Kashfa: Tigopesa wanadhulumu hela za wateja?

hakuna mtandao/company hisiwe na mapungufu ila tigo wamezidi aisee,,niliwai lala na salio la elf2 kwenye simu nikaamka asbh nna mia7
Uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba wafanyakazi wao ni wa kiwango cha chini sana , wengi ni wale wahitimu wa hizi Training college , kama Eagle Training college etc.
 
Ila mimi walonirudishia hata haikufika dk kumi. Nilichokijua ukitaka msaada wa haraka tigo, tumia facebook page yao nyosha maelezokama wapo hewani dk kumi nyingi
 
Niliwahi kupata haya matatizo na huu mtandao na mawazo yangu kiukweli yalikua ni kama ya wengi waliochangia humu ila baada ya maelezo ya kina kutoka kwa mmoja wa mtu ndani niligundua yafuatayo....na kuanzia hapo nilipunguza kulalamika pindi napokosea kufanya muhamala kimakosa.
1.Sababu ya kuchelewa kurudisha pesa uliyotuma kimakosa,au kutoa kimakosa.
-kuna tabia kati yetu watanzania kupata huduma then ukamlipa mhusika kwa tigo pesa then mtu huyo huyo akaenda kupiga simu tigo kuomba zirudishwe,hapa tigo wakiamua kurudisha pesa bila kukoconfirm na receiver kampuni yao lazima iwajibike.
Eg:Mtu kalipa nauli(tax,bus) kwa tigo pesa then akishuka anapiga simu tigo kwamba alikosea,hapa tigo wakirudisha pesa bila kumchek receiver wanakua hawako sahihi.
-pia inatia mashaka kukosea kutuma hela kimakosa kwani process husika inatoa muda kuverifyy jina na number husika
2.Kuhusu kucheleweshewa pesa ili ziibwe na wafanyakazi wa tigo,hii pia sio kweli kabisa....katika taratibu za utumaji na upokeaji pesa kuna wahusika wawili tuu....mtumaji na mpokeaji(sender n receiver),endapo kuna kosa kati ya mmoja wao... Tigo wanachoweza kufanya ni either kurudisha kwa mtumaji au kuziacha kwa mpokeaji....there is no way ukai-divert pesa ya mteja into other number or channel,ndo maana unaona kuna kitu kinaitwa kumbukumbu namba....zile zinatumika kufunga na kurudisha mhumala husika uliokosewa.
NB:kwenye hizi huduma kuna changamoto ya mitandao kudelay na kuleta hasira kwa watumiaji lakini kubwa zaidi ni tabia yetu watumiaji kutokua waaminifu......hizi ni changamoto ambazo zinasababisha kwa kiasi kikubwa delays na baadae mis-interpretation ya huduma za mobile money
 
sasa huyu mteja akipigiwa na akiongopa kuwa "tulikuwa na makubaliano ya kulipana kwa njia ya tigo pesa " nini watafanya?
 
sasa huyu mteja akipigiwa na akiongopa kuwa "tulikuwa na makubaliano ya kulipana kwa njia ya tigo pesa " nini watafanya?
Hapa pesa inakua imezuiliwa(pending),haiko kwa mtumaji wala mpokeaji...mwenye maelezo yenye ushahidi ndie atakaepata....,kwa kawaida muongo ni rahisi kumjua ,kama alietumiwa kimakosa yupo same eneo na mtumaji wanaweza kuombwa kukutana ofisi ya karibu lakini hata kama wapo mbali hua wanaunganishwa pamoja(conference call) hapo muongo utamjuaa tuu.
 
Tatizo linakuja pale Tigo wanapoweka uongo kwamba aliyetumiwa hapatikani wakati yuko hewani .
 
Tigo ni jipu. Ukiweka salio na kama hujajiunga na kifurushi chochote lazima huwa wanakukata tu
 
Voda sijui sa hv kuna siku nilimtumia mtu kimakosa 2.5 saa 11 jioni nilikosa amani sana mana siku hiyo vimeo viliongozana ila Mungu ni mwema nikapiga simu saa moja na nusu hela ikarudi, ila juzi kuna ya tigo nimekosea toka tar 20 mpka leo naambiw nisubir masaa 24 kila siku jibu ni hilo hilo yani
 
Hivi kwanini wanaangaliwa tu ?

Kinachoongelewa na wachangiaji kina ukweli wa 100%,ninasubiri kurejeshewa fedha yangu kwa Zaidi ya wiki mbili sasa.Kuna mtu kauliza swali zuri japoi lina maumivu,hivi kuna watu bado wanatumia tigo.Jibu ni ndiyo tupo kwa kuwa kuna maeneo ndugu zetu waliopo huko hawana mtandao mbadala ukifika ushindani halisi tigo watakuwa na adabu.
 
Ushauri - Tigo ijitoe kwenye mambo ya pesa , itakuja kusababisha umwagaji wa damu .
 
Mtu mmoja usiku wa manane akiwa amelala usingizi mzito saa ile ile Natazama ikatwaliwa laki3 tigoni mwa pesa yake na mjoli aliyetambuliwa kwa jina la Grace Mbaga baada ya ufuatiliaji mkuu sana lakini duru zinaeleza kuwa michezo hiyo ni michezo ya watu wa tigo pesa wenyewe ndipo yule Ndugu aliyetwaliwa fedha yake akalia sana kilio kikuu asiweze kupewa fedha yake hata leo hii na hapo ilikuwa yapata wiki mbili zilizopita.
 
Mimi nilikosea kutuma ela kiasi cha shilingi laki sita na sabini na tano. Hapo hapo nikawapigia simu wakaniambia wameshaizuia na itarudi baada ya masaa 24. Imefika masaa 24 haijarudi nikapiga simu wakaniambia wanashughulikia itarudi baada ya masaa 24. Napo kimya, nilisumbuana nao kila siku kwa siku nne hadi kwenye acount ya facebook. Ndipo baadae wakapiga simu eti tatizo lako linashughulikiwa mpaka tuongee na huyo mtu uliyekosea namba. Nikamshangaa yule mhudumu mbona namba hiyo haipo sasa nyie mumpigie ndio mnirudishie ela yangu wakati mtumaji ni mimi. Akanijibu ndio hivyo akakata simu. Nikakaa baadae nikawapigia simu tena zaidi ya mara tatu wakanijibu tumeshapeleka kwenye dawati linalohusika kurudisha ela. Nikawaacha siku mbili nikaona kimya nikabidi nifunge safari hadi ofisi ya tigo J MALL. kufika pale hata dakika tano haikufika kuirudisha pesa yangu. Nimetoa maelezo na hapo hapo ikarejeshwa. Nikagundua hawa tigo ni wezi
 

Siku ingine ukipata tatizo hilo nenda Tigo shop utasaidiwa.. ila Customer care no 100 hawatoi msaada asilimia 100 just ni sehemu ya kuanzia tu... ila msaada kamili ni tigo shop
 
*Ninachofahamu Mimi ni kwamba,endapo umetuma fedha kwa makosa na kwa bahati mbaya yule ambaye pesa zimeingia kwake akazitoa haraka (Kampuni) huweka mitambo yao katika hali ya alert ili Huyo mtu mara atakapoingiziwa pesa tu huziblock na kuzituma tena kule kwa mlalamikaji./ au aliye mispost ...
*huwa hawana fungu la kurifund zaidi ya kufanya hili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…