TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Katika mambo ambayo yameongeza mvuto wa shughuli za kisiasa hapa nchini, ni kile kinachoonekana kuwa Chama Cha Mapinduzi kushika hatamu katika kuonyesha dira ya uongozi wa shughuli za kisiasa hapa nchini. Hatua hiyo imefikiwa baada ya Chama Cha Mapinduzi kufanya mabadailiko katika safu yake ya uongozi kuanzia ngazi za juu mpaka ngazi za kata na mashina.
Kimsingi ni kwamba hali ya siasa ndani ya chama cha Mapinduzi imeendelea kuwa shwari na ya Utulivu ambayo inawapa fursa viongozi wa chama hiko kufanya kazi kwa ushirikiano na umoja zaidi tofauti na kipindi cha nyuma ambapo makundi yalikaribia kukiangamiza chama hiko kikongwe hapa nchini.
Mafanikio ambayo yanaonekana kupatikana ni pamoja na kuongezeka kwa kasi ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, ambapo kumekuwepo na kasi inayoridhisha ya utekelezaji wa ahadi zake na pia usimamizi makini wa shughuli za serikali katika kuwaletea Maendeleo wananchi.
Kuanzia Mawaziri, Mananibu, Wakuu wa Idara na vitengo Serikalini, wakuu wa mikoa na ma_DC pamoja na wakurugenzi wamegeuka kwa wachapa kazi hodari chini ya usimamizi wa viongozi wa CCM ambao hupita kufanya ziara na kutoa maagizo mbalimbali ya utekelezaji na utatuzi wa kero za wananchi katika maeneo hayo. Ma-DC wapya ambao wengi wametokana na UVCCM, wamekuwa mstari wa mbele katika kusimamia ILANI ya Chama katika ngazi za wilaya wakishirikiana na wa_NEC wa Wilaya pamoja na Wenyeviti wa Chama Wa wilaya wa UVCCM na CCM.
Kasi hii imeongezeka na kutia faraja zaidi kwa chama cha Mapinduzi kufuatia matukio ya Vijana wa Chadema kuuona na kuushuhudia ulaghai mkubwa wa Chama hiko, na hivyo kuamua kuamia CCM makundi kwa makundi, tumeshuhudia Matukio ya Kuhama kwa Mwenyekiti wa Chadema UK, Lukosi na Safu yake ya uongozi na kurudi CCM, tumeshuhudia SHONZA makamu mwenyekiti wa BAVICHA taifa akijiunga na CCM, akiongozana na MTELA na wengineo, tumekuwa tukipata taarifa kila kukicha ya vijana kuhamia CCM hata katika yale maeneo ambayo upinzani umeonekana kuwa ni ngome yao kama mikoa ya Kilimanjaro na Arusha pamoja na Manyara.
Matukio ambayo yamekuwa kivutio cha wengi na hasa baada ya Vijana hao kupata nafasi ya kuieleza hadhira juu ya sababu zao za msingi zilizowakimbiza Chadema ambapo walitaja kuwa ni Ubaguzi uliokithiri na Upendeleo, ambapo wengi wao walieleza kinagaubaga kuwa Chama hiko ni cha wanaharakati na wala si chama ambacho kinaviongozi makini na watawala wenye hekima.
"Chadema haina viongozi wala watawala bali ni kikundi cha wanaharakati ambao wanaendesha harakati zao kwa maslahi binafsi na ubaguzi mkubwa" aliwahi kusikika Mtela Mwampamba ambae alikuwa ni Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Mbeya.
Kwa wale ambao wanawafahamu watu kama LUKOSI, MWAMPAMBA, SHONZA, ABDUL ISSA n.k na harakati zao na mikakati yao ya kuieneza na kuiimarisha CHADEMA hapa nchini, wamepigwa na butwaa baada ya matukio haya ya watu hao kuihama chadema, lakini wengi wameshtushwa zaidi na taarifa hizo juu ya kinachoendelea Chadema, na wanajiuliza hatma ya Chama hiko ni ipi.?
Pamoja na sababu nyingine pia vijana hao walifikia Uamuzi huo wa kukihama chama hiko baada ya kupigania kusimamisha Demokrasia ya kweli ndani ya Chadema na kupinga ukiukwaji wa Katiba, Kanuni na Taratibu uliokuwa ukifanywa na "viongozi wakuu" wa Chadema.
WanaCCM wote pamoja na Mimi tunawapongeza vijana hawa kwa uamuzi wao ambao wenyewe wameutambua kuwa ni "uamuzi sahihi" na kila mmoja katika sisi tumekiri kuwa uamuzi uliofanywa na vijana hawa ni uamuzi sahihi tena ulio thabiti ambao kila kijana ambae anafikiri sawasawa anatakiwa kuuchukua.
Pamoja na pongezi hizo, tuchukue fursa hii kuwataka vijana ambao wanajitoa kuijenga na kuitetea CHADEMA kuona hatari inayoendelea Chadema na hasa baada ya kudhihirika sura yao kamili kwenye macho ya watanzania, kwa yale yaliyobainishwa na Vijana hawa waliohama huko lakini pia haya yaliyoibuliwa katika mitandao na kuwafanya baadhi ya viongozi waandamizi wa chama hiko kuwekwa chini ya Ulinzi.
Umefika wakati sasa wa vijana kukihama na kujiepusha kabisa na shughuli zote zisizo na nia njema na Taifa zinazofanywa na Chadema na kutafuta Chama kingine ambacho kinasimamia Uadilifu, Ukweli, Haki na Nidhamu ya kweli kama CCM.
Karibuni CCM, Chama kinachotoa fursa sawa kwa wanachama wake na kuthamini wanachama kulingana na michango yao na huduma yao kwa Chama.
Kimsingi ni kwamba hali ya siasa ndani ya chama cha Mapinduzi imeendelea kuwa shwari na ya Utulivu ambayo inawapa fursa viongozi wa chama hiko kufanya kazi kwa ushirikiano na umoja zaidi tofauti na kipindi cha nyuma ambapo makundi yalikaribia kukiangamiza chama hiko kikongwe hapa nchini.
Mafanikio ambayo yanaonekana kupatikana ni pamoja na kuongezeka kwa kasi ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, ambapo kumekuwepo na kasi inayoridhisha ya utekelezaji wa ahadi zake na pia usimamizi makini wa shughuli za serikali katika kuwaletea Maendeleo wananchi.
Kuanzia Mawaziri, Mananibu, Wakuu wa Idara na vitengo Serikalini, wakuu wa mikoa na ma_DC pamoja na wakurugenzi wamegeuka kwa wachapa kazi hodari chini ya usimamizi wa viongozi wa CCM ambao hupita kufanya ziara na kutoa maagizo mbalimbali ya utekelezaji na utatuzi wa kero za wananchi katika maeneo hayo. Ma-DC wapya ambao wengi wametokana na UVCCM, wamekuwa mstari wa mbele katika kusimamia ILANI ya Chama katika ngazi za wilaya wakishirikiana na wa_NEC wa Wilaya pamoja na Wenyeviti wa Chama Wa wilaya wa UVCCM na CCM.
Kasi hii imeongezeka na kutia faraja zaidi kwa chama cha Mapinduzi kufuatia matukio ya Vijana wa Chadema kuuona na kuushuhudia ulaghai mkubwa wa Chama hiko, na hivyo kuamua kuamia CCM makundi kwa makundi, tumeshuhudia Matukio ya Kuhama kwa Mwenyekiti wa Chadema UK, Lukosi na Safu yake ya uongozi na kurudi CCM, tumeshuhudia SHONZA makamu mwenyekiti wa BAVICHA taifa akijiunga na CCM, akiongozana na MTELA na wengineo, tumekuwa tukipata taarifa kila kukicha ya vijana kuhamia CCM hata katika yale maeneo ambayo upinzani umeonekana kuwa ni ngome yao kama mikoa ya Kilimanjaro na Arusha pamoja na Manyara.
Matukio ambayo yamekuwa kivutio cha wengi na hasa baada ya Vijana hao kupata nafasi ya kuieleza hadhira juu ya sababu zao za msingi zilizowakimbiza Chadema ambapo walitaja kuwa ni Ubaguzi uliokithiri na Upendeleo, ambapo wengi wao walieleza kinagaubaga kuwa Chama hiko ni cha wanaharakati na wala si chama ambacho kinaviongozi makini na watawala wenye hekima.
"Chadema haina viongozi wala watawala bali ni kikundi cha wanaharakati ambao wanaendesha harakati zao kwa maslahi binafsi na ubaguzi mkubwa" aliwahi kusikika Mtela Mwampamba ambae alikuwa ni Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Mbeya.
Kwa wale ambao wanawafahamu watu kama LUKOSI, MWAMPAMBA, SHONZA, ABDUL ISSA n.k na harakati zao na mikakati yao ya kuieneza na kuiimarisha CHADEMA hapa nchini, wamepigwa na butwaa baada ya matukio haya ya watu hao kuihama chadema, lakini wengi wameshtushwa zaidi na taarifa hizo juu ya kinachoendelea Chadema, na wanajiuliza hatma ya Chama hiko ni ipi.?
Pamoja na sababu nyingine pia vijana hao walifikia Uamuzi huo wa kukihama chama hiko baada ya kupigania kusimamisha Demokrasia ya kweli ndani ya Chadema na kupinga ukiukwaji wa Katiba, Kanuni na Taratibu uliokuwa ukifanywa na "viongozi wakuu" wa Chadema.
WanaCCM wote pamoja na Mimi tunawapongeza vijana hawa kwa uamuzi wao ambao wenyewe wameutambua kuwa ni "uamuzi sahihi" na kila mmoja katika sisi tumekiri kuwa uamuzi uliofanywa na vijana hawa ni uamuzi sahihi tena ulio thabiti ambao kila kijana ambae anafikiri sawasawa anatakiwa kuuchukua.
Pamoja na pongezi hizo, tuchukue fursa hii kuwataka vijana ambao wanajitoa kuijenga na kuitetea CHADEMA kuona hatari inayoendelea Chadema na hasa baada ya kudhihirika sura yao kamili kwenye macho ya watanzania, kwa yale yaliyobainishwa na Vijana hawa waliohama huko lakini pia haya yaliyoibuliwa katika mitandao na kuwafanya baadhi ya viongozi waandamizi wa chama hiko kuwekwa chini ya Ulinzi.
Umefika wakati sasa wa vijana kukihama na kujiepusha kabisa na shughuli zote zisizo na nia njema na Taifa zinazofanywa na Chadema na kutafuta Chama kingine ambacho kinasimamia Uadilifu, Ukweli, Haki na Nidhamu ya kweli kama CCM.
Karibuni CCM, Chama kinachotoa fursa sawa kwa wanachama wake na kuthamini wanachama kulingana na michango yao na huduma yao kwa Chama.