Kamati kuu CHADEMA kufunika Arusha Alhamisi

Kamati kuu CHADEMA kufunika Arusha Alhamisi

EasyFit

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2011
Posts
1,269
Reaction score
1,082
Chadema kimeandaa mkutano mkubwa wa hadhara mjini Arusha Alhamisi wiki hii utakao ongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Freeman Mbowe Kwa kushirikiana na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibroad Slaa, Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe na wajumbe wa CC.

Wajumbe wa CC watakaokwenda kuhutubia mkutano huo ni Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa; Mbunge wa Viti Maalum, Regia Mtema; Mwenyekiti wa baraza la Vijana Taifa wa chama hicho, Heche Suguta; Mbunge wa Viti Maalum, Chiku Abwao na Mbunge wa Nyamagana Ezekia Wenje.

Wengine ni Mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu wa kambi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu; Meya wa Manispaa ya Musoma, Kasululu Malima; Mwenyekiti wa Halmashauri ya Karatu, Lazaro Masai, na Mwenyekiti Manispaa ya Moshi, Jaffar Maiko. Pia atakuwapo Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na madiwani wengine wa Jiji la Arusha.

Madiwani waliofukuzwa

Kutoka kushoto: Estomih Mallah wa Kata ya Kimandolu, John Bayo wa Kata ya Elerai, Ruben Ngowi wa Kata ya Themi, Rehema Mohamed wa Viti Maalum na Charles Mpanda wa Kata ya kaloleni.

Source: Nipashe
 
Tunawatakia kazi njema Makamanda wetu wote watakaoongoza hizo Harakati zakulikomboa Taifa.Wito wangu kwa Wananchi wote wa Arusha nawaomba wajitokeze kwa wingi sana kama walivyojitoa siku walipo wahaga wale wananchi wenzetu watatu waliouwawa, safari bado ni ndefu hawa Wasaliti watano waliodondoka wasitukatishe Tamaa tuendeleze Umoja wetu na Mshikamano wa khali ya juu hasa katika kipindi hiki kigumu chakupigania Haki,kulilia Utu wetu na kufikia Ukombozi wa kweli wa Taifa letu tulipendalo.
 
Hivi alhamisi si bunge litakuwa linaendelea na majority naona ni wabunge inakuwaje hapa.
 
Hongereni MAKAMANDA WETU, PEOPLE'S POWER mpaka kieleweke!
 
Heri CC-Chadema inawajali wapiga kura wake inakwenda kuongea nao kuliko Nec-CCM na kina Nape kazi yao kuwavua magamba wenzao bila hata kuonana na wapiga kura kwenye majimbo husika.
 
Hapana sijalazimishwa isipokuwa wizi na uvunjifu wa amani.Hatutaki mabomu,majeruhi,vifo.

Unataka kufa kibudu, umezoea kupelekwa kikondoo kondoo? Ni uchaguzi wako Mungu akujalie. MAPAMBANO YANAENDELEA usiku, mchana, barabarani, wakati wa kazi, wakati wa faragha MPAKA KIELEWEKE
 
Mchalii wa A-Town mpoooo; wenzenu tunakuja kuwashika hao WACHUMIA TUMBO walioamua kiwasalitini nyinyi wapiga kura Arusha!!!
 
Hapana sijalazimishwa isipokuwa wizi na uvunjifu wa amani.Hatutaki mabomu,majeruhi,vifo.

Kwani Chadema wanamiliki mabomu?! au ndio mshajiandaa kuyalipua kwa kisingizio cha mkutano wa Chadema?!
 
Tunawasubiria sana hawa makamanda,pamoja kwa umoja na uadilifu tutalijenga taifa letu.
 
Heri CC-Chadema inawajali wapiga kura wake inakwenda kuongea nao kuliko Nec-CCM na kina Nape kazi yao kuwavua magamba wenzao bila hata kuonana na wapiga kura kwenye majimbo husika.
Well kama inawajali kwanini iende kuonana nao leo na si kabla ya kuwafukuza.
 
Natoa pongezi nyingi sana kwa maamuzi hayo mazito, mkutano wa hadhara ni muhimu hata kama polisi watazuia lazima ufanyike, hatuwataki MADIWANI wapiga DEAL. Waende CCM wakapatiwe kazi, mchezo wote uliochezwa na Pinda na JK hapo umefikia kikomo.

Diwani yeyote wa CDM atakayebainika kukisaliti chama ni OUT. Hatuogopi kwenda kwenye uchaguzi mdogo, hata kama ni Mbunge kapiga DEAL ni OUT.
 
Back
Top Bottom