Kambi ya Jeshi uraiani ni kosa

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,605
8,743
Mimi nimeshangazwa ni kwanini kambi ya jeshi yenye mabomu imejegwa uraiani??
 
Hata mimi nemeshangaa raia wamejenga kuizingira kambi yajeshi ,nafikiri wanainyemelea ili kurahisha kuiibia.
Labda tuulize Yai na kuku nani alikuja mwanzo ,kila mmoja huenda akadai alimkuta mwenziwe watu wenyewe waBongo wananunua ubishi :D
 
NIJUAVYO NA NDHANIVYO MIMI , NI KUWA KAMBI HUJENGWA PEMBEZONI SANA NA MIJI......lakini sisi raia huisogelea na kukuta tumeizunguka pande zote......!
 
NIJUAVYO NA NDHANIVYO MIMI , NI KUWA KAMBI HUJENGWA PEMBEZONI SANA NA MIJI......lakini sisi raia huisogelea na kukuta tumeizunguka pande zote......!

Kuna watu wa kusimamia sheria tunawalipa mishahara wanafanya kazi gani? Mambo ya buffer zone kwao hayapo? Layman wakati wote bila kuelekezwa na kusimamiwa ipasavyo atakiuka tu taratibu hivyo ni wajibu wa vyombo husika kuhakikisha sheria na taratibu zinafuatwa.
 

Attachments

  • mbagala.jpg
    mbagala.jpg
    114.4 KB · Views: 58
Mimi nimeshangazwa ni kwanini kambi ya jeshi yenye mabomu imejegwa uraiani??

Kambi hizi zilijengwa zamani sana, nyakati hizo raia walikuwa mbali na kambi, this applies to viwanda vya urafiki, wazo hill nakambi zingine nyingi za jeshi.

May be hatukuwa na wataalam wa kukadiria kuwa mji wa DSM utakuwa kawa kasi. katika document moja ya kiwanda cha urafiki inasomeka; '' kiwanda kiko nje kidogo ya mji!''

Nadhani yafanyike mabadiliko a kuyahamisha haya makambi na kuwaka sheria za kuzilinda , ili raia wasiende kujenga karibu nayo.NASHANGAZWA NA WATAALAM WA JESHI SIKU ZOTE WAKO WAPI, KUWAZA HIVI, JAPO WATU WAMESEMA SANA.

HII PIA INAIWEKA TANESCO UBUNGO KUWA IKO ENEO AMBALO AIDHA HAITAKIWI, AU RAIA WAHAME! MAANA LILE NALO NI BOMU!
 
Miaka 10 iliyopita mbagala lilikuwa pori kubwa sana, miaka 5 baadae watu wakawa wanauziwa viwanja na serikari za mitaa wakawa wavidhibitisha kuwa ni viwanja halali then unaenda mwenyewe ardhi kupata hati. kwahiyo basi mlolongo wote huu nikwamba serikali ilikuwa inajua kuwa mbagala kunapanuka kwa haraka maana mashamba yaliokuwa yanauzwa ukikuta ghali sana ni laki 3, hivyo watu wengi walinunua na kuaza kujenga wengine wakafanya mashamba. Nawalio wengi wasiojua athari za kujenga karibu na Jeshi wao waliona ni advantage kwasababu ya security maana walio wengi wanaamini maeneo ya jeshini vibaka ama wezi ni wachache sababu ya kuogopa wanajeshi kwa kipigo ama mataso watakayo pewa punde wanapokamatwa.
Lakini kama serikali ama wizara ya ulinzi ingekuwa inatowa mafunzo ya kuelewesha wananchi athari na faida za kuwa na makazi kenye kambi yeyote ya jeshi sidhani kama tungekuwa na kilio kikubwa hivi kila raia angeopa kujenga maeneo ya jeshi.
 
Hii ya Mbagala iwe funzo kwa Taifa kwa ujumla, na kuna kambi nyingi sana zimezungukwa na makazi ya watu, Ukonga asilimia kubwa ni Jeshi kuna Kikosi cha anga, Magereza na FFU ukija kawe kuna JKT, Lugalo JWTZ, Mgulani JKT, kigamboni ni kikosi cha wanamaji, na vyote hivyo vimezungukwa na raia sasa tuliulize je ikitokea bahati mbaya kama ya mbagala itakuwaje. Na sehemu nyingi za makambi hayo ujenzi wake ni holela na watu ni mwengi nikimaanisha makazi ya watu wengi sana kutofautisha na sehemu nyinginezo.
Ukija Wazo kiwanda cha saruji na chenyewe ni bomu kubwa tu, hapo turudi nyuma kidogo miaka ya mwanzoni mwa 90's kulikuwa pori kubwa hasa tena la kutisha hata njia yenyewe ilukuwa ni mbinde kupita kipindi cha mvua lakini sasa ni kama uzunguni kuna nyumba za kufa mtu barabara zimechongwa vilivyo zinapitika kipindi chote, na sio kuwa waliojenga huko ni kina mbavu mbili lahasha ni watu wenye vijisenti vyao vya uhakika na wanaelewa madhara ya kile kiwanda kiafya na mazingira.

Ukija Tanesco pale Ubungo ile mitambo nayewe siku ya siku ikijibu sijui tutamlaumu nani, mitambo imezungukwa na makazi ya watu wengi mno.

Nina swali moja tu : Je! watu wote waliojenga maeneo hayo hatarishi wapelekwe wapi?


Ushauri wangu kwa Serikali yetu itowe mafunzo au Elimu kwa wananchi.
 
ukweli ni kwamba nasi pia tulitamani kuishi mjin lakini bahati mbaya kulikuwa kumekwishaa jaa na hata ukikipata kiwanja uwezo wa kukinunua inakuwa ni ishu kwa hela zetu za madafu ndio maana tukakimbilia huko maana enzi hizo kulikuwa ni porini hiyo ilikuwa ni 2001 na kulikuwa hakuna vurugu za mjini yaani full amani
 
Back
Top Bottom