Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 844
- 1,604
Kutokana na changamoto kubwa ya upatikanaji wa ajira na mitaji ya kujiajiri hapa nchini, ninaomba Serikali iangalie upya sera ya mafao ya NSSF na kurejesha rasmi Fao la Kujitoa kwa Wafanyakazi wanaoachishwa kazi au ambao mikataba yao imekoma katika sekta binafsi.
Kwa mujibu wa mfumo wa sasa, mfanyakazi aliyeachishwa kazi analipwa 33% ya mshahara wake kwa miezi 6 kama Fao la Kukosa Ajira. Baada ya hapo hulazimika kusubiri miezi 18 kabla ya kupewa salio la michango yake – ikiwa hajapata ajira nyingine.
Changamoto kubwa ni kwamba NSSF wala Serikali hawatoi msaada wowote wa ajira katika kipindi hiki cha kusubiri, hivyo wahanga wengi huishia katika hali ngumu ya kiuchumi bila mtaji, bila kipato na bila matumaini.
Pendekezo langu ni:
NSSF iwe na mfumo unaompa mwanachama uhuru wa kuchagua kati ya:
1. Kulipwa Fao la Kujitoa kwa mkupuo (kiasi chote cha michango yake), au
2. Kuendelea na utaratibu wa sasa wa Fao la Kukosa Ajira.
Ni ukweli mchungu kwamba vijana wengi wenye elimu ya juu ndiyo wanaathirika zaidi na mfumo huu, hali inayowafanya wengine hadi kuficha viwango vya elimu yao ili wapate michango yao. Kadri muda unavyosonga, ndivyo inavyokuwa vigumu zaidi kupata ajira mpya kutokana na ushindani mkubwa wa wahitimu wanaoingia sokoni kila mwaka.
Kwa kuwa Serikali yenyewe inahamasisha suala la kujiajiri, basi ni busara Fao la Kujitoa lirejeshwe ili liwe chanzo cha mtaji wa kuanzisha biashara na miradi midogo midogo.
NSSF pia inaweza kupata uhalisia wa tatizo hili kwa kuhoji wanachama waliolipwa au wanaolipwa Fao la Kukosa Ajira – wengi wao wangethibitisha kuwa kupata fedha zao kwa mkupuo ndilo chaguo lenye tija zaidi.
Inashangaza kuona wabunge – ambao ndio watungaji wa sera hizi – wao hulipwa mafao yao yote mara tu baada ya Bunge kuvunjwa, badala ya kupewa kidogo kidogo kama "Fao la Kukosa Ubunge." Hii ni dhihirisho la wazi kwamba sera hii inawabana wananchi wa kawaida pekee na si viongozi.
Ikiwa sera hii ilikopwa kutoka nchi za nje, basi hakika ilibebwa kutoka mazingira yenye urahisi wa kupata ajira mpya – hali ambayo haipo Tanzania. Hapa kwetu ajira ni haba, na ushahidi upo wazi katika idadi kubwa ya vijana wanaoomba nafasi chache za kazi zinazotangazwa.
Kwa ufupi, Fao la Kujitoa lirejeshwe mara moja ili kusaidia wananchi waliopoteza ajira katika sekta binafsi waweze kujiajiri, kujikimu na kusaidia familia zao, badala ya kulazimishwa kuishi maisha ya kuombaomba wakati michango yao ipo NSSF.
Kwa mujibu wa mfumo wa sasa, mfanyakazi aliyeachishwa kazi analipwa 33% ya mshahara wake kwa miezi 6 kama Fao la Kukosa Ajira. Baada ya hapo hulazimika kusubiri miezi 18 kabla ya kupewa salio la michango yake – ikiwa hajapata ajira nyingine.
Pendekezo langu ni:
NSSF iwe na mfumo unaompa mwanachama uhuru wa kuchagua kati ya:
1. Kulipwa Fao la Kujitoa kwa mkupuo (kiasi chote cha michango yake), au
2. Kuendelea na utaratibu wa sasa wa Fao la Kukosa Ajira.
Ni ukweli mchungu kwamba vijana wengi wenye elimu ya juu ndiyo wanaathirika zaidi na mfumo huu, hali inayowafanya wengine hadi kuficha viwango vya elimu yao ili wapate michango yao. Kadri muda unavyosonga, ndivyo inavyokuwa vigumu zaidi kupata ajira mpya kutokana na ushindani mkubwa wa wahitimu wanaoingia sokoni kila mwaka.
Kwa kuwa Serikali yenyewe inahamasisha suala la kujiajiri, basi ni busara Fao la Kujitoa lirejeshwe ili liwe chanzo cha mtaji wa kuanzisha biashara na miradi midogo midogo.
NSSF pia inaweza kupata uhalisia wa tatizo hili kwa kuhoji wanachama waliolipwa au wanaolipwa Fao la Kukosa Ajira – wengi wao wangethibitisha kuwa kupata fedha zao kwa mkupuo ndilo chaguo lenye tija zaidi.
Inashangaza kuona wabunge – ambao ndio watungaji wa sera hizi – wao hulipwa mafao yao yote mara tu baada ya Bunge kuvunjwa, badala ya kupewa kidogo kidogo kama "Fao la Kukosa Ubunge." Hii ni dhihirisho la wazi kwamba sera hii inawabana wananchi wa kawaida pekee na si viongozi.
Ikiwa sera hii ilikopwa kutoka nchi za nje, basi hakika ilibebwa kutoka mazingira yenye urahisi wa kupata ajira mpya – hali ambayo haipo Tanzania. Hapa kwetu ajira ni haba, na ushahidi upo wazi katika idadi kubwa ya vijana wanaoomba nafasi chache za kazi zinazotangazwa.
Kwa ufupi, Fao la Kujitoa lirejeshwe mara moja ili kusaidia wananchi waliopoteza ajira katika sekta binafsi waweze kujiajiri, kujikimu na kusaidia familia zao, badala ya kulazimishwa kuishi maisha ya kuombaomba wakati michango yao ipo NSSF.