Kanisa Moravian : mnatudhalilisha!

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,882
13,172
kwa muda mrefu sasa Kanisa La Moravian Tanzania (KMT), limekuwa katika mgogoro usioisha.
Kiini cha mgogoro huu ni ugomvi wa madaraka na mapato ndani ya kanisa hili kongwe.

Kanisa la Moravian asili yake ni Nyanda za Juu Kusini ambako lili chanua na kusambaa hadi Mikoa ya Tabora na hata sehemu za Katvi , Iringa na hata Mpanda.

Kinachotusikitisha waumini wa kanisa hili ni huu ugomvi ambao kiini chake ni fedha.
Tukumbuke kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea Pasaka,kipindi alichosulubiwa Mwokozi wetu Yesu Kristo,
ni fedha vile vile zilizo msaliti Bwana Yesu.

Hili somo nafikiri halijatua vema kwa wachungaji wetu ndani ya kanisa hili kongwe, fedha , asili ya tamaa ya kimwili ndio inalisambaratisha kanisa hili.

Pamoja na tamaa za fedha, kitu kinachojitokeza ni uvivu wa wote wanaohusika.

Mtu, uwe mchungaji au m-deacon, kama unslaumiwa kwa ajili ya tamaa zako ni heri tu kujiuzuru ili kanisa lisonge mbele kwa amani.
Lakini kwa sababu ya uvivu na tamaa sijasikia yeyote amejiuzuru,
Tukumbuke kuwa kujiuzuru ni kujitolea kwa kiwango cha chini kabisa ukilinganisha na Bwana wetu Yesu Kristo alivyotoa uhai wake kwa ajili ya dhambi zetu.

Kwa haya yanyoendelea katika Kanisa La Moravian Tanzania, waumini tusali sana ili virusi vya mwovu shetani viweze kudhibitiwa na Roho Mtakatifu.

cc Bujibuji , Baba V
 
Last edited by a moderator:
Watu Wanafanya Kazi Ya Mungu Kwa Mazoea, Ndio Maana Tumefka Hapa Tulipo. lakini pia kunahaja ya kumsihi mungu atusaidie kwa hili.
 
m nalikuwaga pale uhuru morovian enzi hizo kabla sijaenda pentekoste.na nina ndugu na jamaa hadi leo wapo morovian
kinachosababisha haya yote ni nyiny waumini wenyewe mkuwa kondoo sana kwa haya makundi mawili.kwanin msiungane na kuzpinga pande hizi mbili kwa umoja
 
Asante kwa maonyo. Ila kumbuka ulivyosema "Tukumbuke kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea majilio...", tunaelekea kipindi cha Pasaka. Majilio huwa ni maandalizi ya Kuzaliwa kwa Bwana Yesu.
 
Watu Wanafanya Kazi Ya Mungu Kwa Mazoea, Ndio Maana Tumefka Hapa Tulipo. lakini pia kunahaja ya kumsihi mungu atusaidie kwa hili.

Inabidi tumwobe sana Mungu atuepushe na hawa watumishi wa mishara ambao wameweka mbele maslahi binafsi badala ya kulitumikia Neno.
 
m nalikuwaga pale uhuru morovian enzi hizo kabla sijaenda pentekoste.na nina ndugu na jamaa hadi leo wapo morovian
kinachosababisha haya yote ni nyiny waumini wenyewe mkuwa kondoo sana kwa haya makundi mawili.kwanin msiungane na kuzpinga pande hizi mbili kwa umoja

Kanisa hili la Moravian linabibi lipitie kipindi cha Matengenezo kurudisha uchaji ndani ya waumini.

Sasa hivi watumishi wote wamechafuka mno kuhubiri Neno.
 
Nadhani Tanzania pia tumo ndani ya tatu (3) bora katika Afrika juu ya kujibunia njia za ulaji ati kupitia DINI ...!

Naishukuru Serikali kwa kutoa mfano juu ya kugundua mbinu ovu kama zile za lile ati KANISA lilokuwa likizuia watu kwenda maskuli pale KIGOMA.

Tuelekeako ni kutuambia kuwa MIMI NDO MUNGU, Mungu atueke mbali na LAANA kama hiyo.
 
kwa muda mrefu sasa Kanisa La Moravian Tanzania (KMT), limekuwa katika mgogoro usioisha.
Kiini cha mgogoro huu ni ugomvi wa madaraka na mapato ndani ya kanisa hili kongwe.

Kanisa la Moravian asili yake ni Nyanda za Juu Kusini ambako lili chanua na kusambaa hadi Mikoa ya Tabora na hata sehemu za Katvi , Iringa na hata Mpanda.

Kinachotusikitisha waumini wa kanisa hili ni huu ugomvi ambao kiini chake ni fedha.
Tukumbuke kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea Pasaka,kipindi alichosulubiwa Mwokozi wetu Yesu Kristo,
ni fedha vile vile zilizo msaliti Bwana Yesu.

Hili somo nafikiri halijatua vema kwa wachungaji wetu ndani ya kanisa hili kongwe, fedha , asili ya tamaa ya kimwili ndio inalisambaratisha kanisa hili.

Pamoja na tamaa za fedha, kitu kinachojitokeza ni uvivu wa wote wanaohusika.

Mtu, uwe mchungaji au m-deacon, kama unslaumiwa kwa ajili ya tamaa zako ni heri tu kujiuzuru ili kanisa lisonge mbele kwa amani.
Lakini kwa sababu ya uvivu na tamaa sijasikia yeyote amejiuzuru,
Tukumbuke kuwa kujiuzuru ni kujitolea kwa kiwango cha chini kabisa ukilinganisha na Bwana wetu Yesu Kristo alivyotoa uhai wake kwa ajili ya dhambi zetu.

Kwa haya yanyoendelea katika Kanisa La Moravian Tanzania, waumini tusali sana ili virusi vya mwovu shetani viweze kudhibitiwa na Roho Mtakatifu.

cc Bujibuji , Baba V

maspakyindi, hili kanisa sasa limekuwa kama nyumba ya shetani. Kila uchao ni ugomvi tu hamna kingine. Nakumbuka ugomvi mkubwa sana kati ya Mwamlima na Msinjili. Ugomvi huu ulidumu kwa miaka mingi hadi pale Augustino Lyatonga Mrema alipoingilia kati na kufanya maamuzi ya kibabe kumuondoa Mwamlima. Baada ya pale magomvi yakapungua ila sasa naona yamerudi mahala pake
 
Last edited by a moderator:
maspakyindi, hili kanisa sasa limekuwa kama nyumba ya shetani. Kila uchao ni ugomvi tu hamna kingine. Nakumbuka ugomvi mkubwa sana kati ya Mwamlima na Msinjili. Ugomvi huu ulidumu kwa miaka mingi hadi pale Augustino Lyatonga Mrema alipoingilia kati na kufanya maamuzi ya kibabe kumuondoa Mwamlima. Baada ya pale magomvi yakapungua ila sasa naona yamerudi mahala pake

Asante mkuu umetukumbushia yale ya nyuma.
Kwa kweli hawa wanaojiita viongozi wa kirohi sasa wanajionyesha kuwa hamna lolote bali wanaelekea kuwa wachumia tumbo kwa sadaka za waumini.

Wanatutia aibu kwa haya yanayoendelea.
 
Last edited by a moderator:
kwa muda mrefu sasa Kanisa La Moravian Tanzania (KMT), limekuwa katika mgogoro usioisha.
Kiini cha mgogoro huu ni ugomvi wa madaraka na mapato ndani ya kanisa hili kongwe.

Kanisa la Moravian asili yake ni Nyanda za Juu Kusini ambako lili chanua na kusambaa hadi Mikoa ya Tabora na hata sehemu za Katvi , Iringa na hata Mpanda.

Kinachotusikitisha waumini wa kanisa hili ni huu ugomvi ambao kiini chake ni fedha.
Tukumbuke kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea Pasaka,kipindi alichosulubiwa Mwokozi wetu Yesu Kristo,
ni fedha vile vile zilizo msaliti Bwana Yesu.

Hili somo nafikiri halijatua vema kwa wachungaji wetu ndani ya kanisa hili kongwe, fedha , asili ya tamaa ya kimwili ndio inalisambaratisha kanisa hili.

Pamoja na tamaa za fedha, kitu kinachojitokeza ni uvivu wa wote wanaohusika.

Mtu, uwe mchungaji au m-deacon, kama unslaumiwa kwa ajili ya tamaa zako ni heri tu kujiuzuru ili kanisa lisonge mbele kwa amani.
Lakini kwa sababu ya uvivu na tamaa sijasikia yeyote amejiuzuru,
Tukumbuke kuwa kujiuzuru ni kujitolea kwa kiwango cha chini kabisa ukilinganisha na Bwana wetu Yesu Kristo alivyotoa uhai wake kwa ajili ya dhambi zetu.

Kwa haya yanyoendelea katika Kanisa La Moravian Tanzania, waumini tusali sana ili virusi vya mwovu shetani viweze kudhibitiwa na Roho Mtakatifu.

cc Bujibuji , Baba V
Ni keli mkuu Kanisa hili limeingiliwa na wachungaji, maaskofu, watumishi wapenda pesa kama msngi wa wao kukaa madarakani.

Wengi wao hawana wito wa kumtumikia Mungu na ndio maana wamekamatwa kirahisi na yule mwovu.
 
Ni keli mkuu Kanisa hili limeingiliwa na wachungaji, maaskofu, watumishi wapenda pesa kama msngi wa wao kukaa madarakani.

Wengi wao hawana wito wa kumtumikia Mungu na ndio maana wamekamatwa kirahisi na yule mwovu.

Hamia katoliko ufaidike
 
Tatizo liko kwetu waumin na kanisa linako elekea ni mgawanyiko wa sehemu mbili.

Kyala tutuleghe
 
Tatizo liko kwetu waumin na kanisa linako elekea ni mgawanyiko wa sehemu mbili.

Kyala tutuleghe

Labda wajerumani wenye kanisa lao waje watufanyie mahamuz kama wenyewe kwa wenyewe tumeshindwa kuwekana sawa.maana morovian tz sasa kumekuwa ni uwanja wamieleka inabidi waje wamevaa helment kichwani
 
Tatizo ni wachungaji wasio na wito. Akili na Mioyo yao iko kqaajili ya maslahi binafsi. Ndo maana usishangae imani za kishirikina sinazungumzwa makanisani. Kanisa lilisha ooteza mwlekeo. Nashukuru ninekulia kwenye kitovu cha kanisa hili Rungwe. I know it well. Kanisa sio viongozi Dini imebaki kwa waumini. Ila makao makuu( viongozi) Mungu aingilie kati. Na kwa sasa hata Wajerumani wenyewe walisha kata mawasiliano. Inauma, Inasikitisha. Sijajua wanashindwa nini kuiga kwa Waroma au Waluteli. Mbona wenzetu wanafanya vizuri.
 
Back
Top Bottom