Kampeni za Urais, ubunge na Udiwani 2025 kwanini zimeanza kabla hata mwaka haujaisha? Lini tutawaza kuhusu waliowapa kura?

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
539
3,507
Kuna Vita kubwa ndani ya chama cha Mapinduzi kuhusu uchaguzi wa 2025, Vita hii imekuwa kali ikamfanya Mhe. Rais kutangaza nia mapema. Baada ya kutangaza nia mapambano yamekuwa makali kwenye majimbo na kata kundi la utawala uliopo likitaka kuwaondoa waliowekwa na utawala uliopita.

Huko Mbeya/ Songwe tumesikia mapambano ya Mbunge na Kiongozi wa chama, huko Arusha hali ni mbaya, ukienda Kanda ya ziwa napo panafukuta macho. Kundi lililopewa madaraka nje ya uchaguzi halali lipo hatarini kupukutika kwa mbinu mbalimbali ili wale wanaoamini wanakubalika na wapiga kura wapewe nafasi.

Najiuliza, tulisema hakuna siasa baada ya uchaguzi tukasema upinzani unachelewesha maendeleo. Leo hii upinzani ndio wanaopiga kampeni au sisi wenye madaraka ndio tunaoangaika na madaraka ya miaka mitano mbele? Kama tunawaza 2025, leo ni 2021 tunaamini tutawatumikia wananchi au tutawatumikia wenye dhamana yakututeua tugombee 2025?
 
Unajitengenezea taharuki isiyokuwepo mkuu wangu.

Hakuna sehemu mh.Rais na mwenyekiti wa CCM ameanza kampeni.

Kama mwenyekiti anayekijua vyema chama chake, kutokana na kilichotokea na kumfanya yeye apande nafasi moja kumepelekea KUTOA KAULI ILE ili tuendelee kuchapa kazi....ili kusiwe na "power struggle" kabla ya 2025.

Kama mwanachama hakika ninampongeza sana mwenyekiti wetu mh.SSH kwa kukituliza chama ili tuitekeleze ilani yetu iliyotuingiza madarakani 2020!

SIEMPRE MWENYEKITI CHIFU MKUU HANGAYA💪👍🤣🙏

#NchiKwanza
 
Walipewa kura au waliiba kura hawa ccm,kuna tofauti kubwa sana hapo na wewe middle class unakuja na uzi huu kuhalalisha haramu ile,ogopa imani yako
Huna ushahidi kuwa CCM iliiba kura...hunao huo zaidi ya ushabiki tu
 
Unajitengenezea taharuki isiyokuwepo mkuu wangu.

Hakuna sehemu mh.Rais na mwenyekiti wa CCM ameanza kampeni.

Kama mwenyekiti anayekijua vyema chama chake, kutokana na kilichotokea na kumfanya yeye apande nafasi moja kumepelekea KUTOA KAULI ILE ili tuendelee kuchapa kazi....ili kusiwe na "power struggle" kabla ya 2025.

Kama mwanachama hakika ninampongeza sana mwenyekiti wetu mh.SSH kwa kukituliza chama ili tuitekeleze ilani yetu iliyotuingiza madarakani 2020!

SIEMPRE MWENYEKITI CHIFU MKUU HANGAYA💪👍🤣🙏

#NchiKwanza
2020 hapakuwa na uchaguzi. Hata wanaccm wanatamani urudiwe.

Samia mwenyewe anatamani siku ziende kasi apate uchguzi.

Huko madiwani na wabunge ndio usiseme. Ndio maana watu wana hamu na uchaguzi wakati uliopita hata mwaka bado
 
Kuna Vita kubwa ndani ya chama cha Mapinduzi kuhusu uchaguzi wa 2025, Vita hii imekuwa kali ikamfanya Mhe. Rais kutangaza nia mapema. Baada ya kutangaza nia mapambano yamekuwa makali kwenye majimbo na kata kundi la utawala uliopo likitaka kuwaondoa waliowekwa na utawala uliopita.

Huko Mbeya/ Songwe tumesikia mapambano ya Mbunge na Kiongozi wa chama, huko Arusha hali ni mbaya, ukienda Kanda ya ziwa napo panafukuta macho. Kundi lililopewa madaraka nje ya uchaguzi halali lipo hatarini kupukutika kwa mbinu mbalimbali ili wale wanaoamini wanakubalika na wapiga kura wapewe nafasi.

Najiuliza, tulisema hakuna siasa baada ya uchaguzi tukasema upinzani unachelewesha maendeleo. Leo hii upinzani ndio wanaopiga kampeni au sisi wenye madaraka ndio tunaoangaika na madaraka ya miaka mitano mbele? Kama tunawaza 2025, leo ni 2021 tunaamini tutawatumikia wananchi au tutawatumikia wenye dhamana yakututeua tugombee 2025?
fanyeni na nyie, CCM haiwezi gawanyika kamwe
 
Halafu ile takataka inayojiita chief Hagaya ndiyo ilizundua huu ujinga kwa kutangaza nia.Hana hata habari kuwa anapaswa kuwafanyia nini wananchi.She is hopeless inept autocratic!
 
Back
Top Bottom