Mwafrika wa Kike
JF-Expert Member
- Jul 5, 2007
- 5,185
- 56
Kutoka kwa mwanasheria George Kakoti kwenye jumbe za Tanzanet:
"Inaonekana huyo AG anaamini shule ya sheria kaenda peke yake; wengine wote punda wa dobi. Sasa naaanza kuelewa kwa nini kina Mwakyembe walipendekeza aachie bodi. Ni kweli kampuni ni "mtu" kisheria, tofauti na kiumbe aliyehai kama mimi na wewe. Lakini hiyo inamsaidia mtu kupunguza uwajibikaji katika kesi za madai tu. Haimkwepeshi mhalifu akifanya makosa ya jinai kwa kutumia kampuni. Hata hapa Marekani, ambako wasanii hawaishi kufungua makampuni bandia kwa ajili ya kukwepa kodi na uwajibikaji mwingineo, si rahisi kuvunja sheria kwa kutumia kampuni na wewe kusalimika. Ingekuwa rahisi hivyo kila mtu angefanya.
Kampuni inayo wakurugenzi, maafisa, watumishi na mawakala. Hao wote wanaweza kushitakiwa binafsi na kama wawakilishi na watendaji wa kampuni kutokana na uvunjaji wa sheria zozote zile, ziwe za daawa ama jinai. Hii habari ya ugumu kutokana na kampuni kuwa "mtu" tofauti kisheria n.k ni danganya toto tu. Hiyo kinga ya kampuni (corporate veil) haioni ndani iwapo kosa la jinai limefanyika na maofisa wa kampuni kwa maslahi yao binafsi ama ya kampuni. Kuna kitu kinachoitwa "responsible corporate officer doctrine" ambapo afisa, mkurugenzi ama mtumishi wa kampuni anaweza kushitakiwa kwa ukiukwaji wa sheria uliofanywa na kampuni moja kwa moja ama na mtumishi mwingine wa kampuni. Na hii ni kwa hata makosa madogo ambayo mtu hakufanya yeye mwenyewe bali alitambua ama alipaswa kutambua kuwa sheria inakiukwa lakini hakuchukua hatua yeyote kuzuia ama kutibu/kurekebisha ukiukwaji huu.
Suala la ubadhirifu wa pesa (za umma) ni rahisi zaidi. Maafisa, wakurugenzi, n.k. wanao wajibu mkubwa zaidi kuepukana na makosa ya jinai. Hapa watu wanaoneana haya tu. Kwa taratibu za kifedha, kwa malipo makubwa kiasi hiki kuna mtu alitia saini wakati akichukua cheki kutoka BOT, kuna mtu BOT aliidhinisha kwa maandishi kila pesa zilipotolewa, kuna mtu aliyetia saini wakati akideposit cheki kwenye akaunti benki, na wakati akitoa ama kuhamisha pesa kwenye akaunti ya hiyo kampuni ya kifisadi. Haiwezekani ushahidi wa wizi huu wa kipindi kirefu hivyo ukapotea; kwanza hao jamaa walishajisahau.
Utatuzi si mgumu sana iwapo kuna "political will": ni kuwasweka lupango na kuwafungulia mashtaka wakurugenzi, wanahisa, wafanyakazi na watumishi wote wanaoweza kutambulika wa makampuni hayo feki, halafu unawaacha wajichanganye wenyewe. Tatizo ni kwamba rais wetu ni Muungwana, huwa ha"koromi"! Kwa kuwa kipindi hiki sisi ni vipenzi vya GPB, kama JK anawaonea haya jamaa zetu, kwanini tusiombe "utaalam" kutoka kwa GPB badala ya kuafiki visingizio vya kila siku vya "hatuna wataalam"? (Inaelekea waNorwei wametutolea nje maombi yetu ya kupatiwa "wataalam")."
Mwisho wa kunukuu.
Nakwambia kuna siku watu watakuja kuaibika! kitu kimoja kina Mnyika na wenzake serikalini wanasahau ni kuwa nchi hii sio ile ya mwaka 1964 ambapo wasomi wazawa walikuwa wachache.
Nchi imebadilika jamani punguzeni kudharau watanzania na kuzania kuwa ni watoto au watu wasio na elimu.