Samaki amezichambo,kasahau kuna papa,
hula hata kilimbo,japo si wake kikwapa,
vuvi lambwa vuvi rembo,ndoano sio mshipa,
Tembelea kimwaloni,ujue neno jivuni,
Ela uvuvi wa juya, kuvua siutamani
Sababuye 'takwambiya, ufahamiwe mwendani
Ni kwambakwe huingiya, samaki waso thamani
Jabali hulijilisi, jishipi ukilitupa
Na nivuapo maziyo, mavuvi ya kizamani
Kwa hino hali niliyo, huvua kwa kutamani
Hatafuta kiteweyo, cha wali mwema kombeni
Mshipi ukishimeli, samaki hutapatapa
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.