Kampuni ya KANTAKA MOTORS yapewa msamaha wa kodi wa miaka 10

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,066
40,725
Katika juhudi ya kukuza viwanda vya ndani vya magari, serikali ya nchini Ghana imeipa likizo ya kodi ya miaka 10 kampuni ya kutengeneza magari ya mtume Osafo Kantanka ijulikanayo kama KANTANKA MOTORS.

Hatua hii inalengo la kuiwezesha Ghana iweze kushindana na kampuni za magari toka Ulaya, Asia na Marekani, pia inafikiria kupiga tozo kubwa zaidi kwa magari toka nje ili kuvutia wanunuzi wa ndani.

Pia serikali imeweka mkakati wa kuacha kuagiza magari toka nje ya nchi na badala yake wameanza kunua magari yanayozalishwa ndani kwani imebainika ni imara, yana muonekano nadhifu na yanadumu kuliko yale ya Japana na Marekani, poa hatua hii inalengo la kupunguza tatizo la ajira nchini Ghana.

Mambo kama haya ni ya kuigwa na kupigiwa mfano, najiuliza tu, kama kweli serikali yetu inania ya kukuza viwanda vya ndani, inawezaje kuagiza mabuti na sare za jeshi toka China huku maelfu ya vijana waliosomea ushonaji wakiwa hawana ajira, hivi kweli huwa tunatumia kiungo gani cha mwili kufikiri? Msaada tafadhali; video inamaelezo ya ziada.


_________________________________
 
wamefanya jambo zuri katika kuvutia uwekezaji ila wanatakiwa wawe waangalifu katika usimamiaji wa miradi mikubwa kama hiyo ili kuzuia transfer ya mali ukizingatia kuna kipindi cha miaka 10 ya mpito kabla ya kuanza kulipa kodi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wamefanya jambo zuri katika kuvutia uwekezaji ila wanatakiwa wawe waangalifu katika usimamiaji wa miradi mikubwa kama hiyo ili kuzuia transfer ya mali ukizingatia kuna kipindi cha miaka 10 ya mpito kabla ya kuanza kulipa kodi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwenye hiyo kamapuni mtume Osafo Kantanka ni mzawa na ameanza kutengeneza magari hayo kwa njia za kienyeji kabisa hadi sasa wanauwezo wa kutengeneza magari yenye ubora, kila kitu ni locally made, kuanzia engine, chassis hadi body.
Tena bado hawajawa na mitambo mikubwa, hata engine ni wanazitengeneza kwa shida sana, ona mwenyewe, wanahitaji sana hii support.
 
Hivi bei zake zitakuwaje?
Waafrika hatuna upendo wenyewe kwa wenyewe
Hapo tungemuunga hata kutoa orders za gari
Lakini roho za korosho zinaturudisha nyuma

Sent from my SM using Tapatalk
 
Hivi bei zake zitakuwaje?
Waafrika hatuna upendo wenyewe kwa wenyewe
Hapo tungemuunga hata kutoa orders za gari
Lakini roho za korosho zinaturudisha nyuma

Sent from my SM using Tapatalk
Nasikia ni bei nafuu sana, ni sawa tu nakuagiza gari used toka Japan + kodi; maana wao wamepewa tax holiday, kwahiyo hulipi kodi yoyote ile! Angalia tu hapa bongo, kampuni za ushonaji zimejaa tele, wadada washonaji wapo kibao lakini tunaagiza sare za jeshi toka nje, roho za korosho zinatudidimiza sana!
 
Eng.Kantanka kipindi anaanza

Hata ulaya walianza hivi hivi, itafika siku tutabaki Tanzania tu ndio hatujielewi
 
Nasikia ni bei nafuu sana, ni sawa tu nakuagiza gari used toka Japan + kodi; maana wao wamepewa tax holiday, kwahiyo hulipi kodi yoyote ile! Angalia tu hapa bongo, kampuni za ushonaji zimejaa tele, wadada washonaji wapo kibao lakini tunaagiza sare za jeshi toka nje, roho za korosho zinatudidimiza sana!
Unazidi kunitonesha tu
Inauma sana wakati mwingine huwa nasema ningekuwa mimi nisingewanyang'anya watu mashamba yao bali ningewaambia wazungushie uzio na kufuga swala na digidigi
Kweli sio utani nimeona wazungu UK wamebeba wanyama wetu na kuwafungia fence wakizaliana wanauza

Sasa sisi ukifuga kobe unaulizwa kibali wakati ni utajiri wetu ambao wanatakiwa watu wa kutumia akili na kuboresha namna ya kupata faida

Mkuu hilo la washonaji ni kweli, hivi Bangladesh wanatushinda kwa kitu gani angalia wwlivyo duni lakini ndio wanatengeneza nguo %kubwa zinauzwa kwenye maduka makubwa duniani
Hatuwezi kuwa wasindikizaji tu

Sent from my SM using Tapatalk
 
Unazidi kunitonesha tu
Inauma sana wakati mwingine huwa nasema ningekuwa mimi nisingewanyang'anya watu mashamba yao bali ningewaambia wazungushie uzio na kufuga swala na digidigi
Kweli sio utani nimeona wazungu UK wamebeba wanyama wetu na kuwafungia fence wakizaliana wanauza

Sasa sisi ukifuga kobe unaulizwa kibali wakati ni utajiri wetu ambao wanatakiwa watu wa kutumia akili na kuboresha namna ya kupata faida

Mkuu hilo la washonaji ni kweli, hivi Bangladesh wanatushinda kwa kitu gani angalia wwlivyo duni lakini ndio wanatengeneza nguo %kubwa zinauzwa kwenye maduka makubwa duniani
Hatuwezi kuwa wasindikizaji tu

Sent from my SM using Tapatalk
Daah..., hahahah, yaani kobe wanauliza kibali, tutatoboa kweli?
 
Daah..., hahahah, yaani kobe wanauliza kibali, tutatoboa kweli?
Yaani
Unajua sio wote wasiojua bali wapo wenye idea nyingi ila wanakwamishwa na watu wachache ambao wanashindwa kujifunza kwa wengine

Hebu kaulize unataka kupeleka nyanya au maembe ulaya usikie mziki wake
Acha tu

Sent from my SM using Tapatalk
 
Mpaka tuje kufikia huko aisee. Hatari sana.

17e92f2b492c0b788aa55c396f4657669b127d0d.png


MATAGA.
 
Hapa bongo, hasa kipindi cha mkapa na kikwete Wageni walikuwa wanapewa kipindi cha kutolipa kodi huku wazawa wakilipa hata kabla hawajaanza biashara.
 
 
Katika juhudi ya kukuza viwanda vya ndani vya magari, serikali ya nchini Ghana imeipa likizo ya kodi ya miaka 10 kampuni ya kutengeneza magari ya mtume Osafo Kantanka ijulikanayo kama KANTANKA MOTORS. Hatua hii inalengo la kuiwezesha Ghana iweze kushindana na kampuni za magari toka Ulaya, Asia na Marekani, pia inafikiria kupiga tozo kubwa zaidi kwa magari toka nje ili kuvutia wanunuzi wa ndani. Pia serikali imeweka mkakati wa kuacha kuagiza magari toka nje ya nchi na badala yake wameanza kunua magari yanayozalishwa ndani kwani imebainika ni imara, yana muonekano nadhifu na yanadumu kuliko yale ya Japana na Marekani, poa hatua hii inalengo la kupunguza tatizo la ajira nchini Ghana.
Mambo kama haya ni ya kuigwa na kupigiwa mfano, najiuliza tu, kama kweli serikali yetu inania ya kukuza viwanda vya ndani, inawezaje kuagiza mabuti na sare za jeshi toka China huku maelfu ya vijana waliosomea ushonaji wakiwa hawana ajira, hivi kweli huwa tunatumia kiungo gani cha mwili kufikiri? Msaada tafadhali; video inamaelezo ya ziada.




Mboma mwonekano ni kama wameiga wa toyota
 
Back
Top Bottom