Tumefika nyakati ambapo:-
Unaahidiwa kuwa ukichagua upinzani, hutapata au kuletewa maendeleo
Kuweka bendera ya upinzani kwenye duka lako ndio chanzo cha kufungiwa biashara zako zote
Kuweka bango la mgombea wa upinzani ni kujitafutia dhahama
Kumsifia mpinzani, inaonekana ni sawa na kumtukana mtawala
Vyombo vyote vya habari havimtangazi mgombea wa upinzani live
Mawakala wa upinzani ndio wanaopitia taabu zote
Kumtangaza mpinzani kashinda ni marufuku iliyowekwa kitambo sana
Wagombea mbalimbali walioenguliwa, asilimia kubwa ni wa upinzani
Wanaharakati wanaosota magerezani, na kufukuzwa kwenye ofisi zao, wote wanamlengo wa upinzani
Viongozi wa dini wanaowasapoti wapinzani, wanashambuliwa vikali na wenzao
Wanamuziki maarufu na bongo movie, wote sasa wamewapa kisogo wapinzani kwa maslahi ya kazi zao
Viongozi wa upinzani, karibu wote wana kesi mahakamani na wengine wameshahukumiwa vifungo gerezani
Viongozi wa upinzani ndio wanaopigwa na kudhalilishwa bila hatua kuchukuliwa kwa wahusika
Hoja za wapinzani bungeni ndio zinazoongoza kwa kunyamazishwa
Kama upinzani ni uadui, basi tuufute, wote tuwe chama kimoja, tupendane kinafiki, maisha yaende. Hakuna anaefurahia kusikia mpinzani kafanyiwa hiki au kile kibaya, hakuna. Sasa ili tusifanyiane ubaya, basi tuufute usiwepo kisheria kabisaaaa.
NB: Yeyote atakaeshinda, iwe ni ACT, CCM au CHADEMA. Ukishashika dola, ushauri, chakwanza futa vyama vingi. Wote tubaki kwenye chama tawala basi.
Unaahidiwa kuwa ukichagua upinzani, hutapata au kuletewa maendeleo
Kuweka bendera ya upinzani kwenye duka lako ndio chanzo cha kufungiwa biashara zako zote
Kuweka bango la mgombea wa upinzani ni kujitafutia dhahama
Kumsifia mpinzani, inaonekana ni sawa na kumtukana mtawala
Vyombo vyote vya habari havimtangazi mgombea wa upinzani live
Mawakala wa upinzani ndio wanaopitia taabu zote
Kumtangaza mpinzani kashinda ni marufuku iliyowekwa kitambo sana
Wagombea mbalimbali walioenguliwa, asilimia kubwa ni wa upinzani
Wanaharakati wanaosota magerezani, na kufukuzwa kwenye ofisi zao, wote wanamlengo wa upinzani
Viongozi wa dini wanaowasapoti wapinzani, wanashambuliwa vikali na wenzao
Wanamuziki maarufu na bongo movie, wote sasa wamewapa kisogo wapinzani kwa maslahi ya kazi zao
Viongozi wa upinzani, karibu wote wana kesi mahakamani na wengine wameshahukumiwa vifungo gerezani
Viongozi wa upinzani ndio wanaopigwa na kudhalilishwa bila hatua kuchukuliwa kwa wahusika
Hoja za wapinzani bungeni ndio zinazoongoza kwa kunyamazishwa
Kama upinzani ni uadui, basi tuufute, wote tuwe chama kimoja, tupendane kinafiki, maisha yaende. Hakuna anaefurahia kusikia mpinzani kafanyiwa hiki au kile kibaya, hakuna. Sasa ili tusifanyiane ubaya, basi tuufute usiwepo kisheria kabisaaaa.
NB: Yeyote atakaeshinda, iwe ni ACT, CCM au CHADEMA. Ukishashika dola, ushauri, chakwanza futa vyama vingi. Wote tubaki kwenye chama tawala basi.