Mimibaba
JF-Expert Member
- Jul 1, 2009
- 4,557
- 1,291
Jamani ebu tujadili hoja ya Katiba na Uelewa kwa jamii isiyojua kusoma na kuandika. Tunaweza kufanyeje ili kufikisha ujumbe wa kuwashirikisha hata wasiojua kusoma na kuandika kuchangia mawazo yao kikamilifu. Kikubwa zaidi ni jinsi ya kuwajengea ujasiri na imani ya kutambua michango yao kuwa ni muhimu katika zoezi zima kama sehemu ya ushirikishwaji wa kila mwananchi.