TANESCO yapata Mshindani. Kampuni ya TAQWA-DALBIT yapewa tenda ya kuzalisha na kusambaza umeme Migodini

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,053
49,736
Serikali kupitia Wizara ya Madini imeanza mazungumzo na Kampuni ya TAQWA-DALBIT kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa upatikanaji wa nishati ya umeme migodini na maeneo yenye wachimbaji wadogo ili kuchochea shughuli za uchimbaji madini nchini Tanzania.

Mazungumzo hayo yamefanyika Februar 14, 2024 Jijini Dodoma na kuongozwa na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde na Naibu Waziri Madini Mhe. Dkt. Steven Kiruswa pamoja na Menejimenti ya Vongozi wa Kampuni ya TAQA-DALBIT ikiongozwa na Meneja Mkuu Ndugu Amr Aboushad na Mkurgenzi wa maendeleo ya Biashara Ndugu Raphael Banzi.

Akiwasilisha maelezo ya awall, Nougu Amr Aboushad alisema kwamba kampuni yao ipo tayari kuja na mpango wa uzalishaji wa umeme kupitia gesi kwa kufunga mtambo katika migodi na maeneo ya wachimbaji ambayo itasaidia kupunguza gharama za uzalishaji kwa zaidi ya nusu ya gharama inayotumika hivi sasa kupitia matumizi ya mafuta ya dizeli na petroli na awamu ya pili itahusisha uzalishaji wa umeme kupitia mfumo wa umeme jua ambapo Kampuni itafunga mtambo mkubwa kwa gharama yao na kuwaunganisha wachimbaji wadogo kwa malipo ya mwezi ya matumizi ya nishati hiyo.

Akizungumza katika mkutano huo, Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde ameishukuru Kampuni ya TAQA-DALBIT kwa utayari wa kutatua changamoto ya upatikanaji wa nishati ya umeme migodini na kuagiza uongozi wa Wizara kuitisha mkutano wa haraka na wadau wote wakiwemo wachimbaji wadogo na wakubwa ili kupata fursa ya kujadiliana namna bora ya utekelezaji wa mpango huu.

Utekelezaji wa mango hu utasaidia sana kuchochea shughuli za chimbaji chini Tanzania na hivyo kuongeza uzalishaji wa madini.

===

Serikali Kupitia Wizara ya Madini imeamua kuachana na Tanesco na kutafuta mzalishaji na msambazaji wa umeme migodini.

TAQWA-DALBIT Wamesainiana MoU na Wizara ya Madini kuanza kazi hiyo.

Maoni Yangu.
Binafsi sikubaliani na hii Kwa sababu huenda ikawa ni Mpango wa Wanasiasa kujinufaisha na kudidikiza Tanesco Kwa makusudi.

Kwa nini makubaliano yafanyike Sasa wakati bwawa linaenda kukamilika na umeme wa bwerere utakuwepo?

Pili migodi na viwanda ndio sehemu ya uhakika Kwa Tanesco kupata pesa kuliko Kwa individuals consumers ambao Kwa mujibu wa Tanesco wanauziwa umeme Kwa bei ya ruzuku,Je hii sio hujuma ya makusudi?

Tatu, Kwa nini hao TAQWA-DALBIT wasipewe tender ya kujenga miundombinu huko kwenye migodi eg distribution lines Ili kurahisishia Tanesco kuunga umeme?

Kuna harufu ya Ufisadi na Wanasiasa kujinufaisha.Bunge kataeni hili Dili haramu.
 
Mbona migodini tu... Ilitakiwa Tanesco wapate challenges za makampuni binafsi ya kusambaza umeme nchi nzima ili kuua hii monopoly yao...

Wanazingua sana walahi! 😡😡
Wapi kwingine ambako umeme unazalishwa na Kusambaza na kampuni binafsi?

Umeme ni issue ya national security
 
Kwa nini makubaliano yafanyike Sasa wakati bwawa linaenda kukamilika na umeme wa bwerere utakuwepo?

Pili migodi na viwanda ndio sehemu ya uhakika Kwa Tanesco kupata pesa kuliko Kwa individuals consumers ambao Kwa mujibu wa Tanesco wanauziwa umeme Kwa bei ya ruzuku,Je hii sio hujuma ya makusudi?

Tatu,Kwa nini hao TAQWA-DALBIT wasipewe tender ya kujenga miundombinu huko kwenye migodi eg distribution lines Ili kurahisishia Tanesco kuunga umeme?
Kuna sura na baadhi ya viungo vya mwili husema na kutoa taswira halisi ya mambo yanayoendelea
Screenshot_20240217_070955_Samsung Internet.jpg
 
Wapi kwingine ambako umeme unazalishwa na Kusambaza na kampuni binafsi?

Umeme ni issue ya national security
Mkuu kama ni swala la Nation Security! Mbona tuna makampuni binafsi ya kutoa huduma ya mawasiliano ambao ni competitors wa TTCL chini ya sera na usimamizi wa TCRA? Em nambie kati ya huku kwenye nishati ya umeme na huku kwenye mawasiliano ambapo ndiyo pame dominate technologies za nchi nyingi wapi ni easy Nation Security kua compromised?

Tuache kutetea madudu! Zitungwe sera zitakazo simamia hayo makampuni binafsi za kuzalisha na kusambaza umeme kama yakijitokeza, hamna kinachoshindikana hapa chini ya jua kali hili..
 
Mkuu kama ni swala la Nation Security! Mbona tuna makampuni binafsi ya kutoa huduma ya mawasiliano ambao ni competitors wa TTCL chini ya sera na usimamizi wa TCRA? Em nambie kati ya huku kwenye nishati ya umeme na huku kwenye mawasiliano ambapo ndiyo pame dominate technologies ya nchi nyingi wapi ni easy Nation Security kua compromised?

Tuache kutetea madudu! Zitungwe sera zitakazo simamia hayo makampuni binafsi za kuzalisha na kusambaza umeme kama yakijitokeza, hamna kinachoshindikana hapa chini ya jua kali hili..
Server za mawasiliano ziko Bongo na wanaweza kuzimonitor.
 
Naona mafisadi wameanza kufanikiwa Baada ya kuiamuru Tanesco wakatekate umeme bila ya sababu hatimaye wamepata walichokitaka

Baada ya mwaka utasikia Tanesco wanawalipa hao jamaa million 200 Kwa saa ukifuatilia wamiliki wa hiyo kampuni utagundua ni watanzania wenzetu wapiga Dili

R.I.P Magufuli
 
Wapi kwingine ambako umeme unazalishwa na Kusambaza na kampuni binafsi?

Umeme ni issue ya national security
Kama Ni ivyo Ni Bora tu mzungu ama Africans have to recolonize so that we wake up to know how to serve people instead of self interests.
Ukisema viongozi utajiri walio nao waonyeshe mchakato wa kila kitu walivyokipata Bali Ni kuwa wameua mama wajazito na watt kibao Mana ambulance ilikosa,ama road ilikuwa mbaya,ama dawa zilikosekana, ama watalaamu hawakuwepo,pia Kuna watu walishindwa Soma Sayansi Mana mazingira sio rafiki hakuna walimu,madarasa sio mazuri.pia Kuna watoto walifariki walipata kipindupindu na watu wazima pia Mana hawakupata maji salama na Safi kwa matumizi ya nyumbani.
Ila huyu mtu akachukua nguvu za wananchi wake waliomuamini kuwa awaongoze akasaini mktaba kwa ajili yake,akanunua nyumba new York.
Baadaye anahalalisha wizi kuwa ndio usomi,kula kwa kalmu
 
Hii ndo hasara ya ajira za michongo michongo kwenye mambo ya msingi moja wapo ni umeme,maji na afya,

mm na imami kubwa kufeli kwa hii sector wachia wizi ni pamoja kuwa na watishi wa mchongo
 
Mwendelezo wa Giving a Dog a Bad Name so you can Kill it...

Kwahio hao so called wadau wanapewa creme de la creme ili Tanesco iendelee kuhangahika huko in the middle of no where ?!!! Hili nilishaliona kitambo na linakuja Tanesco itauzwa na watu kujichukulia ma-share na huduma kuendelea kuwa mbovu....



 
Hii nchi inabidi mungu atuangamize wote harafu kije kizazi kingine,kizazi kibaya sana,ukichunguza kinachofanya hii nchi isisonge ni viongozi wetu,baadhi yao ni watu wabaya sana,nasikia kuna mwingine ana jumba dubai,kapataje pesa,yeye tu ndo imejulikana,vipi wengine,viongozi tunawaomba sana kuweni na upendo na nchi yenu,tunapenda sisi watanzania tutembee vifua mbele na tuwe na cha kuwajibu nchi jirani zetu kuwa hamuezi kupata viongozi kama wa kwetu,tunataka wawatamani viongozi wetu na waombe mngekuwa kwao,sasa tuambieni lini mtaacha mabaya yenu na kujenga nchi,maana hamjaanza hata kuanza
 
Tanesco ni shirika namba moja nchini Tanzania katika usafirishaji wa nishati ya umeme, haina mpinzani !
 
Back
Top Bottom