Kampuni ya tanzanite one yafilisika kwa madeni, watanzania wa arusha wainunua

MR WRONG

New Member
Sep 9, 2010
3
0
Tanzanite One yafilisika, Watanzania wainunua
Mwandishi Wetu, Manyara

KAMPUNI ya Tanzanite One iliyokuwa ikichimba madini ya vito aina ya Tanzanite,katika mji mdogo wa Mererani, Simanjiro Mkoani Manyara imefilisika na kulazimika kuuza hisa zake zote kwa kampuni ya Sky Associates Group inayomilikiwa na watanzania.

Kampuni hiyo iliyokuwa miongoni mwa kampuni tanzu zinazomilikiwa na kampuni ya Richland Resource ya nchini Uingereza chini ya utendaji wa Bernard Oliver imeamua kuuza hisa zake ambazo ni asilimia 50 kwa kampuni hiyo ya Kitanzania kutokana na kampuni ya Tanzanite One kudaiwa kukumbwa na madeni yanayofikia bilioni 23 na kushindwa kujiendesha.

Wakurugenzi wakuu wenye hisa nyingi katika kampuni ya Sky Associates Group ni Hussein Gonga na Faisal Shahbhati ambao kwa pamoja wamethibitisha kununua hisa zote za Tanzanite One baada ya kampuni hiyo kujitangaza katika mitandao yake ya kibiashara kuwa imeshindwa kujiendesha. Hisa zingine zimenunuliwa na raia wa India Rizwan Ullah.

Mbali ya madeni hayo kampuni hiyo inadai kushindwa kujiendesha kutokana na migogoro kati ya kampuni hiyo na wachimbaji wadogo ambao wamekuwa wakivamia migodi hiyo mara kwa mara na kukosa ulinzi madhubuti.

Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na gazeti hili ikiwemo kushuhudia baadhi ya nyaraka za Sky Associates Group, imethibitika kampuni hiyo ya wazawa imenunua hisa za tanzanite One na mali za kampuni hiyo kwa thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 32 fedha za kitanzania.

Hata hivyo kwa mujibu wa nyaraka hizo na kuthibitishwa na wakurugenzi hao, Sky Associates Group imechalipa bilioni 27 ikiwa ni pamoja na madeni na kumiliki mali za kampuni ya Tanzanite One na kubakiwa na deni la dola za Marekani Milioni 5.1 sawa na fedha za kitanzania shilingi bilioni 8.9

Habari kutoka ndani ya kampuni ya Tanzanite One zinasema kuwa madeni makubwa yanayoikabili kampuni hiyo ni pamoja na taasisi za Serikali na wabia wengine wa kampuni hiyo jambo lililofanya kukua na kufikia kiwango hicho cha shilingi bilioni 23.

Pia uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa kampuni ya Sky Associates Group mbali ya kumilikiwa na wazawa kwa asilimia mia moja lakini imesajiliwa nchini Hong kong na wakurugenzi wa kampuni hiyo wamekuwa wakifanya biashara ya madini katika nchi mbalimbali duniani.

Mmoja wa wakurugenzi wa Sky Associates, Hussein Gonga alipotakiwa kuzungumzia ununuzi wa kampuni hiyo, alikiri yeye na mwenzake Faisal kununua hisa za Tanzanite One na hivyo kufanya wao kuwa wamiliki wabia na Serikali.

‘’Ni kweli sisi wazawa kupitia kampuni ya Skye Associates Group tumeinunua Tanzanite One kwa kununua hisa zake baada ya kukabiliwa na mzigo mkubwa wa madeni na kushindwa kujiendesha kibiashara, hata hivyo taratibu zingine za ununuzi zikikamilika tutatoa taarifa rasmi, ’’alisema Gonga

Kampuni ya Sky Associates Group mbali ya kufanya biashara ya madini pia imekuwa ikifanya utafiti, kutangaza madini yasiyotambulika na yamekuwa na soko zuri katika nchi mbalimbali za mabara ya Ulaya na Asia ambayo yanachimbwa sambamba na Tanzanite .

Miongoni mwa madini hayo ambayo yamekuwa yakitangazwa na kampuni hiyo ni pamoja na Pink tanzanite, Yellow tanzanite, Axinite, Grossular Garnet, Kyenite na Diopsite.

mwisho
 
Husein gonga ameinunua karibu Arusha nzima. Ana magorofa kila mtaa..!
 
hapo li mzee muhongo lingepata chance lingeenda UK kutafuta mwekezaji "mwenye mtaji" na kuwapuuzilia mbali akina hussein gonga na mwenzie,kama aliweza kusema mtaji wa R Mengi unatosha kwa biashara ya juice tu, angeweza kupoteza muda wake kumsikiliza Gonga???
 
Kweli sijawahi kuona Profess muhongo kama huyu, sasa Kina Gonga wamepata wapi mtaji?
 
Husein gonga ameinunua karibu Arusha nzima. Ana magorofa kila mtaa..!
acha upimbi we kada!! eti amenunua karibu arusha nzima!!! kwako we ngarenaro ndiyo arusha? au kununua kale ka banda kenu pale soko mjinga ngarenaro ndiyo ukaona sasa anaweza kununua arusha? nguma kqbisq wee
 
Kweli sijawahi kuona Profess muhongo kama huyu, sasa Kina Gonga wamepata wapi mtaji?

ndiyo mawaziri wa JK mkuu wangu! usiumize kichwa,hata huyo mtembea uchi hapo juu a.k.a laki si pesa anaweza pewa tu uwaziri siku akijipitisha mbele ya mkulu akitingisha.
 
acha upimbi we kada!! eti amenunua karibu arusha nzima!!! kwako we ngarenaro ndiyo arusha? au kununua kale ka banda kenu pale soko mjinga ngarenaro ndiyo ukaona sasa anaweza kununua arusha? nguma kqbisq wee

Kaa kimya we kenge, hujui chochote
 
wakuu hii habari ni uongo mtupu, ukweli ni kuwa hiyo kampuni ya husaein iliomba kuuziwa hisa kidogo na imepewa 10% ya hisa zinazomilikiwa na rich land na sio zote kama mleta taarifa anavyopotosha.
 
TANZANIA
EXPLORATION & PRODUCTION
n°335 - 23/12/2014
Richland brings Sky Associates into tanzanite deal
After several weeks of bargaining, Richland Resources Ltd has reached an agreement to sell its firm TanzaniteOne Ltd to Sky Associates Group Ltd. London-registered Richland had been the lone industrial-scale producer of the precious blue tanzanite gem up to now.

Sky, which laid out $5 million for the stake, is controlled by two businessmen based in Arusha, Faisal Shahbhat and Hussein Gonga. Gonga already owns three other mining companies, namely Capricorn Minerals, Prime Gemstones (T) Ltd and Hugo Gems.

Shahbhat is the founder of Maruti Green Gems and Tanzanite Forever Ltd.

Under the contract, which doesn’t involve marketing the gems - this is done by a firm named Tanzanite Experience that remains controlled by Richland - Sky will take on over $10 million in TanzaniteOne’s debt.

When the transaction is completed, Sky will become a partner of the state-owned mining concern STAMICO in working the tanzanite mine at Mererani. Indeed, Richland formed an equal-share joint venture with STAMICO in December, 2013 for a licence numbered 490/2013.

The sale of the stake underscored the relative failure of the government’s indigenisation policy in the mining industry. In 2012, hundreds of small-scale miners began occupying the underground, block C section of the Mererani mine and have never been totally expelled by the local police, obliging TanzaniteOne to sharply cut back its mining operations.

The small-scale miners have licenses but most of the 600 working on Mererani don’t report how much they produce and thus fail to pay taxes or royalties to the government. In addition, most of the tanzanites are smuggled out to Jaipur in India, where they are cut. Jaipur, India’s gem capital, earned $82 million in exports of tanzanites in 2012 whereas Tanzania itself makes only $20 million per annum from its tanzanite exports.


© Indigo Publications.
 
Back
Top Bottom