Kizimkazimkuu
JF-Expert Member
- Nov 8, 2007
- 337
- 234
Nimeelezwa na jamaa aliyekuwapo uwanja wa mashujaa Moshi katika kampeni za JK Moshi kuwa hali haikuwa kama picha zilizoonyeshwa TBC1 ktk taarifa za habari. Ukweli ni Kuwa CCM walitangaza kuwa mkutanno ungeanza saa 8 lakini BURUDANI ZITAANZA KUANZIA SAA TANO ASUBUHI. Umati ulijaa kuona burudani na ze Comedy na Mkuu aliingia saa 11 jioni badala ya saa 8. Alipoanza tu hotuba, watu wengi wakaanza kutawanyika. Jamaa akaniambia kama nilikuwa makini ningeangalia picha, ni obvious ile picha ilikuwa edited. Ilikuwa ikimuonyesha Kikwete kutokea mbele na then crowd bila kuewa na picha iliyoweka view ya Kikwete na crowd yote similarly kama wanavyofanya kwa SLAA (siku wakipenda) wanamuonyesha pekee yake then wanachagua angle yenye watu wachache na watoto.Lakini hali ya kisiasa CCM wana hali mbaya HAI (Mh.Fuya Kimbita), SIHA (Agrey Mwanri) na Moshi mjini (Justin Salakana). Hapa Ndesamburo kaahidiwa na vijana kuwa kura watampa but awaache tu wapeperushe bendera na mabango ya CCM, Wanahasira mno na kukatwa jina la mfanyabiiashara ''mtoto wa mjini'' Athumani Ramole (Buni).