Kwa hii thread yako nimekubali hlo ni funzoNikiwa form 3 nilianzisha uhusiano na binti yupo form 1. Huyu binti alikua na X wake ambaye yupo form 2, wote tupo shule moja.
Yeye na ex wake walisoma primary pamoja ila jamaa alivyofaulu kuja seco akamtema binti.
Anyway, mapenzi na mimi yakanoga shule nzima ikajua. Nilikua na mashati 3 ya shule, kuna siku alinikumbatia lile shati nililovaa siku ananikimbatia sikulifua nililificha kwenye sanduku, nikimmiss nanusa shati.
Uhusiano ulikua hot mbaya, yaani ilikua siku za mitihani mmoja akimaliza mtihani anaenda kuzengea darasa la mwenzake, na mwenzake akiona tu kua partner kashamaliza na yeye anatoka muda huo huo regardless kamaliza pepa ama la.
Basi siku ikafika ilikua Alhamisi, kipindi cha mitihani, naangalia dirishani naona mchumba yuko nje tayari, nikakusanya pepa hata sijamaliza maswali nikatoka nje. Tukapiga stori mbili tatu kisha akaniambia kuna kitu ataniambia j3 tukimaliza pepa.
Nikakomaa aniambie siku hiyo, akajibu kesho ni pepa, nikamjibu kiingereza hakinisumbui aseme tu.
Akaniuliza "Unaonaje tukiachana?" Nikauliza "Hiki ndiyo ulitaka kuniambia?" Akajibu "Ndiyo"
Nikapiga magoti. Hapo tupo Sinza Kijiweni. Tupo Sinza Kijiweni na sare za shule ila mimi nikapiga magoti huku napigana na machozi yasitoke kumanina. Binti akageuka upande mwingine hata kuniangalia hataki.
Hasira zikanikaba nikainuka nikaingia ndani ya gari. Ghafla mshkaji wangu anaingia ndani ya gari ananiambia "Castr umepanda gari la Msasani" mimi ninaishi Mwananyamala wazee, kushuka nikashindwa.
Nikarudi nyumbani, lile shati nikafua.
Manina, hii ilikua ni break up iliyonijenga mno. Alhamisi nikatemwa. Jumamosi ombi langu kwa binti mmoja hata humu namuona likagonga mwamba.
Nilikua shit si kipolepole.
Binti aliitwa Mwanne.
Pole mkuu... Najua itakuwa uliumia kinoma. Pole sana...!!!Daaaaah! Uzi huu umenikumbusha kitambo mno,,,,baada yakupigana na mdume mwenzangu kwakumuona anamfatilia xana manziyangu"""basi tulifumuana kinyama ila mwisho wapicha tukapelekwa kwamjumbe**mjumbe alifanya uwamuzi wakumuita manzi ili aamuwe ile kesi kwaulahisi ili yeye mjumbe asiumize kichwa,,,,,bhana weeeee manzi kaitwa front aeleze nani true boy wakesiakamtaja yule mdume mwenzangu kuwa ndo true boy wake, kwaiyo mm nikaonekana,tokea hapo nikaapa kutokuja kufanya tena ushujaa kama huo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu simu yako ndo majanga. Ama network yakoJF ya sasa inakera kama nini, unascrol page moja tu comments zingine hazionekani. Kama mnataka kuifunga si muifunge tu tujue imeisha
Huu ungese sasa....kweli huyo ni ng'ombeNoma sana.
Mimi nimeachwa last week siku ya Valentine's. Binti yupo mkoani mimi nipo Dar, katuma picha ya gauni jekundu nimnunulie anataka kuvaa hyo siku ya Valentine anadai ni birthday ya rafiki yake. Nkagoma.
Nusu saa si nyingi zikaingia texts za kibuti. Ndo ntolee hadi leo.
Ng'ombe nyingine tumeachana jana asubuhi, huyu alikua ni just for sex na yeye alikua analijua hilo. Juzi usiku anasema anahisi ana mimba tumeenda kupima jana asubuhi kweli anayo, lakini kwa wiki za hyo mimba kipindi inatungwa mimi sikuonana nae kabisa, manake sio yangu. Nkambana kasema alimpelekea uchi ex wake eti ilikua birthday yake. Imebidi nijisogeze pembeni wapambane
Nakumbuka mi nliachwa July 2019 kwa Phone call. Kwa kweli nilimpenda sana yule binti na kwa muda mfupi nlokua naye alinichuna lakini mi nlichukulia poa kwa sababu nlimpenda saaaaaana
Baada ya kumpiga sound, Nilimsafirisha toka Dar kuja Arusha, bata mbili tatu na baadae nkamrudisha Dar huko huko kuna hela kanikopa ila hata nguvu ya kumdai sina
Akaanza kutopokea simu zangu, hajibu text, ndo ikawa nimepewa silent treatment iyooo na baadae breakup phone call
Aiseeeee nilivyokua na mipango naye nkaona kama ndoto zangu zooote zimezimika ghafla, nikaugua Insomnia, depression na anxiety juuu!
Mpaka sasa hivi bado naendelea ku-recover ila daaaaaa kuna wanawake wanajua kutu-take for granted
One day Yes!!!!
Sent using Jamii Forums mobile app
Kunaviumbe mna hekaya et “mpaka nikihema nahisi kila punzi inatoka na jina lake..." you made mya day chiefBora wewe umeliona na kulikubali...nilimpenda yule manzi..yani mpaka nikihema nahisi kila punzi inatoka na jina lake...cjawah kupenda hivyo...
Me: hey love, morning!
Her: Hammy, naomba leo iwe mwisho kuwasiliana. Nimepata mtu hapa job na tunapendana sana. Naomba usinitafute tena.
Me: sawa, ukinihitaji nipo.
Her: never.
Me: okay
After 3 weeks
Her: hammy mpnz
Me: ......
Her: I am sorry
Me: .....
4th week
Her: hammy naomba unisamehe hata kama haunitaki, najua nlikuumiza. Pls
Me: okay
Nlishamsamehe... ila sijamrudia.
Mi niliacha kimasihara na beby wangu mpk leo bado nampenda ,
Ujinga ulikuwa wangu kuna maneno ya chumban niliyatoa nikasimulia mashoga zangu mtaaani
Basi alivyoyasikia wala hakuniuliza alichofanya ....akasubirj nimemaliza kula , tukaenda kuoga , akanigonga na kimoja tukarudi citing room
Akaniambia beby kuanzia leo mm na ww bac its over tabia yako nimekuonya lakini hutaki kuziacha kweli kwa kipindi kile nilikuwa na tabia za uwongo uwongo
Yaani sikuamini alinifukuza nikagoma kutoka akaniwasha vibao ndio nikajua kuwa yupo serious , nilichezea vitasa nikajikuta nimetoka ndani akanionea huruma
Akwasha gari yake mpk gheton kwangu sikuamini yaani akanisindikiza mpk ndani na maji ya kunywa akaniomba nikampa akanywa akasema maisha mema nilioma kama ndoto
Nililiiia nakumbuka ndio naujauzito wake mchanga , jamaa alikuwa haaamini kbs km nina ujauzito kutoka na tabia za kumdanganya mambo mengi
Mpk niliugua haipertension , ujauzito ukatoka !! Nikabaki kuwa naonana naye kazini
Mpk sasa nampenda japo yupo relation nyingine ila natamani sana abadili msimamo na mawazo yake , sikuwah kupata mwaume kama D wangu
Sio hekima ,busara,kutunza anajali kwenye game ndio usiseme mpk kiu ya maji inakukamata
Najilaumu sana ila ndiyo imetokea japo huwa na mmmisi sana
Sent using Jamii Forums mobile app
Wee jamaa bandidu sanaMimi Kuna manzi mmoja aliniacha kimasihara Sana. Yaani siku iyo alinipigia simu nikamwelekeza nilipokuwa nagonga mtungi. Akaja na jamaa ambaye kwangu alikuwa NI mkubwa kidogo.
Basi wakajoin. Jamaa akawa anasimamia bill zote pale. Mwisho wa siku manzi akaniambia - ujue kawoli hii ndio itakuwa mwisho wa Mimi na wewe kunywa pamoja Kama hivi. Huyu hapa NI Mr T ndio mpenzi wangu mpya nimeona Bora nikutambulishe ili tuachane kwa amani.
Nikaumuuliza tu yule manzi kama Kuna tatizo lolote labda, akajibu Hakuna. Nikamuuliza na Mr T Kama anampenda jwa dhati yule manzi, akajibu Sanaa.
Nikamwambia manzi awe na amani ila Mimi nitakaa Kama miezi sita hivi ndio nitaangalia uwezekano wa kuwa na mahusiano mengine. Ikawa tumeishia hivyo.
Walivokuwa wanaingia kwenye ndinga ya jamaa ili wasepe nikafanya ukauzu kidogo, nikawauliza Sasa mnaniachaje achaje hapa maana ndio kwanza kunaanza kuchangamka.
Basi Mr T kwa mbwembwe akanifata na kunishikisha lakimoja na akaniambia, I have never meet such a nigga in my entire life. Nikamwambia be blessed coz u are lucky to meet me today.
Wakasepa. Ile laki nikaichana yote pale pale na wahuhudumu wa bar. Nikawa Mimi ndio doni.
Nikaja kuonana nae after couple of years akiwa tayari ameshaolewa lkn na mwanaume nwingine sio Mr T, na mm nikiwa kwenye pilika pilika za kuoa. Sikutaka hata kuuliza waliishia wapi kwenye mahusiano yao. Akanichangia elfu70. Maisha yakasonga.
Nlishamsamehe... ila sijamrudia.
DahNakumbuka Ilikuwa Mwaka Jana Mwezi Wa 6 Hivi...Nilikuwa Nimelala Zangu Mida Ya Mchana Mara Text Ikaingia...
"Samahani Sana Kwa Message Hii,Ila Itabidi Kulizika Hili Penzi,Najua Napoteza MTU Muhimu Sana But Ndo Hivyo Inabidi Tuachane Tu Kwani Siitaji Kuwa Na Mpenzi Tena Mpaka Hapo Baadae....!!
Kidume Nilivyomaliza Kuisoma Usingizi Ukaja Tena Nikalala....sikukumbuka Tena kama Nimeachwa!!!
JE, Ushawahi Kuachwa Kwa Message Wewe?