Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,701
- 9,779
Inasikitisha sana ndugu zanguni. Nawaombeni wazazi wote tujifunze kupitia huyu mtu
Mimi ni mfanyabiashara wa duka la jumla la nafaka, mwenye frame inayofuata na yeye ni hivyo hivyo. Mwezi ulioisha kuna gari lilikwama mbele ya frame zetu. Sasa kukawa na Bajaj iliyokuwa inajaribu kupenyeza kurudi nyuma, muda huo huo kuna kijana alibebelea gunia la mchele akikatiza kwenye upenyo huo huo.
Wakati anaikaribia ile Bajaj, aliamua kujibana kuelekea upande ambao wa frame ya jirani yangu, huyu jirani yangu alimsukumiza kijana kwa mgongo, yule kijana katika hali ya kuyumba yumba, alishtukia mguu wake umekanyagwa na Bajaj ile iliyokuwa na magunia kadhaa ya unga kwenye bodi
Kijana aliangua kilio kisicho na kifani, huku mifupa ya kikanyagio chake cha mguu ikiwa nyang'a nyag'a. Jirani yangu alijibu kwa jeuri kuwa kwani alikuwa anawahi nini. Tukio ni la mwezi ulioisha
Juzi kati, mtoto wa kike wa huyo jirani yangu alipakizwa kwenye bodaboda kama ilivyo ada ya kupelekwa shuleni kwa usafiri wa kitajiri. Taarifa mbaya zilitufikia kuwa bodaboda imepata ajali ilipokuwa inafanya juhudi ya kukwepa tandam ya Mahindi. Cha kushangaza bodaboda alichubuka vibaya sana na asivunjike, lakini mtoto alivunjika miguu yote na kuwa pingili pingili. Tulimbeba mgonjwa wetu na kumpeleka hospitali
Leo asubuhi wakati nafungua kijiduka changu cha kimaskini, ndipo kupata taarifa kuwa mguu mmoja wanaunofoa kabisa
Funzo: Malipo yote ni hapahapa duniani. Tenda yale unayopenda kutendewa na wenzio. Epuka matendo maovu ili usije kuingiza wasiohusika kwenye karma yako
Kosa lake yeye, karma kwa mtoto. Inasikitisha sana aisee. Nani atamuoa?
Pia soma: Kama mwenyezi Mungu atatupilia mbali suala la laana na karma, watakaoingia kwenye adhabu ya milele watakuwa wameonewa bure
Mimi ni mfanyabiashara wa duka la jumla la nafaka, mwenye frame inayofuata na yeye ni hivyo hivyo. Mwezi ulioisha kuna gari lilikwama mbele ya frame zetu. Sasa kukawa na Bajaj iliyokuwa inajaribu kupenyeza kurudi nyuma, muda huo huo kuna kijana alibebelea gunia la mchele akikatiza kwenye upenyo huo huo.
Wakati anaikaribia ile Bajaj, aliamua kujibana kuelekea upande ambao wa frame ya jirani yangu, huyu jirani yangu alimsukumiza kijana kwa mgongo, yule kijana katika hali ya kuyumba yumba, alishtukia mguu wake umekanyagwa na Bajaj ile iliyokuwa na magunia kadhaa ya unga kwenye bodi
Kijana aliangua kilio kisicho na kifani, huku mifupa ya kikanyagio chake cha mguu ikiwa nyang'a nyag'a. Jirani yangu alijibu kwa jeuri kuwa kwani alikuwa anawahi nini. Tukio ni la mwezi ulioisha
Juzi kati, mtoto wa kike wa huyo jirani yangu alipakizwa kwenye bodaboda kama ilivyo ada ya kupelekwa shuleni kwa usafiri wa kitajiri. Taarifa mbaya zilitufikia kuwa bodaboda imepata ajali ilipokuwa inafanya juhudi ya kukwepa tandam ya Mahindi. Cha kushangaza bodaboda alichubuka vibaya sana na asivunjike, lakini mtoto alivunjika miguu yote na kuwa pingili pingili. Tulimbeba mgonjwa wetu na kumpeleka hospitali
Leo asubuhi wakati nafungua kijiduka changu cha kimaskini, ndipo kupata taarifa kuwa mguu mmoja wanaunofoa kabisa
Funzo: Malipo yote ni hapahapa duniani. Tenda yale unayopenda kutendewa na wenzio. Epuka matendo maovu ili usije kuingiza wasiohusika kwenye karma yako
Kosa lake yeye, karma kwa mtoto. Inasikitisha sana aisee. Nani atamuoa?
Pia soma: Kama mwenyezi Mungu atatupilia mbali suala la laana na karma, watakaoingia kwenye adhabu ya milele watakuwa wameonewa bure