Mawaiba
JF-Expert Member
- Dec 11, 2011
- 417
- 150
Habari za wikiendi wanaJamii. Naomba msaada juu ya tatizo hii. Nimemtumia mtoto wangu pesa toka jana kupitia tigopesa. Cha ajabu ni kwamba mpaka leo hajapata meseji ya kupokea pesa, na hata balance yake haionyeshi kama kuna pesa imeingia. Kwa upande wangu pia hata meseji ya kuonyesha kama nimetuma pesa sijaipata, lakini salio linaonyesha kwamba pesa imetoka. Naomba msaada kama kuna anayejua jinsi ya kuwasiana na watu wa tigopesa anielekeze. Hapa nilipo hakuna ofisi za tigo, niko chaka sana.