Kati ya Magufuli na JK mkweli yupi???

Kati ya Magufuli na JK mkweli yupi???

Lekakui

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
1,451
Reaction score
590
Wana JF,mimi ningeomba tu mwenye ufafanuzi wa hizi tungo tata anisaidie niweze kuelewa kwani kila jambo naona limegeuzwa kuwa siasa,

Wakati mzee wa Kaya alipokuwa anazindua barabara nyingi hapa nchini waziri wake MAGUFULI alikuwa busy kumsifia kwamba barabara zote zimejengwa kwa kutumia mapato ya ndani na zote ni juhudi za mzee wa kaya according to Magufuli,lakini juzi wakiwa kwenye press conference kati yake na Obama mzee wa kaya alipokuwa akijibu maswali alisema MCC ndo iliyofanya kazi ya kujenga barabara nyingi hapa nchini na yote hayo ni matokeao ya uhusiano mzuri kati ta nchi hizi mbili akaenda zaidi na akazitaja kama huko Mtwara ,Songea etc.

Sasa mimi hapa niko puzzled je tumuamini yupi?
Naomba kuwakilisha
 
Nami nilisikia akisema for example road of Namtumbo and Horohoro
 
Ni suala la uelewa tu. Iko miradi inayofanywa kwa fedha za ndani na mingine kwa fedha za nje. Cha msingi barabara zimetengenezwa. Nafikiri katika hili la barabara linahitaji pongezi hata kama tusingetaka kusema ukweli.
 
Jamaa wote waongo tu. Hata barabara hizo zinajengwa kwa kiwango cha lami si kwa lami ndo maana hazidumu.
 
Ni suala la uelewa tu. Iko miradi inayofanywa kwa fedha za ndani na mingine kwa fedha za nje. Cha msingi barabara zimetengenezwa. Nafikiri katika hili la barabara linahitaji pongezi hata kama tusingetaka kusema ukweli.
Je zimejengwa katika viwango vinavyokidhi?mimi nitakushauri kama unaweza safiri kwa barabara kwenda nairobi pita barabara ya Namanga,zote zimejegwa na hazina zaidi ya miaka miwili,utanimbia tofauti,kati ya namanga Kenya na Namanga Tanzania,
Naomba nikalale nitawasikia tena kesho
 
Jamaa wote waongo tu. Hata barabara hizo zinajengwa kwa kiwango cha lami si kwa lami ndo maana hazidumu.

Mchina akujengee kitu cha kudumu ana wazimu? Anamaliza huku kule alikoanzia kunachimbika mshimo. Kitu kingine ni kwamba hii miradi yote ya barabara hapa nchini ndiyo sehemu hawa waheshimiwa wanapiga (wanafisadi) pesa mbaya.
 
Ni suala la uelewa tu. Iko miradi inayofanywa kwa fedha za ndani na mingine kwa fedha za nje. Cha msingi barabara zimetengenezwa. Nafikiri katika hili la barabara linahitaji pongezi hata kama tusingetaka kusema ukweli.
uko sahihi kuna barabara zinajengwa na fedha za ndani,,nikupe taarifa hakuna mradi unaojengwa kwa fedha za ndani unaoisha on time sababu hela zinachelewa kutoka na miradi yote hii serikali inapata hasara kwa sabubu contractor anaomba extension of time ambako lazima gharama inaongezeka mfano,,,lamadi-maswa,nzega-tabora,mradi wa lindi 60km una more than 4 yrs now, na miradi meingine so serikali haina cha kujisifu,miradi yote iliyoisha on time ni ya mkopo.
 
Mkuu si kila barabara imejengwa kwa hela za nje zipo pia zilizojengwa kwa hela za ndani mfano barabara ya Usagara-Geita kanda ya ziwa, hii imejengwa kwa hela za ndani kwa asilimia mia.
 
Mchina akujengee kitu cha kudumu ana wazimu? Anamaliza huku kule alikoanzia kunachimbika mshimo. Kitu kingine ni kwamba hii miradi yote ya barabara hapa nchini ndiyo sehemu hawa waheshimiwa wanapiga (wanafisadi) pesa mbaya.
hapa kosa si la mchina tatizo hapa ni serikali ya ccm(magamba) inapenda vitu vya bei rahisi,wachina wanajenga barabara kutokana na matakwa ya client(government) mchina hawezi jenga nyumba ya zenge aweke paa la vigae wakati kapewa hela ya kujenga nyumba ya suti (tope chini mpaka juu),,,design life span ya barabara zetu ndio sababu,sisi bado tunajenga barabara za surface dressing(flexible pavement) ambazo life span ni 15-20 yrs wakati nchi nyinge wanajenga concrete road(rigid pavement) ambazo life span ni more than 50 yrs ,,ccm kila kitu ni siasa kikwete anaondoka madarakani barabara zote zitakuwa zimekwisha so tutaanza kuingiza gharama za maintenance wakati hata mikopo bado hatujamaliza wote huu ni usanii tu.
 
vioja haviishi...! mara Obama rais wa Tanzania...huyu kajenga hiki ...ili mradi....!
 
Ni suala la uelewa tu. Iko miradi inayofanywa kwa fedha za ndani na mingine kwa fedha za nje. Cha msingi barabara zimetengenezwa. Nafikiri katika hili la barabara linahitaji pongezi hata kama tusingetaka kusema ukweli.


Kama ni pongezi tuipongeze serikali kwa kusanya kodi na siyo kwamba zinakwenda kwa mtu binafsi. Wizara hii imekuwa ikitengeweza fedha nyingi ukilinganisha na wizara nyingine. Lakini hata hivyo hiyo ndiyo kazi ya Serikali baada ya wananchi kulipa kodi. Kuleta maendeleo.
 
Kama ni pongezi tuipongeze serikali kwa kusanya kodi na siyo kwamba zinakwenda kwa mtu binafsi. Wizara hii imekuwa ikitengeweza fedha nyingi ukilinganisha na wizara nyingine. Lakini hata hivyo hiyo ndiyo kazi ya Serikali baada ya wananchi kulipa kodi. Kuleta maendeleo.

Sijakuelewa mkuu labda unisaidie zaidi. Hatuwezi kuipongeza tu serikali kwa kukusanya mapato kama hatuoni matumizi yake. Ndio maana nikasema kwa suala la barabara serikali imejitahidi sana hasa ukitazama kwa mtizamo positive ukubwa wa nchi hii. Suala la wizara kutengewa fedha nyingi au kidogo hiyo sio issue kwani fedha zinagawanywa kulingana na mipango iliyo katika wizara hiyo. Wizara ya ujenzi imetawanyika nchi nzima, unategemea iwe na mgao kidogo wa fedha? Ni vizuri tukawa wakweli pale serikali inapovurunda tuseme lakini inapofanya vizuri pia tuseme. Tusiwe watu wa kulaumu tu kila kitu. Jifikirie hata wewe mwenyewe (sijui umri wako) k.m. kila siku kila unachokifanya kwa mzazi wako ni lawama tu au kwa mwajiri wako ni lawama tu, hakuna hata siku moja hata atakayosema hapa umejitahidi ongeza bidii; utajisikiaje?
 
Je zimejengwa katika viwango vinavyokidhi?mimi nitakushauri kama unaweza safiri kwa barabara kwenda nairobi pita barabara ya Namanga,zote zimejegwa na hazina zaidi ya miaka miwili,utanimbia tofauti,kati ya namanga Kenya na Namanga Tanzania,
Naomba nikalale nitawasikia tena kesho

Suala la ubora wa barabara hilo nakubali kweli kuna sehemu wanachakachua halina ubishi. Hayo ndiyo tunayotakiwa kyapigia kelele wote. Unajua tatizo la ubinafsi wa mtu usiharibu nia yote njema ya serikali. Mhalifu ashughulikiwe kama mhalifu. Usipige kila mtu barabarani kwa kuwa tu kuna kibaka amekuibia simu.
 
Back
Top Bottom