ZITTO alikuwa na karata kadhaa ambazo zingemuwezesha kusimama na kusumbua nchini lakini zote zimeenda off timing!
1- Karata ya udini yaani uislamu.hii karata imebuma kwa kuwa kuna UKAWA ambao umejumuisha waislamu na wakristu.
2-Karata ya ujiana nayo imebuma kwa kuwa ccm ina watia nia vijana na vikongwe.vijana kama kina makamba na mwigulu wameonesha uzaifu wa kutisha.
3-Karata ya usomi..hapa napo anagonga mwamba kwani chadema ina wasomi wa kufa mtu!
4-karata ya jinsia ...hapa zitto akaamua kumuweka mwanamke kama mwenyekiti wa ACT lakini bado watanzania hawajakubali kuongozwa na mwanamke hata Tibaijuka kachinjiwa baharini.
5-karata ya ufisadi...hapa zitto kakutana na lowassa ambaye anajitahidi kuiondoa turufu hii kama kigezo huku Dr slaa akisimama kama icon ya kuupinga ufisadi.
6-karata ya ukanda...hii nayo imegoma kwani lowassa ni kanda ya kaskazini na zitto hataki kuwaudhi wanaccm wa kanda ya kaskazini.
7-Zitto alitaka kuondoka chadema na kundi kubwa la wanachama na viongozi ...hili nalo likagoma.
8-Karata ya escrow...sifa zimeenda kwa tumbili halafu zitto alichemsha sana alipotaka kukubali mapendekezo ya adhabu yaliyotolewa na mtuhumiwa ...nyoka mwenye makengeza....Ati zitto alikiri uchovu!!!
9-Karata ya mabilioni ya uswiz alitumika kuuzima mjadala badala ya kututajia majina.