Kapuya ajisalimisha polisi

Kapuya ajisalimisha polisi

Suala la hapa si uzinzi bali ni UBAKAJI.
Wanataka kusema, "Asiye mzinzi kati yao, awe wa kwanza kumpiga Kapuya jiwe!" Karibu wote wanaohusika na kesi hiyo wana ukimwi. Mwisho wa siku Kapuya atakuwa hana kesi ya kujibu!
 
Kuna diwani hapo juu anaonekana hataki hili jambo lijadiliwe.Imagine mwakilishi huyu wa wananchi ngazi ya kata hajui madhara ya kitendo cha kapuya(herufi ndogo kuonyesha dharau) kijamii!

Anataka tujadili siasa za Zitto tu.Shame on you A.C.
 
Hivi kesi ya kubaka, kuambukiza UKIMWI kwa makusudi na kutishia kuua, dhamana yake inatolewaje kirahisi rahisi hivyo...


Ninachojiuliza ni hiki.., hivi kipindi kile babu seya kesi yake inaendeshwa aliwahi pewa dhamana kweli?
 
Hiyo single ya Kapuya imeshachuja! Chadema ni saccos inaendeshwa kilaghai!

Mkuu toka lini uliona single za kubaka zinachuja? Kapuya ni mbakaji, ni mhalifu lakini analindwa na serikali ya CCM na si vinginevyo na ingekuwa sheria inafuatwa inchi hii basi jamaa yenu angekuwa Segerea akisubiria haki yake itendeke
 
Ccm ni chama cha vibaka!

Mkuu ukisema "vibaka" ina-sound kama vimtu vidogo vidogo vile wakati ni mijitu mikubwa iliyonona tena mingine mi-professor na inabaka. Inafaa iwe "CCM ni chama cha mabakaji"
 
Hiyo single ya Kapuya imeshachuja! Chadema ni saccos inaendeshwa kilaghai![/QUO

Chadema imeteka maisha ya watu kama wewe !!! Kila kitu unafikiri ni siasa, ukilala ukiamka unawza chadema !!!! Hebu fikiria kama aliyefanyiwa hayo yaliyochuliwa ni mdogo wako au mwanao, bado ungeandika hivyo ? Na kama angekuwa ni mtu wa kawaida alitenda jambo hilo sasa hivi angekuwa mikononi mwa vyombo vya dola, hata dhamana asingepata, tangu lini kosa la ubakaji likadhaminiwa ? lakini kuwa makini na aina ya jamii manayojenga kwa kuoneana aibu na kulindana kwenu. Hivi Babu Seya yuko wapi vile, na je aliwahi kupewa dhamana wakati wa kesi yake ?
 
Mbona jana kama nimemuona bungeni pembeni ya serukamba? sasa alihojiwa saa ngapi na mara katimkia bungeni? Na je bunge limemruhusu mbakaji kuingia bungeni? Mimi naona kuruhusiwa kuingia bungeni ni kama kulidhalilisha bunge au tuseme na wabunge wote ndivyo walivyo?
 
Hiyo single ya Kapuya imeshachuja! Chadema ni saccos inaendeshwa kilaghai!

Jaribu kuwa na fikra na upeo mpana katika kufikiri na kuchangia hoja na sio kila uchafu, wizi na ufidhuli unaofanywa na watawala ndani ya ccm unaona kwako ni sawa na kutetea bila sababu ya msingi. Hata kama CHADEMA ni saccos inahusiana na mambo machafu ya uzinzi na ubakajia anayotuhumiwa kufanya Kapuya; Hii ni aibu na fedheha kwake mwenyewe na watawala wote.

Ni ajabu kuwa kwa Tanzania mambo kama haya yanalindwa na kutetewa na watawala kwa kushirikiana na vyombo vya dola ilhal kwa nchi nyingine angekuwa nyuma ya nondo za mahabusu akisubiri hukumu yake.
 
Hivi kesi ya kubaka, kuambukiza UKIMWI kwa makusudi na kutishia kuua, dhamana yake inatolewaje kirahisi rahisi hivyo...
Aisee tumewaza sawa kabisa na mimi nilitaka kuuliza swali hilo hilo hv kesi ya kubaka ina dhamana???? Naombwa kujuzwa na wenye uelewa wa sheria
 
Back
Top Bottom