Kati ya Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi, Wakili Kibatala anasimama na ACT Wazalendo

mkalamo

JF-Expert Member
Sep 7, 2013
324
347
Kwa sasa Kuna mjadala wa kipi kianze Kati ya katiba ya wananchi na Tume huru ya Uchaguzi.

Mvutano mkubwa unaonekana katika vyama viwili vya ACT Wazalendo na Chadema.

ACT Wazalendo wanataka ianze Tume huru ya Uchaguzi katika kuiendea katiba mpya na Chadema wanataka katiba mpya kwenye kuiendea Tume huru.

Mawazo yao yamewaingiza katika uadui mkubwa huku upande wa ACT Wazalendo ukijenga hoja ya kwanini ni muhimu kuanza na Tume huru na Chadema wakiwangooshea vidole na kuwatukana wakati mwingine kuwa wanatumiwa na serikali kuihujumu

Katika hatua hii Kuna makundi ya watu wenye ushawishi wametoa maoni yao.

Miongoni mwao ni Maria Sarungi kupitia bunge la Space anayetaka katiba mpya kwa kuungana na Chadema

Lakini wote hao hawasemi wataifikia vipi katiba mpya kutoka katika kura za wananchi hadi tume ya Sasa yenye jukumu la kuhesabu kura za maoni zitakazopigwa.

Kwa upande wa ACT Wazalendo,mawazo yao yanaungwa mkono na wanasheria nguli wa Chadema, Peter Kibatala na Tundu Lissu kuwa ni muhimu kuanza na Tume huru kabla ya Katiba mpya huku wakielezea sababu zao.

Kibatala amesema katika moja ya mahojiano na Clouds Tv kuwa sheria ya mabadiliko ya katiba ya Jaji warioba inataja tume ya uchaguzi ya Taifa NEC na ZEC kuwa ndiyo watakaosimamia kura za maoni kwenye kuipata katiba mpya.

Anasema hiyo tume isipokuwa huru hata wananchi asilimia 98 wakiwa wamepigwa kura ya kuidhinisha katiba mpya tume hizo zinaweza kupindisha ukweli na wananchi wakapoteza haki zao.

Pia Tundu Lissu kwa mlango wa Nyuma amesema mchakato wa Katiba uanze na ikiwa itafikia Uchaguzi wa 2024-25 katiba ikiwa haijaakamilika basi iundwe Tume huru,itakayosimamia Uchaguzi huo.

Kauli yake hii ambayo kwa namna moja ama nyingine imebeba tahadhari zote za kuzuia ukosolewaji ndani ya chama inaashiria wazi tamanio lake ni kuanza na Tume huru kabla ya Katiba mpya.

Kwa hiyo utaona mitazamo ya ACT Wazalendo na hao wanasheria nguli kwa pamoja kwao muhimu ni TUME huru Kwanza kabla ya Katiba.

Na Kibatala amekuwa muwazi zaidi katika hili tofauti na Lissu,anayesema chaguo lake kwa kuzunguka
 
..michakato ya tume huru na katiba mpya inatakiwa iende kwa pamoja.

..siamini kama ACT hawataki katiba mpya.

..pia siamini kama CDM hawataki tume huru.

..Ni suala la kila upande kuupa nafasi upande mwingine kufikia malengo yake.
 
..michakato ya tume huru na katiba mpya inatakiwa iende kwa pamoja.

..siamini kama ACT hawataki katiba mpya.

..pia siamini kama CDM hawataki tume huru.

..Ni suala la kila upande kuupa nafasi upande mwingine kufikia malengo yake.
ACT wanatumika na CCM
 
Kwa sasa Kuna mjadala wa kipi kianze Kati ya katiba ya wananchi na Tume huru ya Uchaguzi.

Mvutano mkubwa unaonekana katika vyama viwili vya ACT Wazalendo na Chadema.

ACT Wazalendo wanataka ianze Tume huru ya Uchaguzi katika kuiendea katiba mpya na Chadema wanataka katiba mpya kwenye kuiendea Tume huru.

Mawazo yao yamewaingiza katika uadui mkubwa huku upande wa ACT Wazalendo ukijenga hoja ya kwanini ni muhimu kuanza na Tume huru na Chadema wakiwangooshea vidole na kuwatukana wakati mwingine kuwa wanatumiwa na serikali kuihujumu

Katika hatua hii Kuna makundi ya watu wenye ushawishi wametoa maoni yao.

Miongoni mwao ni Maria Sarungi kupitia bunge la Space anayetaka katiba mpya kwa kuungana na Chadema

Lakini wote hao hawasemi wataifikia vipi katiba mpya kutoka katika kura za wananchi hadi tume ya Sasa yenye jukumu la kuhesabu kura za maoni zitakazopigwa.

Kwa upande wa ACT Wazalendo,mawazo yao yanaungwa mkono na wanasheria nguli wa Chadema, Peter Kibatala na Tundu Lissu kuwa ni muhimu kuanza na Tume huru kabla ya Katiba mpya huku wakielezea sababu zao.

Kibatala amesema katika moja ya mahojiano na Clouds Tv kuwa sheria ya mabadiliko ya katiba ya Jaji warioba inataja tume ya uchaguzi ya Taifa NEC na ZEC kuwa ndiyo watakaosimamia kura za maoni kwenye kuipata katiba mpya.

Anasema hiyo tume isipokuwa huru hata wananchi asilimia 98 wakiwa wamepigwa kura ya kuidhinisha katiba mpya tume hizo zinaweza kupindisha ukweli na wananchi wakapoteza haki zao.

Pia Tundu Lissu kwa mlango wa Nyuma amesema mchakato wa Katiba uanze na ikiwa itafikia Uchaguzi wa 2024-25 katiba ikiwa haijaakamilika basi iundwe Tume huru,itakayosimamia Uchaguzi huo.

Kauli yake hii ambayo kwa namna moja ama nyingine imebeba tahadhari zote za kuzuia ukosolewaji ndani ya chama inaashiria wazi tamanio lake ni kuanza na Tume huru kabla ya Katiba mpya.

Kwa hiyo utaona mitazamo ya ACT Wazalendo na hao wanasheria nguli kwa pamoja kwao muhimu ni TUME huru Kwanza kabla ya Katiba.

Na Kibatala amekuwa muwazi zaidi katika hili tofauti na Lissu,anayesema chaguo lake kwa kuzunguka

..hata kwa mtizamo huo haimaanishi kwamba Kibatala hataki katiba mpya.
 
ACT wanatumika na CCM

..lakini kuwa confront ktk hilo haisadii ktk harakati za kupata katiba mpya.

..CCM wanataka vyama vya upinzani vipoteze muda kulumbana badala ya kupigania katiba mpya na tume huru.

..jambo la msingi na kupambania tume huru na katiba mpya kwa pamoja.
 
Kwa upande wa ACT Wazalendo,mawazo yao yanaungwa mkono na wanasheria nguli wa Chadema Peter Kibatala na Tundu Lissu kuwa ni muhimu kuanza na Tume huru kabla ya Katiba mpya huku wakielezea sababu zao.
Je unuthibitisho wa hiki ulicho andika?
 
..michakato ya tume huru na katiba mpya inatakiwa iende kwa pamoja.

..siamini kama ACT hawataki katiba mpya.

..pia siamini kama CDM hawataki tume huru.

..Ni suala la kila upande kuupa nafasi upande mwingine kufikia malengo yake.
Umeongea kiutu uzima sana
 
Utapataje katiba mpya kwa tume isiyohoru ,chadema wanaakili kisoda sana ,ishu ya kura ya maoni bila tume huru ni ujuha

USSR
Simpo sana mbona... Ni kususpend tume iliyopo na kukasimu majukumu hayo kwa tume ya mpito.
Amin amin nawaambia... Tume Huru nje ya Katiba ni nia ovu zaidi! Kumbuka kuwa hiyo tume bado itateuliwa na Rais wa JMT ambaye ni mwenyekiti wa ccm isiyotaka Katiba Mpya.

Kuweni makini sana.
 
..michakato ya tume huru na katiba mpya inatakiwa iende kwa pamoja.

..siamini kama ACT hawataki katiba mpya.

..pia siamini kama CDM hawataki tume huru.

..Ni suala la kila upande kuupa nafasi upande mwingine kufikia malengo yake.
Ukiona hivyo ujue katiba iliyopo haina tatizo!
 
..lakini kuwa confront ktk hilo haisadii ktk harakati za kupata katiba mpya.

..CCM wanataka vyama vya upinzani vipoteze muda kulumbana badala ya kupigania katiba mpya na tume huru.

..jambo la msingi na kupambania tume huru na katiba mpya kwa pamoja.
Sijuhi kwa nini tunaleta mjadala usiokuwa na umuhimu...
Mjadala wa Tume Huru ni sawa na ule wa Muungano ambayo ni miongoni mwa maeneo ya kupigiwa kura.
Kuna vitu viwili hapa... Tume Huru kusimamia uchaguzi mkuu wa 2025.
Na tume huru kusimamia kura za Katiba Mpya. Sheria ya Katiba Mpya iweke wazi kuwa majukumu hayo hayatasimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa sababu ya conflicting interests.
 
Sijuhi kwa nini tunaleta mjadala usiokuwa na umuhimu...
Mjadala wa Tume Huru ni sawa na ule wa Muungano ambayo ni miongoni mwa maeneo ya kupigiwa kura.
Kuna vitu viwili hapa... Tume Huru kusimamia uchaguzi mkuu wa 2025.
Na tume huru kusimamia kura za Katiba Mpya. Sheria ya Katiba Mpya iweke wazi kuwa majukumu hayo hayatasimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa sababu ya conflicting interests.

..wanaotaka malumbano na magomvi ya tume huru vs katiba mpya ni Ccm.

..wapinzani wawe makini ktk hili waepuke kugombana wao kwa wao.
 
Back
Top Bottom