PreGE2025 Kampeni ya mama asemewe kuandaa kongamano kubwa la wanavyuo Dodoma kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025

PreGE2025 Kampeni ya mama asemewe kuandaa kongamano kubwa la wanavyuo Dodoma kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Kampeni ya Mama Asemewe chini ya Mwenyekiti wake Ndg. Geofrey Kiliba, imeandaa kongamano kubwa la wanavyuo kutoka Vyuo mbalimbali mkoani Dodoma, litakalofanyika tarehe 29 Machi 2025 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre.

Kongamano hilo linalenga kuwakutanisha wasomi kwa ajili ya kujadili na kuweka maazimio ya pamoja kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, likiwa ni sehemu ya juhudi za kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika mchakato huo wa kidemokrasia kwa msingi wa uelewa na uzalendo kwa taifa.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Ndg. Kiliba, kama kiongozi wa kampeni ya Mama Asemewe ataongoza mchakato wa maazimio hayo, ambapo wanavyuo watatoa mtazamo wao kuhusu mustakabali wa Tanzania na namna vijana wanavyoweza kushiriki katika kujenga taifa imara kupitia uchaguzi huu muhimu wa mwaka 2025
 
Uwakumbushe na hii isomeke "Deni la Mama lafikia trillions 97
IMG-20250327-WA0055.jpg
 
..pia kongamano la "No Reforms No Elections" linakuja kwa wanavyuo.
 
Kwanini nilizaliwa kwenye hii nchi?! Enhee Mungu nisaidie niweze kuhama hii nchi Tafadhali.
 
Wasomi mnatumika tu ..vijana wadogo na ndoto zenu
Wakishapata wanachokitafuta mnatupwa
Nendeni Veta mjiajirini🤣🤣🤣
Mtu na degree/ masters yako ulosotea miaka nenda Rudi..🤣
 
Hili limeniliza sana, 😢😢😢
Lia sana.
Ripoti ya CAG inonesha ninkwa namana gani nchi inaendeahwa Kwa hasara,mashirika ya umma ni hasara tup.ttcl hasara,atcl hasara,trc hasara,tanesdsco hasara....bado kwinginw hakuna unafuu.
Biashara unayoiendesha Kwa hasara unaweza ongeza wafanyakazi?
Unaweza ajiri wafanyakazi zaidi?
Utawalipa Nini kama unavhoambulia ni hasara tu
Ni vijana waanagapi watasota mtaani Kwa kukosa ajira Kwa uendeshaji wa kimazoea Kila mwaka hasara....

Badala ya kusikitishwa na kinachoendelea,hata kukemea alishindwa.
Nendeni mkapigie kampeni
 
Back
Top Bottom