Kamanda Kova anastaafu lini?

Nchi hii haiishi maajabu. Pesa ya kuwalipa vizuri waalimu na madaktari tunaowahitaji ni shida, lakini pesa ya kuongezewa mkataba polisi kama kova ambaye hata elimu yake hailingani na cheo alichonacho kwa dunia ya leo inapatikana.

Kielelezo cha matatizo tuliyonayo kwenye vipaumbele.
 
Mleta mada mbona hujatwambia wewe unastaafu lini kazini kwako
 
Ni kweli yaani hata nami baba mdogo kastaafu na cheo ACP alikuwa OC FFU ila kwa ana hali ngumu,hadi namhurumia.

maisha ya wastaafu wote serikalini huwa yapo hatarini baada ya kustaafu. tatizo kubwa linalowakumba ni kuwa, wana muda mrefu wa kuwatumikia watanzania huku wakisahau private life.

hawafanyi kazi nyingine nje ya ajira, matokeo yake kila anachofanya kwa kutumia pension, kinagoma. wanachakaa upesi
 
ASTAFU ILI WAPUMBAVU WAANDAMANE? hakuna hilo itabidi aongezewe miaka 2 tena
Mkuu nenda taratibu,Tambua kuwa si kila anayeandamana ni mwendawazimu,wanayo yao moyoni ambayo waliotakiwa kuwasikiliza hawakuwasikiliza ndipo wakaamua kuandamana;Ndio maana hata sheria za nchi hazikuweka zuio la Watu kuandamana ili kudai haki zao,Mkuu kwa kuwa bado unaishi usije ukamwita binadamu mwenzako anayedai haki zake Mpumbavu,Life is Dynamic,Leo kwangu Kesho kwako,Najua uko upande gani lkn huko uliko ni wataalamu wa kuwa-damp watu wao bila kujali michango yao,waangalie akina Warioba kidogo wale makonde sembuse wewe!!!,jiangalie.
 
Ni kweli yaani hata nami baba mdogo kastaafu na cheo ACP alikuwa OC FFU ila kwa ana hali ngumu,hadi namhurumia.
Kwa hiyo umeona umuanike Baba yako mdogo hapa???,kweli ubinadamu kazi,hapo ukute pesa zingine aliwahi kukunulia nguo au kukulipia Ada lkn leo unamwanika JF.
 
Bado nakumbuka alivyoshadadia kesi ya Jerry Muro. Muuza sura tu.
 
Wenye , kupenda kuona maji ya Washawasha yakiwaadhibu wapinzani basi nao watakutana na pilipili washa.
 
HAtimae kamanda Kova amestaafu rasmi leo tarehe 31 Dec 2015 tutakukumbuka kwa yale mema uliyofanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…