Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 6,160
- 11,228
Wakuu najiuliza kwanini mamlaka haziweki miundombinu vizuri Karikoo yote, baadhi ya mitaa miundombinu imechakaa kana kwamba pale si kitu cha Biashara nchini na nchi jirani.
Barabara nyingi mbovu kupindukia, wakati wa mvua hapatamaniki zinajaa madimbwi, matope mpaka kero.
Miundombinu ya maji taka ndio hatari zaidi, ni kawaida majitaka yanayonuka kinyesi kutiririka mtaani huku wafanyabiashara wakiendelea na shughuli zao. Kuna siku nilipita mitaa ya kuitafuta Jangwani, nilikutana na kifusi robo tani cha mavi, sijui yalikuwa yana muda gani pale, ila mamlaka zingeweza kuchukua hatua haraka iwezekanavyo.
Mamlaka ziiangalie Kariakoo kwa jicho pevu la biashara ili kuweka mambo sawa
Barabara nyingi mbovu kupindukia, wakati wa mvua hapatamaniki zinajaa madimbwi, matope mpaka kero.
Miundombinu ya maji taka ndio hatari zaidi, ni kawaida majitaka yanayonuka kinyesi kutiririka mtaani huku wafanyabiashara wakiendelea na shughuli zao. Kuna siku nilipita mitaa ya kuitafuta Jangwani, nilikutana na kifusi robo tani cha mavi, sijui yalikuwa yana muda gani pale, ila mamlaka zingeweza kuchukua hatua haraka iwezekanavyo.
Mamlaka ziiangalie Kariakoo kwa jicho pevu la biashara ili kuweka mambo sawa