Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje chini ya uenyekiti wa Edward Lowassa ipo ziarani Morocco.Waheshimiwa wetu hawa wakiwa huko wametoa msimamo unaofanana na ule wa Morocco lakini unaokinzana na ule wa serikali ya Tanzania kuhusiana na suala la Sahara Magharibi.
Kamati ya mambo ya nje imetoa msimamo na kudai Tanzania inaunga mkono Morocoo katika harakati zake kwa Sahara Magharibi wakati inavyofahamika ni kwamba Tanzania kwa maana ya serikali haiiungi mkono morocco kwenye suala hilo.
Swali:Je kamati ya bunge ya mambo ya nje inayo mamlaka ya kutoa msimamo kwa niaba ya serikali?kama hapana kuna ushawishi gani wamekumbana nao waheshimiwa hawa wakiwa huko morocco kiasi cha kuwalevya na kuamua kutoa msimamo huo ambao ni Tofauti na msimamo wa serikali?
Kwenye ile thread inayomuhusu Kitine, (https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...nje-ametia-mfukoni-mwake-kutafutia-urais.html) alisema kuwa Kuna waziri keshalamba kwa ajili ya kuiunga mkono Moroco. Sasa kamati baada ya kuona tayari jamaa keshalamba nao wakaona hakuna haja ya kufanya kama Serukamba na Nundu maana anaweza akaibuka Mnyika akaharibu. Hivyo nao wakaamua nao wachukue chao.
Unataka kutuambia Tanzania ina mtazamo tofauti na UN? au hujui alichokisema Lowassa?
"We are in perfect harmony with the U.N. resolutions and Tanzania is satisfied with the autonomy proposal to the southern provinces put forward by Morocco as a solution to the Sahara issue. We consider that the return of the Kingdom to AU can only encourage a swift settlement in its favor," said Lowassa.
Tanzania haijawahi kutangaza kuacha kuiunga mkono Sahara Magharibi katika kujitafutia uhuru toka Morocco. Pia siamini kama Kamati ya Bunge ina madaraka ya kutoa tamko kubwa kama msimamo wa taifa kuhusu mahusiano yake kimataifa!
Kama kweli ni migongano ya EL na Membe ndiyo chanzo cha hili tukio basi ni kithibitisho kibgine cha upumbavu wa jamaa zetu kwa kubeba siasa na misuguano yao hadi katika mambo ya kimataifa na kuaibisha taifa!
Kumbukumbu zangu zimepotea kidogo kwa kuwa jana sikupata kahawa: Hivi Tanzania si tulikuwa na wawakilishi wa POLISARIO miaka ya nyuma huko, je bado wapo?
Pia Morocco iliwahi kusimamishwa uanachama wa OAU by then kwa sababu ya hii Sahara Magharibi. Msimamo wa AU kwa sasa juu ya uhuru wa Sahara Magharibi ukoje?
hili hata mimi nimelisikia na nilikuwa nafuatilia; yawezekana ni katika kumgonganisha Lowassa na Membe. Watu wa Morocco wamekuwa wakjitahidi kutaka Tanzania ibadili msimamo wake wa kuunga mkono harakati za watu wa Western Sahara kuwa na uhuru wao, msimamo ambao kwa wanaoukumbuka ulikuwa ni mmoja kwa Nyerere.
Ndio sababu ya kuunga mkono Palestina, Polisario na Biafra kama ilivyokuwa kwenye kuunga mkono ANC na vyama vya ukombozi wa Afrika.
Naona Mama Shelukindo anacheka jino pembe. Nasikia alishajisalimisha kambini.
Naona Mama Shelukindo anacheka jino pembe. Nasikia alishajisalimisha kambini.
Naona Mama Shelukindo anacheka jino pembe. Nasikia alishajisalimisha kambini.
Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje chini ya uenyekiti wa Edward Lowassa ipo ziarani Morocco.Waheshimiwa wetu hawa wakiwa huko wametoa msimamo unaofanana na ule wa Morocco lakini unaokinzana na ule wa serikali ya Tanzania kuhusiana na suala la Sahara Magharibi.
Kamati ya mambo ya nje imetoa msimamo na kudai Tanzania inaunga mkono Morocoo katika harakati zake kwa Sahara Magharibi wakati inavyofahamika ni kwamba Tanzania kwa maana ya serikali haiiungi mkono morocco kwenye suala hilo.
Swali:Je kamati ya bunge ya mambo ya nje inayo mamlaka ya kutoa msimamo kwa niaba ya serikali?kama hapana kuna ushawishi gani wamekumbana nao waheshimiwa hawa wakiwa huko morocco kiasi cha kuwalevya na kuamua kutoa msimamo huo ambao ni Tofauti na msimamo wa serikali?
Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje chini ya uenyekiti wa Edward Lowassa ipo ziarani Morocco.Waheshimiwa wetu hawa wakiwa huko wametoa msimamo unaofanana na ule wa Morocco lakini unaokinzana na ule wa serikali ya Tanzania kuhusiana na suala la Sahara Magharibi.
Kamati ya mambo ya nje imetoa msimamo na kudai Tanzania inaunga mkono Morocoo katika harakati zake kwa Sahara Magharibi wakati inavyofahamika ni kwamba Tanzania kwa maana ya serikali haiiungi mkono morocco kwenye suala hilo.
Swali:Je kamati ya bunge ya mambo ya nje inayo mamlaka ya kutoa msimamo kwa niaba ya serikali?kama hapana kuna ushawishi gani wamekumbana nao waheshimiwa hawa wakiwa huko morocco kiasi cha kuwalevya na kuamua kutoa msimamo huo ambao ni Tofauti na msimamo wa serikali?