Unasemeje
JF-Expert Member
- Apr 29, 2021
- 249
- 915
Mwanaume kuna mambo hupaswi kufanyiwa na fundi;
1. Kubadili bulb: Yaani taa inaungua, wewe na mke wako mnaona suluhu ni kumwita fundi.
2. Kufunga screen ukutani: Acha uzembe, hilo ni jukumu lako, install app yoyote ya pima maji itakusaidia kunyoosha ili TV isipinde, kuna mtu anafunga TV inapinda utadhani kalazimishwa.
3. Kufunga dish: Unapigwaje pesa kizembe kufunga dish la ku band? Nunua sat finder ya dollar 7 tu zile manual itakusaidia hata ukiwa pekeyako unafunga, ikitokea changamoto yoyote unafix, sio wewe na mke wako mnaita fundi kwa case ya kijinga kama hii.
4. Kufyeka nyasi kuzunguka nyumba yako: Usijifanye uko busy sana mtoto wa kiume wewe, weekend itumie kurekebisha mazingira ya nyumba yako, fyeka, pogoa miti, reki nyasi nk.
5. Kuzibua sink la jikoni: Mke anakwambia baby sinki limeziba wewe akili yako inakutuma kwa fundi, alaah!
6. Kufix matatizo madogo madogo ya umeme: Matatizo kama kubadili fuse, kurekebisha extension, kubadili socket nayo mpaka uite fundi? Sasa topic ya Electricity ulijifunza ili iweje?
7. Kufunga mapazia: Unataka fundi aje chumbani kwako apande juu ya kitanda chako kukuwekea mapazia?
8. Kubadili oil kwenye gari lako na kufanya service ndogo ndogo: Ingia youtube jifunze acha uzembe wewe, ndomaana likitambi linaota sababu ya uzembe.
9. Kuosha gari hata mara 1 kwa mwezi: Fanya hivi watoto waige.
10. Kuendesha vyombo vya moto: Hakikisha unajua kuendesha gari na pikipiki, ikibidi uwe na leseni hata kama haumiliki hivyo vyombo.
NB: Mwanaume unapaswa kumiliki toolbox nyumbani kwako bila kusahau ngazi na vitendea kazi vingine.
Mfanye mke wako aone kuna mwanaume, usiwe mlegevu ukasingizia huna muda kumbe huna maarifa.
Unapomlipa fundi jua kuwa unalipia gharama ya ujinga wako, hakikisha fundi anakuja kwa suala ambalo hata yeye akija atahangaika.
1. Kubadili bulb: Yaani taa inaungua, wewe na mke wako mnaona suluhu ni kumwita fundi.
2. Kufunga screen ukutani: Acha uzembe, hilo ni jukumu lako, install app yoyote ya pima maji itakusaidia kunyoosha ili TV isipinde, kuna mtu anafunga TV inapinda utadhani kalazimishwa.
3. Kufunga dish: Unapigwaje pesa kizembe kufunga dish la ku band? Nunua sat finder ya dollar 7 tu zile manual itakusaidia hata ukiwa pekeyako unafunga, ikitokea changamoto yoyote unafix, sio wewe na mke wako mnaita fundi kwa case ya kijinga kama hii.
4. Kufyeka nyasi kuzunguka nyumba yako: Usijifanye uko busy sana mtoto wa kiume wewe, weekend itumie kurekebisha mazingira ya nyumba yako, fyeka, pogoa miti, reki nyasi nk.
5. Kuzibua sink la jikoni: Mke anakwambia baby sinki limeziba wewe akili yako inakutuma kwa fundi, alaah!
6. Kufix matatizo madogo madogo ya umeme: Matatizo kama kubadili fuse, kurekebisha extension, kubadili socket nayo mpaka uite fundi? Sasa topic ya Electricity ulijifunza ili iweje?
7. Kufunga mapazia: Unataka fundi aje chumbani kwako apande juu ya kitanda chako kukuwekea mapazia?
8. Kubadili oil kwenye gari lako na kufanya service ndogo ndogo: Ingia youtube jifunze acha uzembe wewe, ndomaana likitambi linaota sababu ya uzembe.
9. Kuosha gari hata mara 1 kwa mwezi: Fanya hivi watoto waige.
10. Kuendesha vyombo vya moto: Hakikisha unajua kuendesha gari na pikipiki, ikibidi uwe na leseni hata kama haumiliki hivyo vyombo.
NB: Mwanaume unapaswa kumiliki toolbox nyumbani kwako bila kusahau ngazi na vitendea kazi vingine.
Mfanye mke wako aone kuna mwanaume, usiwe mlegevu ukasingizia huna muda kumbe huna maarifa.
Unapomlipa fundi jua kuwa unalipia gharama ya ujinga wako, hakikisha fundi anakuja kwa suala ambalo hata yeye akija atahangaika.