mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,076
- 4,113
Katika hafla inayoendelea sasa hivi Ikulu ya Utiaji saini kati ya Tanzania na Barrick Gold, Profesa kutoka Jalalani akiwa anatoa hotuba yake bila tashwishwi amedai kwamba alitumwa kazi na Rais Magufuli lakini kazi ile hakufanikiwa na ikawa fedhaha kubwa kwake kwa kutumwa kazi na Rais na kushindwa kuitekeleza, hivyo alichukua maamuzi ya kumwandikia Rais barua ya kujiuzulu lakini kabla hajaifikisha sehemu husika akawa amepokonywa.
Nanukuu
“
Katika kujadili mikataba 9 itakayosainiwa leo, hicho kipindi kilikuwa kigumu. Hawakuwa hawa, walikuwa wenzao hawapo hapa. Sipendi kuwataja majina ila hawakutaka mikataba hii isainiwe na tufanikiwe. Kila tulipokutana na kukubaliana kesho yake walibadilika
Ilifika mahali Rais nilitaka kuingiwa na dhambi ya kukata tamaa na vitimbi hivyo vilishia kwa wao wenyewe kufukuzana kazi. Leo nataka kumshukuru Luteni Kanali Mstaafu Richard William
Tulipofika kukata tamaa, Rais nilikuwa nimendika barua ya kujiuzulu kuja kwako. Kwamba kazi uliyonipa imenishinda. Aibu hii na fedheha hii nitaibeba. Barua hiyo sikuileta maana Casmir Simba Kyuke alininyang'anya na kuichana
Nilisema sijawahi kutumwa kazi na Mkuu wangu wa nchi nikashindwa, ila sasa hawa watu hawataki. Rais unaniuliza mnakwendaje, mbona nasikia hamuendelei! Namjibu tunaendelea huku najua hatuendelei.Ndipo nilipowapigia Maaskofu wangu wa Anglikana.
Nanukuu
“
Katika kujadili mikataba 9 itakayosainiwa leo, hicho kipindi kilikuwa kigumu. Hawakuwa hawa, walikuwa wenzao hawapo hapa. Sipendi kuwataja majina ila hawakutaka mikataba hii isainiwe na tufanikiwe. Kila tulipokutana na kukubaliana kesho yake walibadilika
Ilifika mahali Rais nilitaka kuingiwa na dhambi ya kukata tamaa na vitimbi hivyo vilishia kwa wao wenyewe kufukuzana kazi. Leo nataka kumshukuru Luteni Kanali Mstaafu Richard William
Tulipofika kukata tamaa, Rais nilikuwa nimendika barua ya kujiuzulu kuja kwako. Kwamba kazi uliyonipa imenishinda. Aibu hii na fedheha hii nitaibeba. Barua hiyo sikuileta maana Casmir Simba Kyuke alininyang'anya na kuichana
Nilisema sijawahi kutumwa kazi na Mkuu wangu wa nchi nikashindwa, ila sasa hawa watu hawataki. Rais unaniuliza mnakwendaje, mbona nasikia hamuendelei! Namjibu tunaendelea huku najua hatuendelei.Ndipo nilipowapigia Maaskofu wangu wa Anglikana.