Karibu tutafakari!

Karibu tutafakari!

Jaguar

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2011
Posts
3,440
Reaction score
1,029
Una ndoo mbili,A na B.Ndoo A ina lita mbili za vinegar na ndoo B ina lita mbili za maji.Chukua lita moja ya vinegar kutoka ndoo A kisha changanya na lita mbili za maji katika ndoo B.Changanya vizuri kisha chukua lita moja ya mchanganyiko wa (vinegar-water) kutoka ndoo B,imimine katika ndoo A halafu changanya vizuri.SWALI;Ndoo A ina maji mengi au ndoo B ina vinegar nyingi?
 
Ndoo A ina Vinegar nyingi na ndoo B ina maji mengi.
 
ndoo A itakua na vnager nyingi kuliko maji na ndoo B itakua na maji mengikuliko vinager.
ila, ndoo A itakua na maji pia, na wakati huohuo ndoo B itakua na vinager pia.
 
Labda nifafanue zaidi,originally ndoo A ilikuwa na vinegar na ndoo B ilikuwa na maji,je vinegar iliyohamia kwenye maji ni nyingi kuliko maji yaliyohamia kwenye vinegar?au vice-versa? au ni sawa sawa?
 
Ndoo A ina Vinegar nyingi na ndoo B ina maji mengi.
Sawa mkuu umenijibu,lakini nilichotaka mimi ni comparison ya kiwango cha vinegar iliyomo katika ndoo B dhidi ya kiwango cha maji yaliyomo katika ndoo A.tatizo hili swali unalipa mtazamo rahisi saana!
 
Mi naona mchanganyiko ni ule ule ingawaje ndoo A itakua na vinegar nyng kdogo kwa sababu ule mchanganyko kutoka kwenye B hautaingia wote, lazima ndoo b itabak na unyevu kwa hyo mchanganyko umepungua. Ila point ni kwamba una mchanganyko wa lita 2 za maji na lita 2 za vinegar, jumla lita 4. Nimekujibu mkuu?
 
Au swali tulirahisishe zaidi,tafuta concentration ya maji katika ndoo A na concentration ya vinegar katika ndoo B yenye maji.Concentration ya maji katika ndoo A tuiite X na concentration ya vinegar katika ndoo B tuiite Y.Mwisho.compare X and Y.
 
dah mi naona maluweluwe tu, nimeshasahau chemistry (method of mixture) ndo nilikuwa natumia kusolve maswali ya kinamna hiyo.
 
Ndoo A concetration ya Vinegar itakuwa 1.66 Lt na ndoo B concetratin ya Vinegar itakuwa 0.66Lt...

So ndoo A ina maji 0.34Lt na ndoo B ina Maji 1.34Lt
 
Mentor mbona unasemaga Jaguar hatoagi Senkyuuuu au hujawahi patia nini.....
 
Back
Top Bottom