Kaniacha kisa kumwambia abadili dini

Habari naombeni ushauri!!nimekuwa kwenye mahusiano na binti almost miaka minne japo ni dini tofauti yeye muislamu,mimi mkristo!!Tumefanya vitu vingi sana pamoja na kushirikiana katika mengi tu tangu tukiwa chuo mpaka baada ya kumaliza!in short anajua kila kitu kuhusu mimi nami pia hakuna nisichojua kuhusu yeye!!

Ukweli tumependana sana,mwanzoni tuliona suala la dini halitakuwa tatizo sana binti alijitahid sana kujifunza mambo yanayohusu dini yangu mpaka kuingia kanisani mda mwengine lakini alikuja kubadilika ghafla baada ya kwao kujua na kumgombeza sana kwanin anafanya mambo yaliyo kinyume na dini yake hivyo sikuendelea tena kumuhimiza kujifunza dini yangu.Aliacha kwenda kanisan na kuacha kabisa kufwatilia dini yangu!
Tuliendelea kuwa kwenye mahusiano pasipo kuingiza tena suala la dini!

Lakini lilikuwa ni suala linalomuumiza kila mtu hasa future yetu na watoto wetu ni ipi!na je vp wazazi watakubaliana nasi! Kusema ukweli wazazi na ndugu zangu wasingekubali kabisa hili suala!!nilimficha binti mwanzon na kumtia moyo tu kuwa wazazi wataelewa na kunikubalia kumuoa hivyo hivyo nilifanya hivi ili nisimpoteze na kumkatisha tamaa.

Siku zikazidi kwenda binti akawa hana amani kwani alikuwa anaitaka sana ndoa akaamua kwenda kuwaambia wazazi wake kuhusu mimi na walikubali!ila ukija upande wangu ni suala gumu sana wazazi na ndugu kuelewa!

Ikabidi tu nimueleze wazi kuwa upande wangu hawakubali wanataka abadili dini kwanza japo nilijua ni jambo gumu kwake na hukukubaliana nalo.Mwisho nikamuambia basi itabidi tufunge ndoa ya bomani akakubaliana nayo!wakati namueleza yote hayo wazazi wangu sijawaambia lolote na wala hawajui kuhusu mahusiano yangu na binti.

Siku zikawazinazidi kwenda huku nasita kufanya lolote sababu najua wazazi na ndugu zangu watanipinga.Binti akawa hana amani kwani marafiki zake wanaolewa yeye na mimi tumekwama.Ilifika kipindi binti akawa ananinunia kabisaa wala hajisikii kuongea na mie wala hataki kukutana kimwili sababu ya mawazo ya ndoa.

Nilimuelewa hali alonayo na kumuonea sana huruma kwani watu kibao wa dini yake wanaenda kwao kutaka kumuoa lakini anawakataa sababu yangu hilo lilikuwa linaniumiza kwani mda unazidi kwenda na hamna nachofanya!!

Sikuwa na jinsi ikabid niongee na mama yangu nimueleze kila kitu kuhusu mimi na binti mama alikataa kabisa na kuniambia hilo haliwezekani na hata binti akibadili dini bado litakuwa suala gumu kwani mwisho wa siku atarudi tu dini yake ya mwanzo!!

Nikambembeleza sana mama na kumueleza tulipotoka mbali na binti na jinsi tunavyopendana lakini mama aliishia kuniambia tu tafuta wa dini yako!
Ikabidi tu nimueleze binti ukweli kuwa home wamekataa kabisaa hata ndoa ya bomani hivyo nikamshauri abadili dini ili hili suala liwe jepesi kwetu na hasa future ya watoto wetu waje wapate malezi mazuri!!Binti alikataa kabisa na kuanza kunilaumu nimempotezea mda wake bure na kwanin sikumueleza mapema!alinishukuru na kuniambia maisha mema asanteni sana!!

Yaani kiukweli binti ananichukia sana mimi mpaka ndugu zangu!!Moyo unaniuma kwani nampenda sana na wala sio nia yangu kumpotezea mda au kutokumuoa ila changamoto kubwa ni dini!kila mmoja wetu hataki kubadili kumfwata mwenzake!!

Nimekwama sielewi nifanye nini?wazazi na ndugu zangu wananipinga na hawakubaliani na hili!huku binti nae kanikasirikia hataki hata kunisikia na namba zangu kafuta na kuniblock!hahitaji kuongea lolote na mie kashafanya maamuzi ya kuniacha anasema haikuwa fungu lake mimi kumuoa!!

Naumia sana hasa mda wote tulokuwa pamoja na upendo wangu kwake!Anaona mie nimempotezea mda na simpendi kwani nimekuwa upande wa wazazi na ndugu zangu pia ni selfish nataka abadili yeye tu dini na sio mimi!!
Umegoma kuitwa Hemed naye kagoma kuitwa Sara.Hongera zenu.Msimamo ndiyo maisha yenu.
 
Na mimi nilipata kademu kazuri kakiarabu ila dini ndio ilizingua mimi najua kabisa home hawawezi kukubali kubadili dini na mimi siwezi kubadili dini wala dhehebu ilo nilishajiwekea kabisa kama nadhiri yangu ikabidi nimwache tu demu maana na yeye walikataa nisibadili dini mpaka leo sijabadili

Na demu nilishamwacha kabisa
Mwache tu Mkuu
Hakuna jinsi sasa kama wote mmeshindana ndio hivyo

Hakikisha ukitaka kudate na demu mwingine basi awe wadini yenu Mkuu
Hii itasaidia wewe kupata mke kabisa
Mafala nyie mbona kusaga kaoa mpemba, yaani unakosa nyapu tamu for life kisa dini? Unabadili tu unaoa unaendelea ya dini yako ya awali shwaaaaain!
Ndo maana maskini wa fikra na roho na pesa, dini wewe umekuwa papa au mufti? , waafrika matako kweli.
 
Moja ya vitu vigumu kwenye mahusiano ya kiafrika Ni pamoja na dini.
Mpaka tutakapojitambua kuwa dini Ni utamaduni tu na haina uhusiano na maisha baada ya kufa ndio tutakuwa sawa.
Tumeiga vitu vinavyotuletea shida Sana hata kwenye maisha ya kawaida tunashindwa kushirikiana.
 
Rais wa china amewah kuandika kuwa waafrika tumebeba din kuliko vitu vingine tumesahau kbs vitu vingine ila tulichobeba kwenye fikra zetu ni dini...!!! Hata waliozileta hizo din wao wenyewe hawazifuatishi kama ss tulivyozibeba kwa uzito.. Mi mwenyew ni muhanga wa hili suala lkn mkuu kati ya mambo magumu ambayo kupata ufumbuz wake inakuwa ni mgum sana hasa ukiwa unampenda itakutesa sana nmeandika kwa hisia kwa sabab najua ni jins gan ilivyo ngumu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom