mrelbattawy
JF-Expert Member
- Mar 25, 2013
- 564
- 112
Hakuna shaka kua katiba hii ya ccm haina ridhaa ya wananchi wala vyama vikubwa vya upinzani nchini, hii ni katiba ya Ki (DICTATOR) ambayo ufanyaji wa kazi yake utatokana vyombo vya Dola kutumia (Nguvu) zidi ya raia.
Usimamizi wa Katiba hii itakua ni kutumia vyombo vya Dola kushurudisha yani Raia watanza kukamatwa kamatwa na kubambikiziwa makesi ya Luangwa ,chuki za kisiasa zitanza kabuki na chama tawala hakuna shaka kitakua kinavitumia vibaya vyombo vya Dola kwa shuhuli zao za Kisiasa ambalo jambo hilo tumelizowea.
Hivi sasa tayari kuna mikakati kabambe yaku vizibiti vyama vya kisiasa hususani vile vikuu CHADEMA na CUF ili visifurukute na washindwee kufanya shuhuli zao kwa kutumiwa Vyombo vya Dola na CCM , Watabanwa kufanya mikutano ya Hadhara na Mandamono na vyombo vya Dola vitatafuta visingizio na Sababu ili tu washindwee kufanya Shuhuli zao kwa Uwazi .
Tokea mchakato huu kutekwa na CCM tumeshaona wanavyo vitumia vyombo vya Dola vibaya zidi ya raia na hivi sasa kwavile tunaelekea katika kura ya maoni itakayo pingwa na Wananchi wa Tanzania ,basi tutashuhudia unyanyasaji mkubwaa wa vyombo vya Dola zidi ya raia.
Hatuna wasiwasi kua katiba itakikanayo hii na ccm itapita bila kupingwa kwa vile wamehodhi Nyanja zote za udanganyifu mfano tume za Uchaguzi NEC na ZEC na force ya Vyombo vya Dola kufanya kazi za kichama (CCM).
Kwa hio katakana na hali hii nilazima vyama vya upinzani kuanzia sasa Waitangi upya kupambana na CCM na tasisi zake ikiwemoo vyombo ya Dola na mahkama nchini, bila ya kuto kujipanga basi haki aitopatika na kwa kutengemea mahkama wakati zote hizo nikatika tasisi zake CCM.
Jee vyama ya Upinzani mumejifunza nini kuhusu Uchaguzi mkuu wa 2015 haliyakua CCM wamepindua nchana matokeo ya mchakato wa Katiba?
Hakuna shaka kuwa hili lilikua ni funzo zidi yenu kwa njia ya kuelekea uchaguzi mkuu ambao matayarisho yake huanza kabla ya siku kufika ambayo tumebakia na siku chache tu kufika katika uchaguzi mkuu wa 2015 October,
Hivi kwela vyama vya upinzani ccm itakua tayari kuridhika kiungwana kuchindwa na wakatoa Nchi iongozwee na Vyama vya Upinzani ikiwa wameweza kupindua mchakato wa katiba wayside vipi kutumia tasisi zao za tume za Uchaguzi NEC/ZEC kubadilicha matokeo ?,Hii haingii akilini kabisa .
Njia pekeyake ya ccm kuingoa ni kuamua watakavyo ndio tutakavyo na wachezavyo ndivyo tutakavyo cheza , lakini kusema vyama vya upinzani wazitegemee tume za Uchaguzi au kuibiwaa na kusema wakimbilie Mahakamani? Ni kujidanganya na kupoteza muda wao.
Kwa style hii hakuna mahkama itakayo wafanyia haki kwa vile tumezoea kuona tume za uchaguzi ,Vyombo vya Dola na Mahkama vyote ni matawi ya CCM.