Kampuni ya Mbunge Kigwangalla yahusishwa na utapeli katika soko la dunia

Ili kuweka rekodi sawa niseme tu hapa kwamba Mimi kwa sasa (tokea May 2010 nilipoenda kugombea Ubunge Nzega) sijihusishi na uendeshaji wa kila siku wa Kampuni ya MSK Solutions Ltd na hivyo sijui baadhi ya mambo yanavyoendelea.

Nimesoma upya hiyo article ya The Guardian na nimeuliza kwenye Menejimenti ya Kampuni ya MSK Solutions Ltd (ambayo mimi nina hisa) wamenihakikishia kampuni yetu haiko kwenye Orodha ya Makampuni ya Tanzania yaliyo kwenye 'Blacklist'; ila kilichopo karibu na makala hii ya The Guardian ni kama ifuatavyo: MS inadaiwa marobota ya pamba ambayo ilifanya 'short supply' na kwa kufanya hivyo walijikuta wamekiuka makubaliano ya kimkataba, na Mteja anapenda asaini Mkataba mwingine na MSK mwaka huu ili kiasi ambacho hakikuweza kuwa supplied mwaka Juzi akipate mwaka huu, na hilo halina tatizo, ni kitu cha kawaida na kina utaratibu wa kufuata kabla ya kufikia makubaliano. Mazungumzo yanaendelea. Hata hivyo mteja hakuwa amelipa fedha zozote na huwezi kusema alidhulumiwa ama vipi.

Labda nielezee kwa ufupi tu hapa mchakato unavyokuwaga. Ni kwamba kama kulikuwa na marobota 2000 kwenye mkataba na wewe uka-supply 1700 (kama ilivyokuwa kwa MSK Solutions), utalipwa pesa ya hayo 1700 uliyo-supply tu (kwa mtindo wa Letter of Credit ama hata ule wa Cash against Documents, yaani CAD). Hata hivyo mnunuzi atakudai lazima umalizie hayo 300 yaliyobaki kwa kuwa utakuta na yeye (kama akiwa ni international merchant) alipofunga mkataba na wewe alienda akafunga mkataba na mwingine (mill users) ambao nao wanajipanga kuuza bidhaa yao kwa kuwa wana uhakika wa marobota 3000 kutoka kwake. sasa uki-supply nusu unakuta umesababisha hii chain yote ipate matatizo, na kwa kuwa mikataba ya kimataifa inalindwa na mikataba na kanuni mbalimbali za biashara ya kimataifa kama vile ICA, ICC, Inco-terms unakuta unatakiwa ulipe fidia kwa mteja wako. Sasa huwa kuna arbitral bodies ku-determine haki ya pande mbili na hii hutoa award, ambayo kisheria huja kusajiliwa hapa high court nchini. Pande mbili zina nafasi ya kujadili nini kifanyike (nje ama ndani ya utaratibu wa mahakama) na hivi sasa ndicho kinachofanyika! Hii hutokea mara nyingi tu.

Blacklist ni orodha ya makampuni ambayo hayaruhusiwi kuuza pamba yao nje, na kampuni (muuza pamba kama MSK SOlutions) huingia humo baada ya award na baada ya determination ya high court ya nchi husika, imeendelea kugoma kulipa fidia hiyo ama kufanya makubaliano na kampuni ile nyingine (mteja).

ANGALIZO: Kuna watu wamekuwa kazini usiku na mchana kunitafutia kashfa ili kunimaliza kisiasa na kibiashara. Naomba niwatake waache mara moja ama watayasababishia gharama kubwa magazeti haya kwa vile yatashitakiwa na kudaiwa fidia ama na kampuni ya MSK Solutions Ltd ama na Wanasheria wangu, kwa niaba yangu. Tayari mchakato unaendelea kulishtaki gazeti la Sauti Huru na nimeamua kushauriana na Mwanasheria wangu kuhusu nini kifanyike kuhusiana na hili. Ndg zangu wanabodi, na wanahabari, kuweni makini na 'fair' kwa watu, makampuni na personality zao ili kulinda uhuru na haki ya kila mtu. Tusipende sana kutendewa haki wakati sisi hatautoi haki kwa wengine na wala hatutekelezi wajibu wetu. Mchakato wa kawaida wa utoaji haki ni lazima uendane na utekelezaji wa wajibu na majukumu yetu ipasavyo bila kuathiri wengine.

I am slowly getting fade up na siasa za nchi yetu kwa sababu ya mambo kama haya.

Ahsanteni,
HK.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Jamani Kampuni ya MSK Solutions haijafanya utapeli wowote ule, popote pale. Acheni kuchafuana jamani. Nani amemtuma huyu mtu? Hebu angalia kichwa cha habari cha the Guardian na hicho cha Kwake...yaani ni mbingu na ardhi!

Kisha nani kakwambi ana uchu na uwaziri? Kama Rais anapotoa Uwaziri huwa anawauliza wahusika, fahamu kabisa akifanya hivyo mimi nitakataa! Kelele nyingi utafikiri ukipewa nafasi ya uongozi ni sawa na kupewa pepo ya Mwenyezi Mungu...

Mnawasema viongozi, kwa wivu mpaka wengine sasa hatuna hamu hata ya kuwafanyia hiyo kazi yenu ya kutoa huduma kwa nchi. Bora tubaki mtaani tu tufanye ya kwetu. Na ninawaambia kama tusipojirekebisha tutakosa watu wazuri wa kuendesha nchi, maana kila mtu ni fisadi, mwizi, sasa nani msafi? Mnasema Zitto ana majumba na magari ya kifahari! Mbowe yale yale. Slaa naye ana kashfa ya Josephine na matumizi mabaya ya madaraka...JK yale yake, sasa ni nani msafi kwenu watanzania?


Kigwangala,

Bila shaka utakumbuka kwamba mimi ni mmoja kati ya watu ambao nimekuwa nikukumbusha mara kwa mara kwamba umewaibia watanzania kwa kampuni yako kujipatia fedha za stimulus package lakini mkawadhulumu wakulima wa pamba. Ninapokueleza haya ninafanya hivyo kwa kuamini kwamba unatakiwa kujirekebisha ili uendelee kuwa tumaini kwa watanzania wanaoamini kwamba unaweza kuwa kiongozi mzuri, japo kwa sasa uko kwenye boti isiyo na matumaini sana ya kukuvusha upande wa pili wa bahari, hata hivyo kwa kuwa kuna boti nyengine zinapita karibu na yako, zitakuwa tayari kukuokoa na hivyo kukufikisha katika nchi kavu na ukawatumikie watanzania.

Viongozi lazima msemwe tena kwa sauti ya juu kwa wale wote wanaoonekana kuwasaliti wananchi. Na kwa kiongozi anayejitambua na kutambua wajibu wake ni lazima ahakikishe anawatumkia wananchi, na anatambua kwamba akiboronga tu watamwambia. Na sisi tunaofanya kazi ya kukwambia kila siku mahali ulipokosea ndio tunaokutakia mema, ingawa najua unatuchukia kwa kuwa hatujawahi kuchoka kukwambia ukweli.

Baada ya kusema hayo, rai yangu kwako ni moja tu.Lazima uchukue hatua za makusudi kuwaonyesha watanzania kwamba kama kweli hukuwadhulumu, na kama uliwadhulumu kwa mujibu wa taarifa tulizonazo, ni muhimu ukarudisha fedha zetu na kuomba masamaha kwa yote yaliyotokea, kisha tusonge mbele. Kinyume na hivyo, hili zimwi la MSK Solutions kutuhumiwa kunufaika na stimulus package, na sasa unaona waandishi wa habari wamekwenda hatua moja mbele na kukuonyesha kwamba hata katika soko la dunia nako kampuni yako inatuhumiwa, ni dalili mbaya sana kwa mustakabali wako wa kisiasa na kibiashara.

Mwisho katika hili, nikukumbushe kwamba usijaribu kumhadaa mtu hapa, kati ya watu wanaotamani na kusubiri kuteuliwa kuwa mawaziri wewe ni mmoja wao. Huwezi kumdanganya mtu hapa eti ukiulizwa utakataa. mbona ulipobebwa katika ubunge hukukataa? Je unadhani umefanya nini hadi kustahili kuwa waziri? mdio maana wananchi wanaokufahamu wanajua kwamba ukiteuliwa kuwa waziri itakuwa ni kazi bure, hakuna chochote cha manufaa kwa nchi hii utakachoweza kufanya.
 
Mkuu Kigwangala,
Hoja unayopaswa kujibu au kutolea ufafanuzi ni kwa nini kampuni yako/yenu imekuwa 'blacklisted' na kuwekewa vikwazo vya kutokuuza pamba popote duniani. Hiyo ndo hoja unayopaswa kuitolea maelezo.
 
Kama kila hoja ingekuwa inapatiwa majibu faster kama hii JF would have been the best forum ever in Tz.
Tatizo kuna watu zikiletwa hoja zao umu hawajibu sijui ni kuwa hawana access au ni kudharau.
Hawajui kuwa hoja isipojibiwa kwa ufasha umu hubebwa kama ilivyo kwa wananchi!
Thank u for the updates Dr HK
 
Ili kuweka rekodi sawa niseme tu hapa kwamba Mimi kwa sasa (tokea May 2010 nilipoenda kugombea Ubunge Nzega) sijihusishi na uendeshaji wa kila siku wa Kampuni ya MSK Solutions Ltd na hivyo sijui baadhi ya mambo yanavyoendelea.

Hapa unasema umejiweka pembeni toka katika shughuli za MSK Solutions. Ni jambo zuri sana kama ndivyo ulivyofanya(kama si hadaa), bila shaka ukilenga kujiepusha na kamgogoro ka kimaslahi.

ANGALIZO: Kuna watu wamekuwa kazini usiku na mchana kunitafutia kashfa ili kunimaliza kisiasa na kibiashara. Naomba niwatake waache mara moja ama watayasababishia gharama kubwa magazeti haya kwa vile yatashitakiwa na kudaiwa fidia ama na kampuni ya MSK Solutions Ltd ama na Wanasheria wangu, kwa niaba yangu. Tayari mchakato unaendelea kulishtaki gazeti la Sauti Huru na nimeamua kushauriana na Mwanasheria wangu kuhusu nini kifanyike kuhusiana na hili.

Sasa hapa ndipo umejichanganya tena, unakwenda kuwashitaki the guardian kwa niaba ya MSK Solution ambayo hushughuliki nayo kwa sasa kama ulivyodai hapo juu ama unakwenda kuwashitaki kwa kukukashifu wewe binafsi, na ni wapi the guardian wamekukashifu??

Huu nauona kama ni mkwara mbuzi tu wala hakuna atakayetishika, tena huko mahakamani ndipo watakufunua vizuri. We jaribu kuonja sumu kwa kuilamba, kitakachokupata itakuwa siri yako.
 
Jamani Kampuni ya MSK Solutions haijafanya utapeli wowote ule, popote pale. Acheni kuchafuana jamani. Nani amemtuma huyu mtu? Hebu angalia kichwa cha habari cha the Guardian na hicho cha Kwake...yaani ni mbingu na ardhi!

Kisha nani kakwambi ana uchu na uwaziri? Kama Rais anapotoa Uwaziri huwa anawauliza wahusika, fahamu kabisa akifanya hivyo mimi nitakataa! Kelele nyingi utafikiri ukipewa nafasi ya uongozi ni sawa na kupewa pepo ya Mwenyezi Mungu...

Mnawasema viongozi, kwa wivu mpaka wengine sasa hatuna hamu hata ya kuwafanyia hiyo kazi yenu ya kutoa huduma kwa nchi. Bora tubaki mtaani tu tufanye ya kwetu. Na ninawaambia kama tusipojirekebisha tutakosa watu wazuri wa kuendesha nchi, maana kila mtu ni fisadi, mwizi, sasa nani msafi? Mnasema Zitto ana majumba na magari ya kifahari! Mbowe yale yale. Slaa naye ana kashfa ya Josephine na matumizi mabaya ya madaraka...JK yale yake, sasa ni nani msafi kwenu watanzania?

Acha kujitia ujuaji wewe!

Unawafahamu viongozi wewe??

Nawe unajiita kiongozi kwa kipi hasa unachoamini?? You are not self-centered in thinking!!

Bendera fata upepo!!

This is not the board for glorifying thieves, mipango mnayopanga na vikampuni vyenu hewa hivyo wakulima wa pamba wameshastuka, kwanza ninyi wote mliokula stimulus package ni makada wa magamba. Usidhani kukaa Bungeni ndio inakufanya ujione nawe ni kiongozi. Tunawaona viongozi ambao wanafanya legislature duties at their best na haumo kati ya hao.

Nilikwambia kule na hapa narudia, hufai period!
 
Jamani Kampuni ya MSK Solutions haijafanya utapeli wowote ule, popote pale. Acheni kuchafuana jamani. Nani amemtuma huyu mtu? Hebu angalia kichwa cha habari cha the Guardian na hicho cha Kwake...yaani ni mbingu na ardhi!

Kisha nani kakwambi ana uchu na uwaziri? Kama Rais anapotoa Uwaziri huwa anawauliza wahusika, fahamu kabisa akifanya hivyo mimi nitakataa! Kelele nyingi utafikiri ukipewa nafasi ya uongozi ni sawa na kupewa pepo ya Mwenyezi Mungu...

Mnawasema viongozi, kwa wivu mpaka wengine sasa hatuna hamu hata ya kuwafanyia hiyo kazi yenu ya kutoa huduma kwa nchi. Bora tubaki mtaani tu tufanye ya kwetu. Na ninawaambia kama tusipojirekebisha tutakosa watu wazuri wa kuendesha nchi, maana kila mtu ni fisadi, mwizi, sasa nani msafi? Mnasema Zitto ana majumba na magari ya kifahari! Mbowe yale yale. Slaa naye ana kashfa ya Josephine na matumizi mabaya ya madaraka...JK yale yake, sasa ni nani msafi kwenu watanzania?

Chonde ndugu yangu Hamis(MB)

Usimsafishe huyo mtu niliyemuwekea red, utajishushia hadhi.

Hilo linatuuma sana sisi wananchi wapenda haki
 
HK your a*s is on fire,msk ilipata stimulus package,jk anawatumiaga watu kama hawa kupiga hela..credit crunch haikuigusa bongo kabisa,hiyo package ilikuwa moja ya ufisadi wa jk na genge lake la majambazi wa rasilimali zetu.
 
HKigwangalla,

Nimesoma upya hiyo article ya The Guardian na nimeuliza kwenye Menejimenti ya Kampuni ya MSK Solutions Ltd (ambayo mimi nina hisa) ...
Hayo ndiyo mambo uliyotakiwa kufanya kabla ya kujibu hoja kwamba (a) unasoma article vizuri na kuielewa na (b) kupata facts zote toka kwa wenzako wa MSK.

I am slowly getting fade up na siasa za nchi yetu kwa sababu ya mambo kama haya.
If you cant stand the heat get out of the kitchen.
 
Mh Dr HK,
Ahsante kwa kuja jamvini na hoja zako ingawa napata wasiwasi na vitisho na maneno kuwa mtoa mada anatumiwa. Mimi ni mtanzania wa kawaida tena wa kijijini lakini ni huru na Mzalendo halisi wa nchi hii. Akina Maxence Melo wakati wanalianzisha jukwaa hili waliamini litakuwa huru na chachu ya kuleta maendeleo ya taifa letu, hasa katika kupata viongozi bora. Kiongozi bora kaka yangu HK ni yule aliye PASS THE PUBLIC SCRUTINY test na akaonekana hana shaka yoyote katika uadilifu. Kama JF ingekuwepo kabla ya 2005 viongozi wengi wabovu tulionao leo katika hii serikali yetu wala wasingekuwepo madarakani kwani usafi na uchafu wao ungejadiliwa na jamii na wale wenye uchafu usiotia shaka wangepatikana kutuongoza. Kitendo cha wewe kujibu hii hoja kimekusafisha kwa watanzania wengi na watu wamepata fursa kujua kuwa nawe ulikuwa mmoja wa wafanyabiashara wa pamba. Kama ni msafi au sio mimi siwezi kujua lakini ufafanuzi wako kwa hii hoja umekuimarisha sana kisiasa kama hujui. Huenda hata King Maker alivyoona hii makala alielewa kama mimi na sasa ameclear mashaka kuhusu usanii wa hii kampuni na uhusika wako. Tukitumia vizuri jukwaa hili bila kuwa subjective tunayo nafasi nzuri sana kupata viongozi bora hapa nchini kwetu. Najua umechukizwa na hii habari kwa kuwa utaratibu wa kupata viongozi wasio na mashaka kwa jamii ni mgeni lakini kuna siku tukifika kwenye Tanzania tunayoipenda mimi na wewe, tofauti na hii unayoipenda wewe kwa kuwa unamudu kununua debe la mahindi wakati mimi nisiye na 12,000 ya kununulia debe la mahindi naichukia Tanzania. Again thanks mheshimiwa kwa kunijibu mimi mtanzania wa kawaida, tena wa kijijina na pia thanks JF kwa kutupa fursa wanyonge kuclear doubts zetu juu ya nyie viongozi wetu. Kichwa cha habari hakijasema wewe ni tapeli but kampuni yako imehusishwa na utapeli. Hakuna Blacklist bila utapeli popote duniani na mikataba huwa ina clause za kuzungumzia kama kiwango cha bidhaa mlizouziana hakikutimia, please refer to The Sale of Goods Act brother.
 
kingwangala huwa kila mara nakuwa na mashaka sana na elimu yako au upeo wako wa akili maana maada unayojibu siyo iliyoandikwa hapa na unaleta mikanganyiko mimgi sana kwenye hili mara wewe huhusiki mara unamuda mrefu hujihusishii na company hii tuchukue lipi?
 
Mimi bado na wasiwasi na majibu ya HK ,naona bado yanatongotongo hivi.Nanukuu"Mimi sihusiku na uendeshaji wa kila siku wa MSK tangu niwe mbunge lakini bado ninahisa zangu".Hayo ni majibu mepesi kweli hasa katika issue ya corprate management.Mwanahisa yeyote lazima apate management reports,inamaanisha yeye bado ni director hivyo management bado inawajibika kwake kupitia taarifa mbalibali au kuhudhuria vikao vya bodi ya wakurugenzi.Katika mazingira yoyote yale anajua in and out of the corporate liability of MSK.Jenga hoja yako bwana naona bado kiza kwenye MSK .Taarifa ya the Guardian ipo nzuri na imejitosheleza vizuri.
 
Back
Top Bottom