Kamati Kuu ya CCM kukutana Julai 04, 2015 saa nne asubuhi, Dodoma

Firauni mwenyewe shenzytype

ngosha, yamekuwa hayo? Kwani Lowasa kakulisha maharage ya wapi yale? Mshamgeuza nabii na uko radhi kumfia eti eeh! Kubalini tu yaishe kwani yote ni matokeo ila kulazimisha apitishwe tena na vitisho juu si sawa. Kila mgombea ana fursa sawa na msiulazimishe umma kumwamini na kumuunga mkono EL kwani ni sawa na kuyazuia mafuriko kwa mikono. Hafai na hana sifa za kuiongoza hii nchi kwa maana ya kushindwa kuutetea uwaziri mkuu na jimbo lake kuwa maskini wa kupindukia. Auchukie umaskini wa wanamonduli kwanza.
 
Kwa vigezo nilivyosikia akitaja Mangula .lowasa anaenguliwa saa 2 asubuhi labda wafanye mabadiliko ya kanuni.za chama chao ili kumpitisha kwa nguvu.
 
Wampitishe huyo fisadi Lowasa alietajwa kwenye Weakleaks, Ukawa tumnyoe hizo mvi
 
Ccm tutakutana mtaani awamu hii jandoni lazima mpitie walah tunawakata jando october.NA MAGOVI YENU LAZIMA TUWATIE SUNA NA KISU BUTU CHA NGALIBA.
 
Naomba kuelimishwa! Hivi fomu za kuomba udhamini zilikuwa kwa ajili ya wanachama 30 tu kwa kila mkoa (mikoa 15), ama zaidi? Je zilipo jaa, especially za ENL, je alirudi kuongeza zingine ama la?. Kama hakurudi kuongeza zingine, je, hizo za nyongeza alizidurufu ama alizi-photocopy?

Kama alizidurufu, je hazikuwa na serial number na kuwa issued serially na watu wa CCM HQ?

Kama zulikuwa na serial numbers, je hayo mafuriko ya wadhamini si "yatakuwa" yamerekodiwa kwenye fomu feki? (Najaribu kulinganisha na noti feki)!

Nielimishe usinitukane, nataka kujifunza tu!
 
Fuata maelekezo ya mtihani: Maelekezo yakisema zungushia herufi yenye jibu sahihi, wewe ukatoa maelezo ya jibu sahihi hata kama ni kweli hutapata.

Maelekezo ya Chama cha Mapinduzi yalisema ulete wadhamini 450 kutoka katika mikoa 15 ya Tanzania bara na mitatu Zanzibar, wewe unaleta wadhamini 200,000 ktoka mkoa mmoja.

Ina maana Mwenyekiti anatoa maelekezo kutoka kichwani mwake. Akiambiwa na mama Salma usiku basi, kesho maelekezo yanabadilika?

Kamati kuu(CC) labda wanakutana kwa ajili ya kupanga ratiba za Kampeni ya kukamilisha ratiba na wapinzani tu na kuangalia wajumbe watakaoshiriki kubariki jina la ENL, maana jina tayari lilishajulikana na ENL alishamaliza kampeni ndani ya Chama.

Watangaza nia wengine walidangany'wa kwamba wakati wa kutafuta wadhamini wasiwe na mikusanyiko ya watu wengi, kumbe ENL yeye alipewa maelekezo tofauti kwamba amalize kabisa na kampeni, ndiyo maana kigezo chake cha kuwa watu na wengi (Mafuriko yasiyozuiliwa kwa mkono) wakati wa kutafuta wadhamini ndiyo Kamati Kuu (CC) itatumia kama kigezo cha ENL kukubalika ndani na nje ya chama.

Watia nia wengine walie tuu, maana waliingia kwenye mtego, wakati Mwenyekiti wa Chama alishaelekeza kigezo kikuu ni kukubalika ndani na nje ya chama, maelezo ambayo ENL aliyafanyia kazi kwa asilimia 100, na ndicho kigezo pekee kitakachotumika. Kuna wagombea walipuuza kigezo cha Mwenyekiti, wakafuata maelekezo ya NAPE ambaye hakuna anayemsikiliza kwenye kikao cha CC.

POLENI WATIA NIA na HONGERENI kwa kuchangia chama, KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
Anayefikiria mgombea safi CCM, ni sawa na anayehangaika kutafuta hereni zilizotupwa dampo atajirike.
 
Back
Top Bottom