changamoto ambazo zinapaswa zifanyiwe kazi. Kwa mfano,
bado matengenezo ya vituo vya kupandisha abiria na vibanda vya tiketi hayajakamilika,
eneo la kupishana treni za TRL lililopo Buguruni ambapo treni moja ilishindwa kufanya kazi juzi.
tatizo la maegesho ya magari ili wenye magari wayahifadhi na kupanda treni kwenda katikati ya Jiji.
Tiketi hazitoshi
wauzaji hawana chenji, hivyo abiria kupata kisingizio cha kusafiri bure.
kutokuwapo ulinzi wa kutosha na kanuni na taratibu za kuhakikisha usafiri huo unakuwa wa kistaarabu.
Ni matumaini yetu kwamba Waziri Mwakyembe ataona umuhimu siyo tu wa kupanua huduma hiyo ya usafiri wa treni kwa sehemu nyingi za Jiji, bali pia atahakikisha huduma hiyo inatolewa kwa wakati wote badala ya asubuhi na jioni kama ilivyo sasa. Tunamtakia kila la kheri.