Sir R
JF-Expert Member
- Oct 23, 2009
- 2,175
- 298
Rais JK alipokuwa anawahutubia wazee wa Dar es salaam (CCM) alisema wazi kuwa hajali kura za wafanyakazi yaani yuko tayari kukosa kura 350000 za wafanyakazi. Ni kauli iliyojaa kiburi, ubabe na kejeli
Nilishangazwa sana na ujasiri wa JK kwani najua atakuwa mgombea wa urais october mwaka huu, nilifikiri angechagua maneno ya kusema wakati huu tunapoelekea october.
Nimeamua kuwahamasisha wafanyakazi wenzangu kumnyima JK na CCM kura mwaka huu. Vile vile nimeona hiyo haitoshi, kila mfanyakazi ajitahidi kutafuta si chini ya watu 50 watakaomnyima JK na CCM kura kwa kumpa mgombea wa upinzani, tujifunze kwa waingereza, Godon Brown alimkejeli Bi kizee mmoja na watu wakamfundisha nidhamu.
Kila atakayesoma ujumbe huu amtumie mwenzake hasa mfanyakazi,
Ewe mfanyakazi popote ulipo hamasisha watu kushiriki uchaguzi mwaka huu na wasiwape wagombea wa CCM na JK wao kwani kauli yake ni matusi kwa wafanyakazi na watanzania kwa ujumla.
Wafanyakazi tushiriki katika KAMPENI YA KURA 50+ tutabadilisha historia ya nchi.
Nakaribisha michango itakayoleta mabadiliko.
NAKUPENDA EWE TANZANIA
Nilishangazwa sana na ujasiri wa JK kwani najua atakuwa mgombea wa urais october mwaka huu, nilifikiri angechagua maneno ya kusema wakati huu tunapoelekea october.
Nimeamua kuwahamasisha wafanyakazi wenzangu kumnyima JK na CCM kura mwaka huu. Vile vile nimeona hiyo haitoshi, kila mfanyakazi ajitahidi kutafuta si chini ya watu 50 watakaomnyima JK na CCM kura kwa kumpa mgombea wa upinzani, tujifunze kwa waingereza, Godon Brown alimkejeli Bi kizee mmoja na watu wakamfundisha nidhamu.
Kila atakayesoma ujumbe huu amtumie mwenzake hasa mfanyakazi,
Ewe mfanyakazi popote ulipo hamasisha watu kushiriki uchaguzi mwaka huu na wasiwape wagombea wa CCM na JK wao kwani kauli yake ni matusi kwa wafanyakazi na watanzania kwa ujumla.
Wafanyakazi tushiriki katika KAMPENI YA KURA 50+ tutabadilisha historia ya nchi.
Nakaribisha michango itakayoleta mabadiliko.
NAKUPENDA EWE TANZANIA