kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,247
- 16,169
Watu wetu hawajui kufanya biashara, hawamjali mteja, hawajui kuweka kumbukumbu. Miaka 20 mtu amebaki kuwa machinga. Watu wetu wanapata uzoefu wa kuuza kutoka kwao. Kuwafukuza wachina na wageni tutawadumaza watu wetu na waendelee kutoa huduma mbaya kwa wateja
TFF iliporuhusu wachezaji 12 kwa timu Moja vijana wetu walipata uzoefu mkubwa kutoka kwa wageni. Kila golikipa sasa hivi anadaka kama Diara na Camara.
Utakuwa ujinga kama tutasema waondoke ili watu wetu wafanye hizo biashara, watakuwa machinga milele na kutoa huduma mbovu kwa wateja wao. Hata ukienda bar watu wetu hawajui kuwahudumia wateja wao.
Unapochangamana na mchina au mgeni tumia hiyo fursa kuuliza na kujifunza badala ya kumchukia na kulalamika na kukodoa macho kodo eti aondoke ili wewe uendelee na uvivu wako na lugha mbaya yako kwa wateja; koma kabisa.
Kondacta wa daladala anawasokomeza watu kwenye daladala huku akiwaambia kama hutaki piga chini, daladala halijai kama ndoo ya maji huku akipita katikati yao kuwapanga na kukusanya nauli na nguo zake chafu. Vipi kama akija kondacta mchina na madaladala yake akaja na level seat akiwa amevalia suluali nyeusi na shati jeupe la mikono mirefu na tai yake shingoni?
TFF iliporuhusu wachezaji 12 kwa timu Moja vijana wetu walipata uzoefu mkubwa kutoka kwa wageni. Kila golikipa sasa hivi anadaka kama Diara na Camara.
Utakuwa ujinga kama tutasema waondoke ili watu wetu wafanye hizo biashara, watakuwa machinga milele na kutoa huduma mbovu kwa wateja wao. Hata ukienda bar watu wetu hawajui kuwahudumia wateja wao.
Unapochangamana na mchina au mgeni tumia hiyo fursa kuuliza na kujifunza badala ya kumchukia na kulalamika na kukodoa macho kodo eti aondoke ili wewe uendelee na uvivu wako na lugha mbaya yako kwa wateja; koma kabisa.
Kondacta wa daladala anawasokomeza watu kwenye daladala huku akiwaambia kama hutaki piga chini, daladala halijai kama ndoo ya maji huku akipita katikati yao kuwapanga na kukusanya nauli na nguo zake chafu. Vipi kama akija kondacta mchina na madaladala yake akaja na level seat akiwa amevalia suluali nyeusi na shati jeupe la mikono mirefu na tai yake shingoni?