Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,559
- 3,953
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mwibara kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kangi Lugola amepanda jukwaani kuzungumza na wananchi wa Mkoa wa Mara waliojitokeza kumpokea Mgombea Mwenza wa nafasi ya Makamu wa Rais Dkt. Emmanuel Nchimbi Agosti 30, 2025 mara baada ya kuwasili mkoani Mara.
Kangi amesema kuwa Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na mgombea mwenza wake watashinda mapema sana siku ya Uchaguzi Oktoba 29, 2025 kabla hata ya saa 5 asubuhi
Amesema "Kati ya wagombea 17 tunaoshindana nao, miongoni mwao kuna Wagombea 6 ni marafiki zangu. Walikuwa wananiambia wao hawatagombea, ila waliposikia Samia katoa magari kwa Wagombea wakaamua kuchukua fomu za kugombea. Nikawapigia simu, 'mbona sasa mmenidanganya?', wakasema 'hapana sisi uchaguzi wetu ni magari tumeshatiki ila Oktoba 29, ni Mama Samia na amepita"
Kangi amesema kuwa Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na mgombea mwenza wake watashinda mapema sana siku ya Uchaguzi Oktoba 29, 2025 kabla hata ya saa 5 asubuhi
Amesema "Kati ya wagombea 17 tunaoshindana nao, miongoni mwao kuna Wagombea 6 ni marafiki zangu. Walikuwa wananiambia wao hawatagombea, ila waliposikia Samia katoa magari kwa Wagombea wakaamua kuchukua fomu za kugombea. Nikawapigia simu, 'mbona sasa mmenidanganya?', wakasema 'hapana sisi uchaguzi wetu ni magari tumeshatiki ila Oktoba 29, ni Mama Samia na amepita"