GE2025 Kamanda wa Polisi Morogoro, SACP Alex Mkama: Hatufanyi Mazoezi ili kutisha watu

GE2025 Kamanda wa Polisi Morogoro, SACP Alex Mkama: Hatufanyi Mazoezi ili kutisha watu

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Code zenu tunazijua wakuu na hamuwezi kufunguka maana tayari mmejawa woga kuhusu hatua inayofuata
Wananchi wamechoka ujinga unaoendelea

-------------
Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mkoani Morogoro leo Oktoba 18, 2025, yamefanya mazoezi ya pamoja yenye lengo la kuimarisha mshikamano, ushirikiano na utayari wa kulinda usalama wa wananchi na mali zao

Akizungumza wakati wa mazoezi hayo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, SACP Alex Mkama, amesema mazoezi hayo ni sehemu ya maandalizi ya kawaida na yanalenga kuongeza ufanisi wa vyombo vya ulinzi na usalama, siyo kuwatisha wananchi kama ambavyo baadhi ya watu wanavyodhani

Ameongeza kuwa ni muhimu kwa jamii kuelewa kuwa kuwepo kwa mazoezi hayo ni ishara ya utayari wa vyombo hivyo katika kukabiliana na changamoto za kiusalama, hususan kuelekea kipindi cha Uchaguzi Mkuu

Baadhi ya washiriki wameeleza kuwa mazoezi hayo yanasaidia pia katika kuimarisha afya ya miili yao, kuleta mshikamano miongoni mwa vikosi mbalimbali na kujenga ushirikiano imara, unaohitajika katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku

Soma pia GE2025 - Jeshi la polisi na vyombo vya ulinzi Morogoro limefanya mazoezi ya pamoja kuimarisha ushirikiano na usalama kwa jamii



Chanzo: Jambo TV
 
Wasichokijua nikwamba ,kutokea tokea kwao kwenye jamii iliyokuwa inawaogopa inawafanya waonekane wa kawaida .

Mimi nawasihi waendelee kufanya hayo mazoezi kila siku ili waisaidie jamii kuondoa uwoga waliyonao juu yao .

Kwa mara ya kwanza tangu uwepo wa Taifa letu tujiandae kuona askari wakichezea makofi kutoka kwa raia hapo 29_10_2025 .

Taifa let linaviongozi wapuuzi sana .

Mbinu iliyotumika zaidi ya miaka 40 huko wanataka iendelee kuwatisha watu hadi leo , nonsense.

Wasichokijua nikwamba , askari wanaheshimika ,hawaogopwi so ogopa sana kwenye eneo ambalo heshima imeondoshwa ndiyo tutacheka kichina dadadeeki.
 
Back
Top Bottom