavicha mnavioja.

Uwepo na Uimara wa CDM unapimwa kwa uwepo wa CCM, kazi ya uongozi wa sasa ni kuiondoa CCM Madarakani, mnataka tuubadirishe ili iweje?

Acha kuiwaza, naiota CCM (Jinamizi) karibia kila usiku.
 
Katiba ifuatwe sio ichakachuliwe kwa manufaa ya wachache.........
 
Wanachama wa chadema wenye kadi zetu hatutaki uchaguzi tuna mwenyekiti wetu wa maisha mpaka afe ndo tuchague mwengine tena lazima atoke kwetu atakae taka uchaguzi tunamfukuza,aende kwa maccm yanayotaka uchaguzi.
 
Wanachama wa chadema wenye kadi zetu hatutaki uchaguzi tuna mwenyekiti wetu wa maisha mpaka afe ndo tuchague mwengine tena lazima atoke kwetu atakae taka uchaguzi tunamfukuza,aende kwa maccm yanayotaka uchaguzi.

Pandikizi.
 
napendekeza mbowe awe mwenyekiti milele kama mrema na mzee mapesa....
 
Kuna nini cha msingi cha kusogezea uchaguzi mbele?! Yani hofu tu kwamba zito naye atachukua fomu ya kugombea uenyekiti ndo mnaamua kusogeza mbele mpaka pale mtakapomaliza kumfukuza uanachama ndo muitishe uchaguzi!
 
Back
Top Bottom