Katiba inamruhusu JK kumpa Ubunge Mbatia

Katiba inamruhusu JK kumpa Ubunge Mbatia

AMARIDONG

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2010
Posts
2,501
Reaction score
189
IBARA YA 55 INAMRUHUSU RAISI KUMTEUA MBATIA KAMA WAZIRI NA KAMA ATAKUWA NAIBU WAZIRI KAMA INAVYOSEMEKAKA NGUVU YAKE ITAKUUWA NDOGO KWANA HATAKUWA MJUMBE WA BARAZA LA MAWAZIRI


55.-(1) Mawaziri wote ambao ni wajumbe wa Baraza la
Mawaziri kwa mujibu wa ibara ya 54 watateuliwa na Rais baada
ya kushauriana na Waziri Mkuu.
(2) Pamoja na Mawaziri waliotanjwa katika ibara ndogo ya (1),
Rais aweza, baada ya kushauriana na Waziri Mkuu, kuwateua
Naibu Mawaziri. Naibu Mawaziri wote hawatakuwa wajumbe wa
Baraza la Mawaziri.
(3) Rais aweza kuteua idadi yoyote ya Naibu Mawaziri ambao
watawasaidia Mawaziri katika utekelezaji wa kazi na shughuli zao.
(4) Mawaziri na Naibu Mawaziri wote watateuliwa kutoka
miongoni mwa Wabunge.
(5) Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo ya (1) ikitokea
kwamba Rais anahitajiwa kumteua Waziri au Naibu Waziri baada
ya Bunge kuvunjwa, basi aweza kumteua mtu yeyote ambaye
alikiwa Mbunge kabla ya Bunge kuvunjwa.
 
Hi Wana JK, Hivi kuna kifungu chochote kwenye sheria zetu kinachomruhusu Rais kuteua wabunge wa upinzani kuwa mawaziri? Thx!!!!!
 
nimekuwa nikijiuliza sana hili, acha wanaojua watasema tukapanua maarifa
 
IBARA YA 55 INAMRUHUSU RAISI KUMTEUA MBATIA KAMA WAZIRI NA KAMA ATAKUWA NAIBU WAZIRI KAMA INAVYOSEMEKAKA NGUVU YAKE ITAKUUWA NDOGO KWANA HATAKUWA MJUMBE WA BARAZA LA MAWAZIRI


55.-(1) Mawaziri wote ambao ni wajumbe wa Baraza la
Mawaziri kwa mujibu wa ibara ya 54 watateuliwa na Rais baada
ya kushauriana na Waziri Mkuu.
(2) Pamoja na Mawaziri waliotanjwa katika ibara ndogo ya (1),
Rais aweza, baada ya kushauriana na Waziri Mkuu, kuwateua
Naibu Mawaziri. Naibu Mawaziri wote hawatakuwa wajumbe wa
Baraza la Mawaziri.
(3) Rais aweza kuteua idadi yoyote ya Naibu Mawaziri ambao
watawasaidia Mawaziri katika utekelezaji wa kazi na shughuli zao.
(4) Mawaziri na Naibu Mawaziri wote watateuliwa kutoka
miongoni mwa Wabunge.
(5) Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo ya (1) ikitokea
kwamba Rais anahitajiwa kumteua Waziri au Naibu Waziri baada
ya Bunge kuvunjwa, basi aweza kumteua mtu yeyote ambaye
alikiwa Mbunge kabla ya Bunge kuvunjwa.


It is a good piece of information. Thank you
 
thank you MINJA kwa kutetea MBATIA

hii haiondoi ile fact aliyosema halima kwamba Mbatia ni kibaraka wa CCM
 
Swali dogo, Ikitokea Chadema wameshinda urais kwa 51% na CCM wakapata 49% ya popular vote, lakini Bungeni majority wabunge CCM kwa tofauti ya viti vichache. Ila CUF, UDP, NCCR ,TLP wabunge wao wanatosha kuipa Chadema majority je Chadema haitahitaji kuwa na mawaziri wa vyama vingine including CCM yenyewe?

Tafakari...
 
Sheria haimbani Raisi katika uteuzi wake wa baraza la mawaziri...anaweza kumchagua mbunge yeyote kuwa waziri either kutoka chama chake au chama cha upinzani sema imezoeleka kuwa chama kinachoshinda mara nyingi kinachagua mawaziri watakaounda serikali kutoka miongoni mwa makada wa chama chake bungeni..raisi akitamani mtu flani ambaye sio mbunge awe waziri huwa anatumia uwezo/ mamlaka yake ya kikatiba kumteua mtu huyo awe mbunge kwanza n then baadae namteua kuwa waziri kwa kuwa tayari ni mbunge...aina ya serikali inayoundwa kwa staili hii ndiyo wanaiita serikali ya mseto...
 
Watu wananishangaza sana; Kama Rais kaamua kumteua Mbatia kwa mamlaka aliyopewa kwenye katiba kuna tatizo gani? Hii ni political maturity; Mbatia ameonyesha nia ya kuwatumikia Watanzania kwa muda mrefu sana. Kagombea Ubunge Kawe, kura hazikutimia. Akaenda Mahakamani, lakini kwa kutumia uungwana wake, akaondosha kesi. Akagombea Afrika Mashariki, mambo hayakuwa mazuri. Sasa Rais, akaona ni vyema aende Bungeni akatoe sauti yake kwenye chombo cha kutunga sheria. Watu hawajaridhika! Hivi kuna kosa Rais kumteua Mbatia? mie naona ni ukomavu wa siasa
 
Watu wananishangaza sana; Kama Rais kaamua kumteua Mbatia kwa mamlaka aliyopewa kwenye katiba kuna tatizo gani? Hii ni political maturity; Mbatia ameonyesha nia ya kuwatumikia Watanzania kwa muda mrefu sana. Kagombea Ubunge Kawe, kura hazikutimia. Akaenda Mahakamani, lakini kwa kutumia uungwana wake, akaondosha kesi. Akagombea Afrika Mashariki, mambo hayakuwa mazuri. Sasa Rais, akaona ni vyema aende Bungeni akatoe sauti yake kwenye chombo cha kutunga sheria. Watu hawajaridhika! Hivi kuna kosa Rais kumteua Mbatia? mie naona ni ukomavu wa siasa
Makame,
Nakuunga mkono sana kwa JMK wetu kutumia ukomavu wake wa kisiasa kumteua Mbatia kuwa Mbunge. Lakini Rais alitengewa nafasi hizi 10 kwenye KATIBA yetu ya JMT ili azitumie vizuri kupata WATANZANIA waadilifu, wachapakazi, thinktanks watakaomsaidia yeye na TAIFA hili ili tusonge mbele. Watu ambao wanaweza kutoa majibu mazuri katika maswali magumu yanayolikabili Taifa hili. Watu ambao hata wakiteuliwa Watanzania wawakubali. Mbatia ni mmoja wao kweli?
Tunao Watanzania wanaostahili teuzi kama hizi. Akina Jenerali, Prof Issa Shivji, Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Samatta, Mzee Mwanakijiji,... Nahisi Rais wetu hazitumii vizuri fursa hizi za kuteua na ndio maana haishi kuunda na kuteua kila wiki kama sio kila siku.
 
Makame,
, Mzee Mwanakijiji,... .

Naomba rekodi ya huyo bwana aliwahi kufanya kazi wapi na alipata mafanikio gani?

Au unataka apewe cheo kwa uhodari wake wa kuleta hoja hapa JF?

Ni nini kinakufanya uamini Shivji na Jenerali wanaweza kuwa viongozi wazuri?
 
Makame,
Nakuunga mkono sana kwa JMK wetu kutumia ukomavu wake wa kisiasa kumteua Mbatia kuwa Mbunge. Lakini Rais alitengewa nafasi hizi 10 kwenye KATIBA yetu ya JMT ili azitumie vizuri kupata WATANZANIA waadilifu, wachapakazi, thinktanks watakaomsaidia yeye na TAIFA hili ili tusonge mbele. Watu ambao wanaweza kutoa majibu mazuri katika maswali magumu yanayolikabili Taifa hili. Watu ambao hata wakiteuliwa Watanzania wawakubali. Mbatia ni mmoja wao kweli?
Tunao Watanzania wanaostahili teuzi kama hizi. Akina Jenerali, Prof Issa Shivji, Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Samatta, Mzee Mwanakijiji,... Nahisi Rais wetu hazitumii vizuri fursa hizi za kuteua na ndio maana haishi kuunda na kuteua kila wiki kama sio kila siku.

Mtu kama Mwanakijiji au Shivji kumpa uwaziri katika serikali ya JK ni kama kumharibu/ku under utilise uwezo wake wa kufikiria...ni vizuri wakafanywa kuwa wakuu wa THINK TANKS flani katika organs za serikalli badala ya wasimamizi wa utendaji katika wizara..haha
 
Back
Top Bottom