Jamani! Hawa wangeendelea na masomo. CCM hawana huruma, wanakatisha vipindi kupeleka wanafunzi kwenye kampeni ya JK, ingekuwa Dr Slaa angeonekana amekiuka sheria.
Jamani! Hawa wangeendelea na masomo. CCM hawana huruma, wanakatisha vipindi kupeleka wanafunzi kwenye kampeni ya JK, ingekuwa Dr Slaa angeonekana amekiuka sheria.
Watetezi wa haki za watoto wa shule tunzeni hii picha. Katika kesi kibao zitakazofunguliwa dhidi ya mafisadi wa ccm, hii ya kulazimisha watoto wa shule kwenda kwenye mikutano ya kampeni ya ccm itakuwa kwenye top ten:
mimi nimeanza kuichukia ccm miaka ya 1982 na kuendelea na kwa utoto wangu wakati ule tulikuwa tunahudhuria sana hivi vitu, kwa maandamano tena enzi za mchonga. emagine mnatoka shuleni saa tatu uwanjani mnafika saa nne au tano, mnashinda uwanjani mpaka saa tisa ndo mgeni rasmi aje. hapo mmeshinda njaa,kiu ya maji. hiyo kitu sikuipenda kabisa na nakumbuka nilipewa magwanda ya chipukizi enzi zile ipo moto nikayakataa. kwa kweli ccm mnatesa wanafunzi siwapendi kabisaaaaaaaa
Hapa ni Ilula, wanafunzi ni wa shule ya Changa kabisa, iliyotoa F.IV ya kwanza mwaka huu. Shule changa kama hizi, wanapotezewa muda wao wa masomo eti tu wakaongeze idadi wa watu kumdanganya JK! Walionelewa sana. Maskini pia wale watoto wa shule za msingi, hawajui lolote katika upigaji wa kura, wanakatishwa masomo yao hivi hivi!!!