Kampuni ya Tigo mnawaibia wateja!

kajembe

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
1,012
Reaction score
447
Wanajamvi mjihadhali na wizi wa kampuni ya Tigo,mimi nimekutana na mkasa wa kuibiwa na Tigo mara tatu,nimejaribu kuwapigia kwenye number yao ya customer care napata majibu ya computer kwamba nirecord malalamiko yangu halafu watanijibu baadae,sijawahi kukopa kutoka tigo lakini nikiweka pesa tu wanakata pesa kama sh mia mbili na kuniambia nimemaliza deni langu.Hiki kitu inaniudhi sana na sasa nimeamua kuachana Tigo kabisa! hata kama pesa kidogo lakini ni wizi na huenda wanaibiwa watu wengi na huo ni utapeli,kwanini mteja akiwa na malalamiko arekodi ili ajibiwe baadae?

Kampuni za simu zinabidi kuchunguzwa sana kwa style za namna hii za wizi na nina wasiwasi hata kwenye tigo pesa watakua wanaiba pesa nyingi sana bila watu kujua.:disapointed:
 
mimi nina wiki sasa sipati huduma yao ya kabang! najiunga hela zinakatwa lakini sipati dakika za maongezi!
 
Airtel Yatosha ndio habari ya mjini recharge tsh 10000 unakula 1gb na muda wa maongezi dakika 300 kwenda mitandao yote one month. uko kwa wasanii mnasubili nini?
 
Airtel Yatosha ndio habari ya mjini recharge tsh 10000 unakula 1gb na muda wa maongezi dakika 300 kwenda mitandao yote one month. uko kwa wasanii mnasubili nini?

Ni dakika 550 sio 300 hivyo ni rahisi zaidi kuliko kampuni wezi Voda na Tigo wanaobaka wateja mchana kweupe.....Jamani TTCL mko wapi pesa iwe inaenda serikalini maana haya makampuni binafsi yana tamaa ya fisi ama nyie vile vile mnatamaa ya kibinafsi maana hatuwaoni wakati mna mitambo yenye ubora kuliko hawa jamaa ambao vile vile wanatumia mitambo yenu, NEW CEO KIJANA UKO WAPI LETE MAPINDUZI YA AKINA MSECHU WA NHC.
 

Matola says thaks for this useful post.
 
Airtel Yatosha ndio habari ya mjini recharge tsh 10000 unakula 1gb na muda wa maongezi dakika 300 kwenda mitandao yote one month. uko kwa wasanii mnasubili nini?

Leo leo najiunga na AIRTEL,tigo wameniibia vyakutosha mwisho nitakuwa masikini bure.kwaheri tigo kaeni na wizi wenu.
 
tigo ni majizi walishawahi kunipiga 35,000 kwenye tigopesa na huduma yao ya extreme pack ni wizi mtupu,ukufika mda uliojiunga kesho yake hata kama una sms 300 wanakwambia huna salio,majizi tu haya kama ccm.
 
Kampumi ya simu ya tigo wamekua wasanii sana na ukweli wameanza utapeli wa waziwazi,ni karibu mwezi wa pili sasa naamaishwa na hela yangu 175,000/= ambayo niliingiza mwenyewe kwenye akaunti yangu ya tigopesa kwa nia ya kuiifadhi,lakini baada ya siku mbili hela ile ikawa haipo tena,nimewafuatilia nenda rudi nenda rudi,majibu yao wanayonipa ni upuuzi ule ule kila siku kua line yangu ina matatizo nikae baada ya masaa 48 watanitumia msg,mpaka leo hizo masaa 48 zimepita zaidi ya ishirini!na lingine ni kua,laini yangu sasa imekua na matatizo kiasi kwamba kuna baadhi ya namba nikipiga haziendi na hata nikipigiwa baadhi ya namba pia haziingii,week iliyopita kuna rafiki yangu nae kapata tatizo ilo ilo,hela yake 81,000/= haionekani,nae wamemuambia hayo masaa yao ya kitapeli 48 mpaka leo hajapata hela yake na line yake nae imeanza kumsumbua!kuna mtu wa tigo ametutonya kua utapeli huo unafanywa na tigo/wafanyakazi wenyewe kwa nia ya kumsumbua mteja mpaka akate tamaha na hela uhamishia kwenye akaunti zao za simu ambazo ni fake na wametengeneza kwa ajili hiyo tu!na hizo kesi kwa sasa zimekua nyingi mno bila kupatiwa ufumbuzi wowote,naombeni msaada wenu wadau je nifanyaje juu ya wizi huu wa wazi wazi wa tigo?
 
kweli usanii ni kila mahali wahusika hata hawana habari ya kufuatilia
 
Hawa jamaha wa tigo kwa kweli ni wezi wa kutupwa!nadhani so far kwa makampuni yote ya simu yaliyopo nchini Airtel wako better kwa kila kitu,huduma,gharama,network coverage e.t.c
 
Wana tabia moja mbaya sana siku hizi ukitaka kununua Kabaang wanakta hela na hizo dakika
hawakupi,ukiwapigia wanakwambia tutalipeleka section inayohusika,ujue ndiyo imetoka hapo'
 

Hii shida nami nakumbana nayo sana.Napia najaribu kupiga 100 aipokelewi.Ni kweli kabisa ukiongeza salio kwenye line ya Tigo na usipo itumia unakutwa umekatwa sasa wakati mwingine natamani nimpate customers care wao apatikani,mara nyingine najiuliza au wa tozo ya service charge ambayo atujajulishwa,mbona Voda na Airtel ukiweka salio usipotumia awakati hata senti moja.Kwanini iwe ni Tigo tu.Kama wafanyakazi wao wapo huku lifanyie hilo swala kazi.Na msije na majibu ya kwamba umejiunga au ulijiunga kwenye huduma ambayo unakatwa mi kwenye line yangu ya Tigo sijawai jiunga na huduma yoyote zaidi ya BB Service na huduma ya kawaida ya kununua bundle hiyo hela nyingine nayo kwatwa inatokana na nini.Katika ulimwengu wa biashara ukimpoteza mteja mmoja,kumrudisha ni kazi.
 
habari kajembe, tatizo limeanza lini na unalipata ukiwa maeneo gani? pia tupe namba yako kwa msaada zaidi..
 
hakuna kampuni ya simu ambayo haijaniibia,hivyo watu wakilalamika mtandao huu na kudhani ule una nafuu huwa nawaangalia tu,wote wezi wanachopokezana ni wakati wa kuiba leo huyu kesho yule!
 
hakuna kampuni ya simu ambayo haijaniibia,hivyo watu wakilalamika mtandao huu na kudhani ule una nafuu huwa nawaangalia tu,wote wezi wanachopokezana ni wakati wa kuiba leo huyu kesho yule!

haswaaaaa ila tigo ni washindi kuliko wote, last week niliweka buku 2 eti badala ya msg kunipa balance ya 2,000 inanijulisha kuwa balance yangu ni sh 446 tu kwamba wamekata deni lao, sijawahi kopa hata siku moja na hata kama ni charge ya mlio ndio iwe 1,600! sasa hivi naweka 500 tu kwa wiki nzima, niko kwenye mitandao yenye adabu kidogo angalao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…