Kamata kamata ya Polisi na kunyimwa dhamana. Ushauri wa bure kwa Rais Magufuli

kwa sasa hatuna kiongozi yeyote wa kukemea huu uvunjaji wa katiba unaoendelea. r.i.p mwalimu nyerere...
 
Kwa hali ilivyo sasa, ili kupiga hatua za maendeleo katika nchi yetu ni lazima kwanza rais awadhibiti wote wanaojaribu kuhatarisha hali ya usalama kwa matamko yasiyo na tija kwa maendeleo ya nchi yetu. Ifike mahala tuwe wakweli katika hili. Watu hawa wamekuwa hawana jema, kazi yao kubwa ni kupinga kila jambo linalofanywa na mheshimiwa rais Magufuli. Zaidi ya hayo wamekuwa wakitoa lugha za matusi na kejeli. Mtu waliyemwita fisadi kwa vinywa vyao leo hii kwao amekuwa mtakatifu, je watu hawa tuwaweke kwenye kundi gani? UFISADI ulipokuwa umeshamiri katika nchi hii walikaa kimya bila kuleta fyoko fyoko wala katangaza maandamano. Leo mheshimiwa rais Magufuli amejitahidi kwa kiasi kikubwa kupiga vita ufisadi, wao wanaanza kuleta fujo, kejeli na matusi. Je, watu hawa wana uchungu wowote juu ya nchi yetu? Mimi naona bado rais ana huruma ndiyo maana wanarudia rudia kutoa kauli za kuudhi. MHESHIMIWA RAIS MAGUFULI, NAOMBA UCHUKUE HATUA KALI ZAIDI DHIDI YA WATU WANAOTAKA KUFIFISHA JUHUDI ZAKO KATIKA KUIJENGA NCHI YETU. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MBARIKI RAIS MAGUFULI NA VIONGOZI WOTE WA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. AMINA.
 
Jenerali Ulimwengu Mzee huyu heshima kwake aliona mbali na aliitumia fursa kuwaambia 'Watukufu sana' ukweli uliopo kwa nyakati hizi ,pale alipoonesha matamanio ya kuondolewa kwa kinga ya kuwashitaki viongozi wa juu (kama Raisi) wastaafu..

Mfano ,anaweza kutumia madaraka yake vibaya kwa sababu yeyote ile huku akijua fika kuwa haokuja kushitakiwa kwa lolote lile..

Matokeo yaliyokwisha kuonekana na yanayoendelea kujidhihirisha ni mfano tosha ,makosa yenye dhamana kwa mtuhumiwa hawapewi dhamana..Hizi kauli za "Ni maagizo kutoka juu" ni alama tosha kuwa wanaotakiwa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa utaratibu hawafanyi hivyo bali hufanya kwa maagizo ya flani kutoka juuu...

Tunatengeneza chuki zinazo ubomoa umoja wetu kama Taifa ,wanacho jisahau watawala ni kuwa kwa wao kutofuata utaratibu wanawafundisha wale wanao ona wanaonewa isivyo nao kufikiria au kutenda kwa aina ile ile wanayo pimiwa..

Binadamu nae anazo hisia /anaumia kama wengine hawezi kuvumilia kama wanyama ,anacho kikomo cha uvumilivu kama vile walio juu wanavyo kuwa na kikomo cha uvumilvu..Nchi ni yetu sote tuujenge Umoja wetu kwa kila mmoja wetu kufuata Sheria hasa kuheshimu haki za msingi za wengine...

Nnawaza tu kwa sauti.....
 
1. Maendeleo hayaji kwa kudhibiti wanaohatarisha hali ya usalama kwa matamko unayoyadai. Hakuna utafiti wowote unaounga mkono unachokisema zaidi sana ni propaganda za kila siku za wasio na elimu kudai kuwa wapinzani wanahatarisha amani wakati haijawahi kutokea hata siku moja.

2. Ni uongo tena wa kitoto kudai kuwa wapinzani wanapinga kila kitu, labda kama unaweza kutoa ushahidi wa kudhihirisha hilo.

3. Vita ya Magufuli dhidi ya ufisadi kama unavyoinadi mpaka sasa imeonekana kuwa selective, yaani anachagua wapi apige hiyo vita. Kwa haraka haraka tu ni kwamba kashfa ya Lugumi ameiogopa na pia utakumbuka kuwa hajajibu lolote kuhusiana na boti ya kwenda Bagamoyo. Je, hii ndiyo vita yake dhidi ya ufisadi au ni yale yale ya mwenzie aliyemuachia nchi?

Kwa hali ilivyo sasa, ili kupiga hatua za maendeleo katika nchi yetu ni lazima kwanza rais awadhibiti wote wanaojaribu kuhatarisha hali ya usalama kwa matamko yasiyo na tija kwa maendeleo ya nchi yetu. Ifike mahala tuwe wakweli katika hili. Watu hawa wamekuwa hawana jema, kazi yao kubwa ni kupinga kila jambo linalofanywa na mheshimiwa rais Magufuli. Zaidi ya hayo wamekuwa wakitoa lugha za matusi na kejeli. Mtu waliyemwita fisadi kwa vinywa vyao leo hii kwao amekuwa mtakatifu, je watu hawa tuwaweke kwenye kundi gani? UFISADI ulipokuwa umeshamiri katika nchi hii walikaa kimya bila kuleta fyoko fyoko wala katangaza maandamano. Leo mheshimiwa rais Magufuli amejitahidi kwa kiasi kikubwa kupiga vita ufisadi, wao wanaanza kuleta fujo, kejeli na matusi. Je, watu hawa wana uchungu wowote juu ya nchi yetu? Mimi naona bado rais ana huruma ndiyo maana wanarudia rudia kutoa kauli za kuudhi. MHESHIMIWA RAIS MAGUFULI, NAOMBA UCHUKUE HATUA KALI ZAIDI DHIDI YA WATU WANAOTAKA KUFIFISHA JUHUDI ZAKO KATIKA KUIJENGA NCHI YETU. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MBARIKI RAIS MAGUFULI NA VIONGOZI WOTE WA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. AMINA.
 
Mada iko wazi: tuheshimu sheria na katiba. Kutii sheria bila shuruti ni wajibu ni wajibu wa kila mtu (raia, pokisi, nk). Vile vile kutoheshimu sheria au katiba kwa polisi kuwakandamiza wengine yakiwamo kuwakamata na kuwanyima dhamana kinyume cha sheria na katiba kufikia "si utii wa sheria bila shuruti -- huu ni utovu mkubwa aka jipu lililoiva sana linapaswa kutumbuliwa haraka si la kulea hata kidogo".

Kwa maana nyingine mkuu -- wanaotakiwa kutii sheria bila shuruti ni watu wote wakiwamo polisi pia.

Au wewe huoni hivyo?

Nchi hii itajengwa na sisi sote. Hebu isifike mahali wengine wakadhani wao ni bora zaidi. Sisi sote tu sawa mbele ya sheria na katiba mkuu. Hakuna aliye juu ya hapo.
Walioleta hiyo kauli mbiu hawalijui hilo wakiamini wao sheria haziwahusu
 
Back
Top Bottom