Kuna tatizo kubwa katika uongozi wa rais wa awamu hii. Rais anatumia vibaya madaraka yake kupuuza na "ku-dismiss" tuhuma na malalamiko ya wananchi dhidi ya watu anaowapenda na kuwateua kuwa wasaidizi wake.
Kiongozi anayepingana, kupuuza na kudharau maoni au malalamiko ya wanachi wake hudhihirisha kiburi, majivuno na ubinafsi alionao.
Kujiwekea msimamo kuwa wananchi wote ni "wajinga", bali ni yeye peke yake kama kiongozi mkuu wa nchi ndiye anayejua usahihi wa "mambo ya nchi" ni kujidanganya. Hii ndo tabia ya rais wetu.
Rais wetu mara nyingi amekuwa akifanya maamuzi yanayosigana na matakwa, maoni na mitazamo ya wananchi. Anafanya hivi si kwa bahati mbaya, bali anakusudia mambo yafuatayo;
1. Kuonesha kuwa yeye ndiye mkuu wa nchi na hapangiwi la kufanya kupitia maoni na mitazamo ya watu. Alipomtumbua Nape na Mwigulu kutokana na kujaribu kuwachukulia hatua watu aliowateuwa yeye ilikuwa ni kuonesha "ukuu" wake yeye kama rais na kuwalinda wapendwa wake.
2. Kusafisha tuhuma za mtu anayempenda na kuonesha kuwa mtu huyo hana "madudu" ila tu watu "wanamchafua" kwa nia mbaya dhidi yake. Kwa mfano alipompandisha cheo Mnyeti kutoka DC na kuwa RC ilikuwa ni kuonesha kitendo chake cha kuwashawishi madiwani wa CDM wajiunge CCM kwa ahadi ya vyeo haikuwa rushwa. Mwenyekiti mpya wa Bodi ya VETA, Mtendaji Mkuu wa TPDC na Lugola wote aliwateuwa wakiwa wanakabiliwa na tuhuma za kifisadi katika katika utendaji wao.
3. Ikiwa anayelalamikiwa au kutuhumiwa ni mtu aliyemteuwa yeye, hapendi ionekane kuwa "rais alikosea" katika uteuzi wa mtu huyo. Mfano hai ni kuacha kumtumbua RC Makonda kutokana na tuhuma za kuhujumu uchumi kwa kujaribu kukwepa kodi ya kontena zake bandarini.
4. "Kuwaumiza roho" watu "fulani" kwavile anatambua watu hao wanachukizwa na maamuzi yake kutokana na sababu mbalimbali. Mathalani kuwateuwa wapinzani katika nafasi ambazo walistahili kupewa wana CCM, wapo wana ccm wasiofurahishwa na teuzi hizo kwa wapinzani.
Alipuuzia tuhuma za rushwa dhidi ya Lugola na kumteua kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na leo anamtumbua kwa tuhuma ya rushwa ya Romania. Wananchi hatuna zaidi ya kusema Rais ajifunze kuzingatia maoni, matakwa au malalamiko yetu katika maamuzi mbalimbali anayoyafanya. Bali katika jamii ya watu zaidj ya 50 milioni haiwezekani yeye peke yake ndo mwenye akili ya kujua jema na batili eti kwavile tu ni rais.
Kiongozi anayepingana, kupuuza na kudharau maoni au malalamiko ya wanachi wake hudhihirisha kiburi, majivuno na ubinafsi alionao.
Kujiwekea msimamo kuwa wananchi wote ni "wajinga", bali ni yeye peke yake kama kiongozi mkuu wa nchi ndiye anayejua usahihi wa "mambo ya nchi" ni kujidanganya. Hii ndo tabia ya rais wetu.
Rais wetu mara nyingi amekuwa akifanya maamuzi yanayosigana na matakwa, maoni na mitazamo ya wananchi. Anafanya hivi si kwa bahati mbaya, bali anakusudia mambo yafuatayo;
1. Kuonesha kuwa yeye ndiye mkuu wa nchi na hapangiwi la kufanya kupitia maoni na mitazamo ya watu. Alipomtumbua Nape na Mwigulu kutokana na kujaribu kuwachukulia hatua watu aliowateuwa yeye ilikuwa ni kuonesha "ukuu" wake yeye kama rais na kuwalinda wapendwa wake.
2. Kusafisha tuhuma za mtu anayempenda na kuonesha kuwa mtu huyo hana "madudu" ila tu watu "wanamchafua" kwa nia mbaya dhidi yake. Kwa mfano alipompandisha cheo Mnyeti kutoka DC na kuwa RC ilikuwa ni kuonesha kitendo chake cha kuwashawishi madiwani wa CDM wajiunge CCM kwa ahadi ya vyeo haikuwa rushwa. Mwenyekiti mpya wa Bodi ya VETA, Mtendaji Mkuu wa TPDC na Lugola wote aliwateuwa wakiwa wanakabiliwa na tuhuma za kifisadi katika katika utendaji wao.
3. Ikiwa anayelalamikiwa au kutuhumiwa ni mtu aliyemteuwa yeye, hapendi ionekane kuwa "rais alikosea" katika uteuzi wa mtu huyo. Mfano hai ni kuacha kumtumbua RC Makonda kutokana na tuhuma za kuhujumu uchumi kwa kujaribu kukwepa kodi ya kontena zake bandarini.
4. "Kuwaumiza roho" watu "fulani" kwavile anatambua watu hao wanachukizwa na maamuzi yake kutokana na sababu mbalimbali. Mathalani kuwateuwa wapinzani katika nafasi ambazo walistahili kupewa wana CCM, wapo wana ccm wasiofurahishwa na teuzi hizo kwa wapinzani.
Alipuuzia tuhuma za rushwa dhidi ya Lugola na kumteua kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na leo anamtumbua kwa tuhuma ya rushwa ya Romania. Wananchi hatuna zaidi ya kusema Rais ajifunze kuzingatia maoni, matakwa au malalamiko yetu katika maamuzi mbalimbali anayoyafanya. Bali katika jamii ya watu zaidj ya 50 milioni haiwezekani yeye peke yake ndo mwenye akili ya kujua jema na batili eti kwavile tu ni rais.