Kati ya kilimo na kuuza mazao kipi kina faida?

Kati ya kilimo na kuuza mazao kipi kina faida?

clementmj

Member
Joined
Jul 13, 2025
Posts
5
Reaction score
12
Habari ya leo ndungu zanguni, Jackson hapa. Naitaji ushauli ndugu zangu

Hivi kati ya kujikita kwenye kilimo au kujikita kwenye kununua mazao kipi kinafaida kubwa? Na kipi kina risk kubwa?

Kwa maoni yako wewe kama wewe let’s say una mtaji wa 20M TZshillings unaweza kuwekeza kwenye kilimo au kwenye kununua Mazao? Thanks in advance!!
 
Nunua mazao itakuwa nzuri zaidi kama una access ya kununua mpunga itakuwa bora zaidi weka stock huku ukisubiri bei ichangamke then koboa mpunga wako uza mchele.
 
Bro hebu tuseme ukweli, kilimo kinaweza kukuingizia mkwanja mrefu ila kinahitaji uvumilivu, muda na mtaji wa maana—mbegu, mbolea, na gharama za kulima. Siku zote kuna risk kama ukame, wadudu au bei kushuka sokoni. Lakini ukiwa na ardhi yako na ukalima kisasa, unaweza kuvuna hadi mamilioni kama utapata soko la uhakika.

Lakini sasa upande wa kuuza mazao, hii ni njia ya haraka kupata pesa bila kulima. Unanunua kwa wakulima kwa bei ya chini msimu wa mavuno, halafu unauza mjini au kwa viwanda kwa bei ya juu. Hapa unatakiwa kuwa mjanja sokoni, ujue bei, muda wa msimu na maeneo ya soko. Faida yake inaweza kuwa ya haraka ukicheza karata zako vizuri. Kwa hiyo, kama huna ardhi wala muda wa kulima, kuuza mazao ni njia laini ya kuingiza hela.
 
Kilimo Bora kabisa ni cha umwagiliaji, hii ya kulima Kwa msimu, mazao yanakutana sokoni, bei unakuwa ya kiwendawazimu.
Mvua zikigoma ndio balaa, hasara huu ya hasara

Kuwa mtu wa kati
 
Kwa 20m bora ununue na kuuza tu
Kilimo kinataka hela ndefu sana, kama umeamua kuingia mazima.

Kilimo kinalipa sana ila na investment iwe kubwa pia.

Kilimo cha umwagiliaji na shamba likiwa kubwa na zana ukiwa nazo kama tractor basi utajiri upo huko.

Pambana na mazao ila napo faida yake unapoyahifadhi kwa mda wa miezi kadhaa

Ila kwa hizo hela anza na kuuza ila usitume mtu nenda mwenyewe field
 
Nielewe vizuri... Hakuna sehemu nimesema ni rahisi kununua mazao mm nimetoa ushauri tuu huwezi kujua mhusika mwenyewe amejipanga vp....
 
Kwa 20m bora ununue na kuuza tu
Kilimo kinataka hela ndefu sana, kama umeamua kuingia mazima.

Kilimo kinalipa sana ila na investment iwe kubwa pia.

Kilimo cha umwagiliaji na shamba likiwa kubwa na zana ukiwa nazo kama tractor basi utajiri upo huko.

Pambana na mazao ila napo faida yake unapoyahifadhi kwa mda wa miezi kadhaa

Ila kwa hizo hela anza na kuuza ila usitume mtu nenda mwenyewe field
Mkuu watu kama wewe mnawarudisha nyuma na kuwavunja moyo sana vijana wenzetu!

Imagine umesema m20 ni ndogo haitoshi kwenye kilimo serious? Kwamba kulima lazima uwe na tractor tu ?

Tractor inalima sh 50-60k kwa heka huwezi kodi ikakulimia?Mimi ni mkulima japo sio mkubwa ni mdogo tu
Basi shemeji yangu huwa analima kwa kukodi mashamba na tractor muda mwingine kwa majembe yanayo kokotwa na ng'ombe mwaka huu kulikuwa na changamoto ya mvua lakini ana magunia 470 ya mpunga utasemaje kulima hadi uwe na trctor tu?
 
Mkuu watu kama wewe mnawarudisha nyuma na kuwavunja moyo sana vijana wenzetu!

Imagine umesema m20 ni ndogo haitoshi kwenye kilimo serious? Kwamba kulima lazima uwe na tractor tu ?

Tractor inalima sh 50-60k kwa heka huwezi kodi ikakulimia?Mimi ni mkulima japo sio mkubwa ni mdogo tu
Basi shemeji yangu huwa analima kwa kukodi mashamba na tractor muda mwingine kwa majembe yanayo kokotwa na ng'ombe mwaka huu kulikuwa na changamoto ya mvua lakini ana magunia 470 ya mpunga utasemaje kulima hadi uwe na trctor tu?
Ni kweli usemalo lakini pia ujue kila mmoja ana mawazo yake
Na hapa ndio mahali pazuri pa kupata ushauri wa pande zote.

Yeye ndio muamuzi wa Mwisho na anasoma comment zetu wote.

Anachambua lipi linamfaa, kama anaona comment yako basi yangu ataiweka kapuni.

Asante kwa masahihisho lakini
 
Mkuu watu kama wewe mnawarudisha nyuma na kuwavunja moyo sana vijana wenzetu!

Imagine umesema m20 ni ndogo haitoshi kwenye kilimo serious? Kwamba kulima lazima uwe na tractor tu ?

Tractor inalima sh 50-60k kwa heka huwezi kodi ikakulimia?Mimi ni mkulima japo sio mkubwa ni mdogo tu
Basi shemeji yangu huwa analima kwa kukodi mashamba na tractor muda mwingine kwa majembe yanayo kokotwa na ng'ombe mwaka huu kulikuwa na changamoto ya mvua lakini ana magunia 470 ya mpunga utasemaje kulima hadi uwe na trctor tu?
Yani kama mi alinivunja moyo sana, nikabaki kimya tuu hata kuchangia mada nikaogopa.
 
Habari ya leo ndungu zanguni, Jackson hapa. Naitaji ushauli ndugu zangu

Hivi kati ya kujikita kwenye kilimo au kujikita kwenye kununua mazao kipi kinafaida kubwa? Na kipi kina risk kubwa?

Kwa maoni yako wewe kama wewe let’s say una mtaji wa 20M TZshillings unaweza kuwekeza kwenye kilimo au kwenye kununua Mazao? Thanks in advance!!
bora kununua, ila uwe na timing nzuri, store, na pia uelewa wa soko.
 
Back
Top Bottom